Tuesday, December 21, 2021

TASAF YAJENGA NYUMBA YA MGANGA KIJIJI CHA KAGONGO-KIGOMA KUWAWEZESHA WANANCHI KUPATA HUDUMA KWA WAKATI

Na. James K. Mwanamyoto-Kigoma

Tarehe 21 Desemba, 2021

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema TASAF imejenga nyumba ya Mganga katika Kijiji cha Kagongo, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa lengo la kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa wakati katika Zahanati ya kijiji hicho.

Akizungumza na wananchi na walengwa wa TASAF katika Kijiji cha Kagongo, Mhe. Mchengerwa amesema, ujenzi wa nyumba hiyo umewaondolea adha wananchi wa kijijiji hicho ya kuchelewa kupata huduma kwani Mganga aliyekuwa akiwahudumia alilazimika kusafiri takribani kilomita kumi kila siku ili kutoa huduma kwa wananchi wa kijiji hicho.

“Tumefanikisha ujenzi wa nyumba hii, Mganga anaishi hapa na huduma zinatolewa kwa wakati, hii ndio dhamira ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwasogezea huduma wananchi,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa, Serikali kupitia TASAF itaendelea kuboresha huduma za kijamii ili wananchi waweze kunufaika na huduma zinazotolewa na Serikali yao kama ambavyo Rais wa Awamu ya Sita, Mhe. Samia Suluhu Hassan amedhamiria.

Katika kuhakikisha dhamira hiyo inatekelezwa, Mhe. Mchengerwa amesema, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha za kutosha kuwezesha upatikanaji wa huduma za kijamii katika maeneo yote yenye uhitaji.

“Nataka niwatoe hofu Watanzania wenzangu waliokuwa wanafikiri mradi huu wa TASAF hautaendelea, napenda niwaambie kuwa, Rais wetu ametupatia kiasi cha shilingi trilioni 2.03 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya TASAF, hii ina maana kuwa, tutazifikia kaya zote maskini nchini ambazo hazikufikiwa na mpango katika awamu zilizopita,” Mhe. Mchengerwa ameongeza.

Mhe. Mchengerwa anaendelea na ziara ya kikazi mkoani Kigoma ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akimpongeza mlengwa wa TASAF, Bw. Luciano Miheze wa Kijiji cha Kagongo, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa matumizi mazuri ya ruzuku ya TASAF wakati wa  ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mkoa wa Kigoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akilakiwa na wananchi na walengwa wa TASAF wa Kijiji cha Kagongo, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Kigoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na wananchi na walengwa wa TASAF wa Kijiji cha Kagongo, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma mbele ya nyumba ya Mganga wa Zahanati ya Kijiji cha Kagongo iliyojengwa na TASAF, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mkoa wa Kigoma. 


Umati wa wananchi na walengwa wa TASAF wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mkoa wa Kigoma.



Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Emmanuel Macha akitoa salam za TASAF kwa walengwa wa TASAF wa Kijiji cha Kagongo wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Kigoma.

Baadhi ya wananchi na walengwa wa TASAF wa Kijiji cha Kagongo, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wakiwa kwenye mkutano wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati wa ziara ya kikazi ya Mhe. Mchengerwa ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Kigoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akisikiliza ushuhuda wa mlengwa wa TASAF, Bw. Luciano Miheze wa Kijiji cha Kagongo, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wakati akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mkoa wa Kigoma. 

 

No comments:

Post a Comment