Na
Eric Amani na Antonia Mbwambo, Mtumba Dodoma
Tarehe
24.09.2025
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi, leo Septemba 24, 2025 amepokea makombe ya ushindi
yaliyonyakuliwa na timu ya OfisI yake katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya
Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) 2025, yaliyofanyika
jijini Mwanza huku akisisitiza umuhimu wa michezo kwa Watumishi wa Umma nchini.
Akizungumza katika hafla fupi
iliyofanyika sehemu ya wazi ya Ofisi hiyo, Katibu Mkuu Bw. Mkomi amezipongeza
timu zote zilizoshiriki katika mashindano hayo ya SHIMIWI jijini Mwanza kwa
juhudi na uzalendo waliouonesha hadi kuibuka mabingwa katika michezo mbalimbali
ikiwemo mpira
wa miguu (wanaume) mabingwa nafasi ya kwanza, netiboli (wanawake)
nafasi ya tatu, mbio za baiskeli na mchezo wa “darts” walipata ushindi wa nafasi ya tatu kwa
jumla, aidha kwenye mbio za kupokeza mita 400 (Relay) mshindi wa kwanza kwa
wanawake na wa pili kwa wanaume.
Bw. Mkomi amesema ushindi huo
ni ishara ya mshikamano, nidhamu na mazoezi ya muda mrefu ya timu nzima.
Amesisitiza kuwa michezo si tu burudani, bali pia ni nyenzo muhimu ya
kuimarisha afya, mahusiano kazini na kuongeza ufanisi wa kazi.
“Michezo ni afya, hivyo
ninawahimiza Watumishi wa Umma msiache kushiriki michezo kwani afya zenu zikiwa
nzuri basi huduma zinatolewa kikamilifu kwa wananchi.” Amesisitiza na kuongeza
kuwa pamoja na kuimarisha afya, pia inaleta ushirikiano.
Amesema Ofisi yake imeweka
utaratibu wa watumishi kufanya mazoezi kila siku ya Jumanne na Alhamisi, hivyo
amewasisitiza watumishi hao kushiriki kikamilifu.
“Utaratibu wa kufanya mazoezi
kila Jumanne na Alhamisi tumeuweka makusudi ili kila mmoja ashiriki, hivyo
ukifika muda uliopangwa wa kuanza mazoezi wote tunatakiwa kuelekea kwenye
mazoezi,” ameongeza.
Pamoja na kuhimiza kushiriki
michezo, Katibu Mkuu Mkomi amewataka Watumishi wa Umma kujiepusha na tabia
zinazoharibu taswira ya Ofisi. “Haipendezi kuona mtumishi wa umma anafanya
mambo ya ajabu huko mtaani, sisi ni kioo, hivyo tunatakiwa kuwa mfano wa kuigwa
katika kuzingatia maadili ndani na nje ya ofisi," amesema.
Naye Kiongozi wa timu ya
UTUMISHI ambaye ni Afisa Tawala Mwandamizi wa Ofisi hiyo, Bw. Charles Shija kwa
niaba ya wanamichezo wote, alimshukuru Katibu Mkuu kwa kuwawezesha kushiriki
michezo hiyo na kupata ushindi.
Aidha, Bw. Shija pamoja na
wanamichezo hao walitumia fursa hiyo kumkabidhi Katibu Mkuu makombe hayo huku
wakiahidi kuendelea kujiimarisha zaidi katika michezo kwa ustawi wa taifa.
Katibu
Mkuu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wanne kutoka kushoto) akipokea kombe la mchezo
wa “Darts” kutoka kwa Mtumishi wa ofisi hiyo, Bi
Loveness Choga (watatu kutoka kulia) wakati wa hafla fupi ya kupokea makombe
hayo yaliyopatikana wakati wa mashindano ya michezo ya SHIMIWI.
Mwenyekiti wa Timu za Michezo mbalimbali
kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Charles
Shija akitoa maneno ya utangulizi kwa Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi
(hayupo pichani) kuhusu ushindi walioupata katika mashindano ya SHIMIWI.
Watumishi wa Ofisi ya Rais,
UTUMISHI wakiwa nje ya ofisi hiyo tayari kwa kupokea Makombe ya ushindi kutoka
kwa washiriki wa mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha ya mbio za kupokezana, darts
na mchezo wa baiskeli waliyoyapata katika mashindano ya SHIMIWI yaliyofanyika
jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Timu mbalimbali
za Michezo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Bw. Charles Shija akikabidhi Kombe la Ubingwa wa Mpira wa Miguu kwa Mgeni
Rasmi ambaye ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi wakati wa hafla fupi
iliyofanyika jijini Dodoma
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Bw. Juma Mkomi (aliyenyanyua kombe) akifurahia ushindi walioupata Watumishi
wanamichezo wa ofisi hiyo kwenye mashindano ya michezo ya SHIMIWI.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Bw. Juma Mkomi akifurahia pamoja na Wakurugenzi wa Idara na Vitengo, Watumishi
na timu ya michezo ya ofisi hiyo ushindi wa makombe waliyoyapata kwenye
mashindano ya michezo ya SHIMIWI.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya
pamoja na Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka katika ofisi hiyo na timu ya
washiriki wa michezo ya SHIMIWI mara baada kupokea makombe ya ushindi ya mashindano
ya michezo ya SHIMIWI.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (watano kutoka kulia) akipokea kombe la mchezo wa
Baiskeli kutoka kwa Mtumishi wa Ofisi hiyo, Bw. Hassan Ligoneko (wasita kutoka
kulia) wakati wa hafla fupi ya kupokea makombe ya ushindi ya mashindano ya
michezo ya SHIMIWI.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Bw. Juma Mkomi akiwa ameongozana na baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi hiyo mara
baada ya kupokea makombe ya ushindi ya mashindano ya michezo ya SHIMIWI.
Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
wakionyesha makombe ya ushindi kwa Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo
pichani) waliyoyapata katika mashindano ya michezo ya SHIMIWI.
Watumishi wa Ofisi ya Rais,
UTUMISHI wakiwa nje ya ofisi hiyo tayari kwa kupokea Makombe ya ushindi kutoka
kwa washiriki wa mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha ya mbio za kupokezana, darts
na mchezo wa baiskeli waliyoyapata katika mashindano ya SHIMIWI yaliyofanyika
jijini Mwanza.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Bw. Juma Mkomi (kulia) akiwa anateta jambo na Mkurugenzi Idara ya Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli (kushoto) wakati wa hafla fupi
ya kupokea makombe ya ushindi walioupata katika michezo ya SHIMIWI.
Mlezi wa Timu za michezo mbalimbali
kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi
Mwanadawa Nchemwa (watano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mgeni
Rasmi ambaye ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (watatu kutoka
kushoto) baada ya kukabidhi Kombe la Ushindi uliotokana na mchezo wa netiboli wakati
wakati wa mashindano ya SHIMIWI.
No comments:
Post a Comment