Sunday, February 24, 2019

SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI MCHANGO WA WATUMISHI WA UMMA KATIKA KULETA MAENDELEO YA NCHI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb), akisalimiana na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi kabla ya kuingia katika ukumbi wa halmashauri hiyo kuzungumza na watumishi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb), akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi (hawapo pichani) katika kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo. Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Rehema Madenge na kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga.
Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Manispaa ya Lindi.
Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga akitoa neno la shukrani baada ya kikao kazi kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) na watumishi wa halmashauri ya Manispaa ya Lindi kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo.


No comments:

Post a Comment