Friday, December 17, 2021

MHE. RAIS SAMIA ANAENDELEZA FIKRA ZA BABA WA TAIFA ZA KUONDOA UMASKINI KUPITIA TASAF – Mhe. Mchengerwa


Na. James K. Mwanamyoto-Geita

Tarehe 17 Desemba, 2021

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema utekelezaji wa miradi ya TASAF unaohimizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan unaendeleza fikra za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere za kuondoa umaskini kwa Watanzania ili waweze kujitegemea.

Akizungumza na walengwa na wananchi wa Kijiji cha Kanyala mkoani Geita, Mhe. Mchengerwa amesema Mwalimu Nyerere aliamini taifa haliwezi kujikomboa na kujitawala kwa ufasaha iwapo kundi kubwa la Watanzania watakuwa tegemezi.

Kutokana na fikra za Baba wa Taifa, miradi ya TASAF ilibuniwa na Viongozi wa nchi waliotangulia na Mhe. Rais Samia alipoingia madarakani alitaka kuendeleza fikra hizo ili kuhakikisha kila Mtanzania anajikomboa kutoka kweye lindi la umaskini.

Mhe. Mchengerwa amesema miradi ya TASAF tangu ianze, ilitekelezwa kwa asilimia 70 tu ambapo maeneo mengi yakiwemo ya Mkoa wa Geita hayakuwepo kwenye mpango, lakini Mhe. Rais Samia amedhamiria kuziingiza kwenye mpango kaya zote zenye sifa zilizobakia ili ziweze kunufaika na mpango huo na kuhakikisha kila Mtanzania anajitegemea kwa kuinua uchumi wake.

“Hakuna kijiji, kitongoji, wilaya wala mkoa ambao hautaguswa na fedha ambazo Mhe. Rais anazitoa ili kuhakikisha kila Mtanzania anajitegemea, hivyo tutuwajengee uwezo, tuwakomboe katika uchumi wa mtu mmoja mmoja ili kuondoa umaskini,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Mhe. Mchengerwa yuko mkoani Geita kwenye ziara ya kikazi ya siku mbili yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma na kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na walengwa wa TASAF na wananchi wa Kijiji cha Kanyala wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Geita.


Umati wa walengwa wa TASAF na wananchi wa Kijiji cha Kanyala wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Geita.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Emmanuel Macha akizungumza na walengwa wa TASAF na wananchi wa Kijiji cha Kanyala kwenye ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Geita.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kanyala wanaodai kutoingizwa kwenye Mpango wa TASAF wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Geita.


Mratibu wa TASAF wa Halmashauri ya Mji-Geita, Bi. Upendo Kilonge akitekeleza maelekezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ya kuandika majina ya wananchi wa Kijiji cha Kanyala wanaodai kutoingizwa kwenye Mpango wa TASAF wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Geita.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akimpongeza mlengwa wa TASAF wa Kijiji cha Kanyala aliyetumia vizuri ruzuku yake kwa kufungua duka ili kumudu kuendesha maisha yake wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Geita.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akimsikiliza mlengwa wa TASAF wa Kijiji cha Kanyala aliyetumia vizuri ruzuku yake kujenga nyumba, choo bora na kuchimba kisima wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF mkoani Geita.


 

No comments:

Post a Comment