Sunday, March 12, 2023

KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA IMEJIPANGA KIKAMILIFU KUISIMAMIA OFISI YA RAIS-UTUMISHI KUFIKIA MALENGO

 Na. James K. Mwanamyoto-Dodoma

Tarehe 12 Machi, 2023

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Florent Kyombo amesema kamati yake imejipanga kikamilifu kutekeleza wajibu wa kuisimamia, kuishauri na kuipa mwongozo sahihi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake ili ziweze kutoa mchango wenye tija katika maendeleo ya taifa na kufikia lengo la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mhe. Kyombo amesema hayo jijini Dodoma wakati wa kikao kazi cha kamati yake na viongozi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kilicholenga kuwasilisha muundo na majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kwa kamati hiyo.

Mhe. Kyombo amesisitiza kuwa, wajumbe wa kamati yake wako tayari kufanya kazi ya kuishauri ipasavyo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake ili kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuujenga Utumishi wa Umma unaowajibika kwa wananchi.

Aidha, Mhe. Kyombo ametoa wito kwa watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake, kila mmoja kwa nafasi yake kutimiza wajibu wake ili kuiwezesha kamati yake kutekeleza jukumu la kushauri na kusimamia vema utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake.

Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema watendaji wa ofisi yake wanategemea sana mwongozo wa Mwenyekiti na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawalaz, Katiba na Sheria utakaowawezesha kutekeza majukumu yao kikamilifu ili kufikia lengo la kuboresha utoaji huduma bora kwa wananchi kama ilivyokusudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria, Mhe. Florent Kyombo akiongoza kikao kazi cha kamati yake na viongozi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kilicholenga kuiwezesha kamati hiyo kupokea wasilisho la muundo na majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake.


Mhe. Yahaya Massare (aliyeinua mkono) akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na viongozi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kilicholenga kuiwezesha kamati hiyo kupokea wasilisho la muundo na majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa ufafanuzi wa muundo na majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na watendaji wa ofisi yake. 


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Abdullah Mwinyi akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi cha   Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na viongozi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kilicholenga kuiwezesha kamati hiyo kupokea wasilisho la muundo na majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake.

 

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Ahmed Ngwali akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na viongozi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kilicholenga kuiwezesha kamati hiyo kupokea wasilisho la muundo na majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Suleiman Zedi akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na viongozi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kilicholenga kuiwezesha kamati hiyo kupokea wasilisho la muundo na majukumu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akiwaongoza watendaji wa taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI kujibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete na Naibu Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Xavier Daudi wakipokea hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na watendaji wa ofisi yake.

 



 

No comments:

Post a Comment