Monday, September 1, 2025

WATUMISHI WA OFISI YA RAIS - UTUMISHI WAPATIWA MAFUNZO JUU YA KUJITAMBUA

 

Na Eric Amani

Watumishi wa Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, leo Septemba 1, 2025 katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma wamepatiwa mafunzo ya kujitambua kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi na kuboresha utoaji wa huduma kwa umma.

Akizungumza baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo hayo, Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera amesema kuwa kujitambua ni msingi wa kila mtumishi kujua nafasi yake, uwezo wake na wajibu wake katika kuwahudumia wananchi kwa weledi na uadilifu.

Mafunzo hayo ambayo hufanyika kila Jumatatu ya wiki yameelezwa kuwa ni sehemu ya mkakati wa ofisi hiyo kuboresha utendaji kazi na kuwajengea uwezo watumishi wa umma katika maeneo ya mawasiliano, uongozi, ubunifu na uwajibikaji.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo Bi. Noela Bomani ameeleza kuwa kujitambua sio nguzo muhimu ya mafanikio ya mtu binafsi tu, bali ni ya taasisi, kwani humsaidia mtumishi wa umma kutambua nguvu na udhaifu wake, hivyo kuwezesha kufanya maamuzi sahihi ya kikazi na kijamii.

Mafunzo hayo yametoa msisitizo katika maeneo ya mawasiliano chanya, nidhamu ya kazi, kujenga mshikamano wa kikazi, ushirikiano ikiwa pamoja na kukuza thamani ya Taifa na utu. Aidha, watumishi wametakiwa kutumia uelewa walioupata ili kuongeza ari ya kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Cyrus Kapinga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera Leo Septemba 1,2025 akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo baada ya mafunzo ya kila jumatatu ya wiki ikiwa kwa watumisha hao kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.  
Sehemu ya Wakugrugenzi wa Ofisi ya Rais - UTUMISHI wakifatilia mafunzo ya kila Jumatatu ambapo mafunzo hayo hulenga kuwajenga watumishi wa umma kuwa bora katika utendaji kazi wao.


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikilizia Mwezeshaji Bi Noela akitoa mafunzo juu ya akili hisia Leo Sepetemba 1, 2025.

Mwezeshaji Bi. Noela Bomani Leo Septemba 1,2025 katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma   ametoa mafunzo kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais - UTUMISHI juu ya Kujitambua "SELF AWARENESS". 


Baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifatilia kwa umakini mafunzo kutoka kwa Mwezeshaji Kuhusu Kujitambua Leo Septemba 1, 2025 katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. 

Sehemu ya Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi na watumishi wa Ofisi ya Rais - UTUMISHI wakifatilia kwa kina Mafunzo ya Jumatatu ambayo hutolewa kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wao.  

No comments:

Post a Comment