Thursday, December 31, 2020

MHE. NDEJEMBI AENDELEA NA ZIARA YA KUJITAMBULISHA NA KUHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA TAASISI ZAKE


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na Watumishi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi Jijini Dodoma yenye lengo la kufahamiana na watumishi wa Taasisi hiyo na kuhimiza uwajibikaji. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga.



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)     Bw. Ladislaus Mwamanga alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi yake wakati wa ziara ya kikazi ya Mhe. Ndejembi aliyoifanya katika Taasisi hiyo Jijini Dodoma kwa lengo la kufahamiana na watumishi wa Mamlaka hiyo na kuhimiza uwajibikaji.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akisoma taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakati wa ziara yake ya kikazi katika taasisi hiyo yenye lengo la kufahamiana na watumishi wa Mamlaka hiyo na kuhimiza uwajibikaji. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga.

 

 

No comments:

Post a Comment