Tuesday, November 25, 2025

WATUMISHI WA UMMA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA WAISHUKURU SERIKALI KUANZISHA MRADI WA UJENZI WA MAKAZI NCHINI

Na. Veronica Mwafisi-Ruvuma

Tarehe 25 Novemba, 2025

Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Kilagano na Shule ya Sekondari Jenista Mhagama waliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea wameishukuru Serikali kupitia Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments kwa kuanzisha Mradi wa Ujenzi wa Makazi kwa Watumishi wa Umma nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Watumishi hao, Mkuu wa Shule ya Sekondari Jenista Mhagama, Bi. Felister Kulwambalo amesema, Watumishi wa Shule ya Sekondari Jenista Mhagama wanaishukuru Serikali kupitia timu hiyo kwa kusimamia, kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi huo na kuahidi watakapokabidhiwa tija ya utendaji kazi itaongezeka.

 “Tunaishukuru sana Serikali kwa kuona umuhimu wa kutujengea makazi bora, tunaahidi tutakapokabidhiwa rasmi nyumba hizi tija ya utendaji kazi itaongezeka sana, lakini pia adha ya watumishi kutoka umbali mrefu kuja katika eneo la kazi itapungua,” amesema Bi. Kulwambalo

Timu hiyo ya Wataalam imeongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute wakati wa ziara ya kikazi waliyoifanya kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma kwa lengo la kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma utakaosaidia kuondokana na changamoto ya makazi kwa watumishi hao ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mradi huo wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma kwa awamu ya kwanza umetekelezwa katika mikoa ya Dodoma, Singida, Lindi, Pwani na Ruvuma.


Mwonekano wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma lililopo katika Kituo cha Afya Kilagano, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.


Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akisisitiza jambo mara baada ya Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika Kituo cha Afya Kilagano, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma. 


Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji kutoka Watumishi Housing Investments, Bw. Paskali Massawe (aliyenyoosha mkono) akizungumza jambo wakati Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments ilipofika kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika Kituo cha Afya Kilagano, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti, Bi. Julieth Magambo.



Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (kulia) na Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji kutoka Watumishi Housing Investments, Bw. Paskali Massawe (kushoto) wakimsikiliza Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya Kilagano (katikati) mara baada ya timu hiyo kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika Kituo hicho kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.


Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha kidole) akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Jenista Mhagama, Bi. Felister Kulwambalo (wakwanza kushoto) wakati Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments ilipokuwa ikikagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika Shule hiyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.


Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bi. Julieth Magambo (aliyevaa miwani) akizungumza jambo wakati wa ziara ya Timu ya wataalam kutoka Ofisi hiyo, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika Kituo cha Afya Kilagano, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.



Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wakwanza kushoto), Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji kutoka Watumishi Housing Investments, Bw. Paskali Massawe (katikati) na Afisa Usimamizi wa Fedha kutoka Wizara ya fedha, Bw. Ezekiel Odipo (wakwanza kulia) wakizungumza jambo mara baada ya kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika Kituo cha Afya Kilagano, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments ikiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Shule ya Sekondari Jenista Mhagama mara baada ya timu hiyo kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika shule hiyo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma.


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments ikijadili jambo mara baada ya kukagua na kufanya tathmini ya mwisho ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma katika Shule ya Sekondari Jenista Mhagama, Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma. Wengine ni Walimu wa Shule hiyo.


 



 

No comments:

Post a Comment