Monday, September 22, 2025

WADAU WASISITIZWA KUIBUA VIGEZO VITAKAVYOKUBALIKA KUFANYA TATHMINI YA MAHITAJI YA RASILIMALIWATU KATIKA ZOEZI LA KUSAFISHA TAARIFA KWENYE MFUMO WA e-MSAWAZO

Na. Antonia Mbwambo- Dodoma

Tarehe 22.09.2025

Ili kuhakikisha takwimu za mahitaji ya watumishi katika taasisi za umma zina uhalisia utakaowezesha maamuzi mbalimbali kuhusiana na rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeandaa mikakati itakayoboresha utekelezaji wa Mfumo wa e-Msawazo ikiwemo kujadili na kukubaliana na wadau wa Mfumo kuhusu vigezo vitakavyotumika katika kutathmini mahitaji ya watumishi zikiwemo Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Hayo yamesemwa leo tarehe 22.09.2025 jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cosmas Ngangaji wakati akimwakilisha Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kufungua kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Bw. Ngangaji amesema, Ofisi ya Rais-UTUMISHI inaendelea kuchukua hatua na kuhakikisha Mfumo wa e-Msawazo unaendelea kuwa nyenzo itakayowezesha Serikali kuwa na takwimu sahihi za Watumishi waliopo na wanaohitajika kwa masilahi ya taifa.

“Mfumo wa e-Msawazo unaendelea kuboreshwa ili taarifa zinazopatikana kupitia Mfumo zinaendelea kuwa sahihi zaidi kuwezesha maamuzi mbalimbali ya usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma.” Amesisitiza Bw. Ngangaji.

Bw. Ngangaji amewaelekeza washiriki wa kikao kazi hicho, kutumia vizuri fursa hiyo ili kupata vigezo vitakavyokubalika kufanya tathmini ya mahitaji vitakavyotumika katika zoezi la kusafisha taarifa kwenye Mfumo wa e-Msawazo katika Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa na kufanya e-Msawazo inakuwa na tija.

Akitoa neno la utangulizi, Mkurugenzi wa Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda amesema kikao kazi hicho ni mahususi kwa ajili ya wadau ili waweze kujadili tathmini ya mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma kwa lengo la kupata maoni toka kwa wadau hao na kuboresha mfumo huo katika Utumishi wa Umma kwa masilahi mapana ya taifa.  

“Tumepata matokeo ya tathmini, sasa kabla ya kuendelea na mchakato mwingine, tumeona ni vema tukakutana na wadau hawa, tumeanza na wadau wa OR -TAMISEMI kutokana na uwingi wa uwakilishi wao katika Utumishi wa Umma.” Ameongeza Bw. Kipanda

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki, Mwenyekiti wa kikao kazi hicho ambaye ni Afisa Rasilimaliwatu, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Bw. Shaban Duru ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa ili kupata matokeo tarajiwa kama ilivyokusudiwa.

Mgeni Rasmi Bw. Cosmas Ngangaji(aliyeshika daftari na Faili) akiwasili katika Ukumbi wa NAOT katika ufunguzi wa kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cosmas Ngangaji akitoa hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Ofisi za NAOT jijini Dodoma.

Mgeni Rasmi Bw. Cosmas Ngangaji ambaye ni Mkurugenzi wa Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI (wa pili kutoka kulia),akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda kutoka Ofisi hiyo, (wa kwanza kushoto) na Afisa Rasilimaliwatu, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Bw. Shaban Duru (wa kwanza kulia) kabla ya kufungua kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa . 

Mkurugenzi wa Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda Ofisi ya Rais UTUMISHI, akitoa neno la utangulizi katika kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kabla ya mgeni rasmi  kufungua kikao hicho leo jijini Dodoma.

Mgeni Rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cosmas Ngangaji akitia saini kwenye kitabu cha wageni katika Ofisi za NAOT Jijini Dodoma mara baada ya kuwasili katika Ofisi hizo kwa lengo la kufungua kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa 

Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais,UTUMISHI, wakipata picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Bw. Cosmas Ngangaji ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango katika Ofisi hiyo mara baada ya kufungua kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa jijini Dodoma

Baadhi wa wakurugenzi na washiriki wengine, wakifuatilia kikao kazi cha e- Msawazo wakati Mgeni Rasmi alipokuwa akitoa hotuba ya ufunguzi wa kikao hicho.

Wakurugenzi wasaidizi pamoja na wawezeshaji wa kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mara baada ya Mgeni Rasmi kufungua kikao hicho.

Washiriki kutoka Sekretarieti za Mikoa pamoja na Halmashauri ya jiji wakipata picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Bw. Cosmas Ngangaji mara baada ya kufungua kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa jijini Dodoma


Washiriki kutoka Halmashauri za Miji,Halmashauri za Wilaya na Halmashauri za manispaa wakipata picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Bw. Cosmas Ngangaji ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango katika Ofisi hiyo mara baada ya kufungua kikao kazi cha siku mbili cha wadau kujadili vigezo vitakavyotumika katika kusafisha takwimu za mahitaji ya Watumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa jijini Dodoma

Wadau kutoka Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wakifuatilia kikao kazi cha e- Msawazo kilichofanyika katika Ofisi za NAOT jijini Dodoma.

Wadau kutoka Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wakifuatilia kikao kazi cha e- Msawazo kilichofanyika katika Ofisi za NAOT jijini Dodoma.

Washiriki kutoka Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wakifuatilia kikao kazi cha e- Msawazo kilichofanyika katika Ofisi za NAOT jijini Dodoma.



No comments:

Post a Comment