Monday, November 24, 2025

MHE. RIDHIWANI KIKWETE ATEMBELEA TUME YA UTUMISHI WA UMMA, ATOA MAELEKEZO YA KUBORESHA UTENDAJI KWA USTAWI WA TAIFA

 

Na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 24 Novemba, 2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amefanya ziara ya kikazi Tume ya Utumishi wa umma na kutoa maelekezo mbalimbali ya kuboresha utendaji kwa ustawi wa taifa.

 

Mhe. Kikwete ametoa maelekezo hayo akiwa kwenye ziara yake ya kwanza katika Tume hiyo tangu alipoapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 18 Novemba, 2025 kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Pamoja na masuala mengine, Mhe. Kikwete ameilekeza Tume hiyo kuendelea kutenda haki katika kushughulikia Rufani na malalamiko ya Watumishi wa Umma na Mamlaka za Nidhamu. “Tutende haki, tusimame katika haki, lazima tuangalie katika utoaji haki, taratibu zizingatiwe, uchunguzi wa kina ufanyike kabla ya kumchukulia mtumishi hatua,” amesisitiza Mhe. Kikwete.

 Pia ameitaka Tume hiyo kuendelea kutoa nafasi kwa Warufani na Warufaniwa kufika na kusikilizwa mbele ya Tume kwa ajili ya kutoa ushahidi zaidi.

 

Mhe. Kikwete ameisisitiza Tume kuendelea kutoa Miongozo ya masuala ya Ajira na Nidhamu ambayo husaidia kuwa na tafsiri sahihi ya utekelezaji wa sheria katika Utumishi wa Umma.

 

Aidha, ameielekeza Tume hiyo kuendelea kufanya ukaguzi wa masuala ya Rasilimaliwatu na uzingatiaji wa Sheria katika Taasisi za Umma hususani kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mashirika ya Umma ili kuhakikisha Watumishi wa Umma wanapata haki zao kuanzia wanapoajiriwa hadi wanapostaafu.

 

Mhe. Kikwete ametoa wito kwa Tume hiyo kuwashauri waajiri kuweka mazingira wezeshi ya kufanya kazi (vitendea kazi, maslahi na miundo mbinu sahihi ya kufanya kazi) na kuhakikisha uwepo wa Mabaraza ya Wafanyakazi yaliyo hai na yanafanya kazi kwa mujibu wa Sheria.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akitaka ufafanuzi wa jambo wakati wa ziara ya Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete katika Ofisi za Tume ya Utumishi wa Umma leo tarehe 24 November,2025 Jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa tatu kulia) Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Umma wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi hiyo leo tarehe 24. Novemba, 2025 jijini Dodoma. Kulia kwake ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray na Kushoto kwake ni Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Bw. John Mbisso.


   Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akimsikiliza Waziri wa Ofisi hiyo Mh. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi hiyo leo tarehe 24. Novemba, 2025 jijini Dodoma

 Naibu Katibu Idara ya Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria katika Utumishi wa Umma Bi.Celina Maongezi akielezea jambo wakati wa ziara ya kikazi ya  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete katika Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Umma tarehe 24 November 2025

Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Bw. John Mbisso akifafanua kuhusu jukumu la Ofisi hiyo leo tarehe 24 November,2027 wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete tarehe 24. Novemba, 2025 jijini Dodoma

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wa kwanza kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (wa pili kushoto) wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwenye Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Umma tarehe 24. Novemba, 2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Umma katika ziara yake ya kikazi leo Tarehe 24, Novemba, 2025

1Menejimenti ya Watumishi wa Tume ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao katika ziara yake ya kikazi katika Ofisi hiyo leo jijini Dodoma.

1  Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray wakiwa wanamsubiri Waziri wa Ofisi hyo Mhe. Ridhiwani Kikwete kuwasili katika Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Umma ambapo alikuwa na ziara ya kikazi leo tarehe 24 November,2025 kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Umma katika ziara yake ya kikazi leo Tarehe 24, Novemba, 2025



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Menejimenti ya watumishi wa Tume ya Utumishi wa Umma (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi hiyo leo tarehe 24 Novemba, 2025 jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment