Na
Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe
17.11.2025
Katibu Mkuu Mkomi ameyasema
hayo leo tarehe 17/11/2025 alipokuwa akizungumza na watumishi wa Ofisi
anayoingoza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao
yanayofanyika katika eneo maalum la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Aidha, Bw. Mkomi amewaasa
Watumishi wa Umma kuendelea na uwajibikaji wenye kutoa huduma bora kwa wananchi
kwa kuzingatia misingi ya maadili inayowaongoza kama Uzalendo, Uaminifu na
Mteja kwanza ili kukidhi mahitaji ya wananchi na kuondoa tofauti zilizopo kati
ya serikali na wananchi kwa ustawi wa Taifa.
“Uwajibikaji na Amani ni vitu
vinavyoenda sambamba katika kujenga jamii bora na imara, kila mtumishi
anapotekeleza wajibu wake kwa dhati, hujenga
msingi mzuri wa amani kwa kuwa amani inahitaji ushirikiano wa pamoja katika
kutatua changamoto za wananchi na hivyo jamii kuwa na uwezo wa kukua na kuwa na
maendeleo endelevu” alisema Bw. Mkomi.
Awali akiwasilisha mafunzo
hayo, Mwezeshaji ambaye ni Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Polisi
Mkoa wa Dodoma ASP Christer Kayombo ameeleza sababu mbalimbali zinazopelekea
kuwepo kwa vitendo vinavyosababisha ukosefu wa amani, ikiwa ni pamoja na
upotoshaji kupitia mitandao ya kijamii, uvivu pamoja na watoto kukosa misingi
bora ya malezi wakiwa wadogo na hivyo kukua na hali ya ujasiri wa kufanya maovu
hayo bila hofu.
ASP Kayombo alihitimisha mafunzo
hayo kwa kutoa wito kwa Watumishi wa Umma na wananchi wote kwa ujumla kuungana
kwa sauti moja katika kuhamasisha amani ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya namna
ya kuepuka vitendo viovu vitakavyosababisha uvunjifu wa amani na kukemea
vitendo hivyo kwa maslahi ya Taifa.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa
Umma, SACP. Ibrahim Mahumi, akimshukuru Katibu Mkuu (kwa
niaba ya mapolisi wote waliopo Ofisi hiyo na watumishi wote) kwa kutoa fursa ya
kupata mafunzo hayo ya kila jumatatu kwa lengo la kuwajengea watumishi uwezo wa
kiutendaji katika majukumu yao ya kila siku baada ya mwezeshaji kuhitimisha mafunzo hayo yalifanyika
katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba Jijini Dodoma leo tarehe 17/11/2025.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kushoto) akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavery Daudi (wa tatu kulia) wakati wakiendelea na mafunzo ya kuwajengea watumishi uwezo ambayo hufanyika kila jumatatu, yaliyotolewa na Mwezeshaji ambaye ni Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Polisi Mkoa wa Dodoma ASP Christer Kayombo katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba Jijini Dodoma leo tarehe 17/11/2025.
Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
wakifuatilia mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo katika
utendaji wao ambayo hufanyika kila jumatatu katika eneo maalum lililopo kwenye
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma leo tarehe 17/11/2025.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyesimama
mbele) akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo katika eneo maalumu la kutolea
mafunzo ya kuwajengea uwezo baada ya mwezeshaji kuhitimisha mafunzo hayo leo tarehe 17/11/2025
Mtumba jijini Dodoma
Mwezeshaji
ambaye ni Mkuu
wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Polisi Mkoa wa Dodoma ASP Christer Kayombo
(aliyesimama
mbele) akitoa mafunzo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyolenga kuwajengea uwezo wa
kiutendaji ambayo yalifanyika katika eneo la Ofisi
hiyo lililopo Mtumba Jijini Dodoma leo
tarehe 17/11/2025.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa
Umma, SACP. Ibrahim Mahumi, akimshukuru Katibu Mkuu (kwa
niaba ya mapolisi wote waliopo Ofisi hiyo na watumishi wote) kwa kutoa fursa ya
kupata mafunzo hayo ya kila jumatatu kwa lengo la kuwajengea watumishi uwezo wa
kiutendaji katika majukumu yao ya kila siku baada ya mwezeshaji kuhitimisha mafunzo hayo yalifanyika
katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba Jijini Dodoma leo tarehe 17/11/2025.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Bw.Musa Magufuli akimshukuru mwezeshaji kwa mafunzo aliyoyatoa na kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi, ili aseme neno kwa niaba ya mapolisi wote waliopo Ofisi hiyo na watumishi wote kutokana na mafunzo hayo yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba Jijini Dodoma leo tarehe 17/11/2025
Mkuu
wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Polisi Mkoa wa Dodoma ASP Christer Kayombo
akiwaelezea
kwa vitendo watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI namna ya kujitetea ili
kujinasua wanapokutana na vitendo uonevu au vitakavyosababisha uvunjifu wa
amani leo tarehe 17/11/2025 katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba Jijini
Dodoma.
Baadhi ya wakurugenzi na wakurugenzi wasaidizi kutoka Idara na vitengo mbalimbali vya Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia mada iliyokuwa ikiendelea katika mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo katika utendaji wao ambayo hufanyika kila jumatatu katika eneo maalum lililopo kwenye Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma leo tarehe 17/11/2025.
Mkuu
wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Polisi Mkoa wa Dodoma ASP Christer Kayombo
(aliyesimama mbele) akitoa ufafanuzi wa namna ya kuepuka vishawishi
vitakavyosababisha kuwepo kwa vitendo vya uvunjifu wa amani,wakati akitoa
mafunzo hayo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma leo
tarehe 17/11/2025.
Mkuu wa Dawati la Jinsia na
Watoto kutoka Polisi Mkoa wa Dodoma ASP Christer Kayombo (aliyesimama mbele)
akiwaongoza watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuimba wimbo wa kukiri na
kuahidi uaminifu katika kuilinda na kutetea nchi ya Tanzania na maslahi yake leo
tarehe 17/11/2025 katika Ofisi hiyo iliyopo Mtumba
jijini Dodoma.

No comments:
Post a Comment