Monday, September 29, 2025

WATUMISHI WATAKIWA KUJENGA IMANI KWA WANANCHI

Na. Mwandishi Wetu

“Wananchi wanaimani na utendaji wa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, hivyo hakuna budi kuilinda imani hiyo kwa kuendelea kutoa huduma bora kwa umma”.

Maneno hayo yamesemwa Bw. Paul Mashauri ambaye ni Mchumi na Mjasiliamali, Septemba 29, 2025 wakati akitoa mafunzo ya namna bora ya kuboresha utendaji wa Watumishi wa umma yaliyofanyika katika Jengo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma.

Aliongeza kuwa, kila mwananchi anatamani kupata huduma bora haraka na kwa wakati, hivyo watumishi wanatakiwa kuwathamini wananchi na kuwapa huduma wanayohitaji ndani ya muda mfupi ili kuongeza imani kwa Serikali.

“Ni kazi ya Watumishi wa Umma kutafsiri Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwa kutoa huduma bora kwa wananchi. Wananchi hawawezi kusoma nyaraka za mipango ya maendeleo ya nchi kwa upana wake isipokuwa ni jukumu la watumishi na wananchi wanataka kuona huduma bora tu” alifafanua Bw. Mashauri.

Kwa upande mwingine, Mtaalamu wa Epidemiolojia sehemu ya Magonjwa Yasiyoambukiza kutoka Wizara ya Afya Bw.Jofrey Mtewele aliwataka watumishi hao kuepuka visababishi na kuwa makini na magonjwa yasiyoambukiza kwa kuwa hapa Tanzania yanachangia vifo kwa asilimia 33.

Bw. Mtewele alitaja baadhi ya magonjwa hayo kuwa ni saratani, kisukari, ugonjwa wa mifumo ya upumuaji, moyo na mishipa ya damu.

Naye, Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga amewashukuru wawezeshaji hao Bw. Mashauri na Bw. Mtewele kwa kutoa mafunzo muafaka kwa watumishi wa ofisi hiyo na kuwaahidi kutekeleza kwa vitendo mafunzo hayo.

Aidha, Bw. Kapinga ametoa rai kwa watumishi wote kufanya uchunguzi wa afya zao mara kwa mara kwa kuwa magonjwa yaliyotajwa na wataalamu yapo na yanaweza kutibika.

Vilevile, Bw. Kapinga ametumia fursa hiyo kuwapongeza watumishi wa ofisi yake waliozaliwa mwezi Septemba na kuwatakia kila kheri katika maisha yao.

Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais - UTUMISHI wakifuatilia mada zilizowasilishwa na Wawezeshaji Bw. Paul Mashauri na Bw.Jofrey Mtewele (Hawapo pichani) kuhusu  namna ya kuboresha utendaji wa watumishi na magonjwa yasiyoambukiza mtawalia yaliyofanyika katika Jengo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma, Septemba 29, 2025.





Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais - UTUMISHI wakifuatilia mada zilizowasilishwa na Wawezeshaji Bw. Paul Mashauri na Bw.Jofrey Mtewele (Hawapo pichani) kuhusu  namna ya kuboresha utendaji wa watumishi na magonjwa yasiyoambukiza mtawalia yaliyofanyika katika Jengo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma, Septemba 29, 2025.

Mchumi na Mjasiliamali Bw. Paul Mashauri akiwasilisha mada kuhusu  namna ya kuboresha utendaji wa watumishi wakati wa mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI,. Mafunzo yamefanyika katika Jengo la  Utumishi Mtumba Jijini Dodoma, Septemba 29, 2025.



Mtaalamu wa Epidemiolojia sehemu ya Magonjwa Yasiyoambukiza kutoka Wizara ya Afya Bw.Jofrey Mtewele akiwasilisha mada kuhusu  namna ya kuepuka Magonjwa hayo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI. Mafunzo yamefanyika katika Jengo la  Utumishi Mtumba-Dodoma, Septemba 29, 2025.

Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia mada mbalimbali
 
Bi. Hulay Mpamka akiandaa keki kwa niamba ya watumishi wa Ofisi ya Rais UTUMISHI waliozaliwa Mwezi Septemba.


Kaimu Katibu Mkuu Bw. Syrus Kapinga akichukua kipande cha keki tayari kwa ajili ya kuwalisha watumishi waliozaliwa Mwezi Septemba.

 Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bi. Geva Mbughi ambaye anasherehekea siku ya kuzaliwa kwake.
 Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bi. Hulay Mpamka ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.
 Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bw. Imani Mtumbi ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bw. Innocent Kessy  ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akitoa nasaha kwa watumishi wa ofisi yake wanaoadhimisha siku ya kuzaliwa kwao mwezi septemba.

Keki Maalum kwa ajili ya Watumishi wa Ofisi ya Rais UTUMISHI wanaoadhimisha siku yao ya kuzaliwa mwezi Septemba.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bw. Kelvin Munubi ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bw. Lusanda Kokolo ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.
Watumishi wa Ofisi ya Rais UTUMISHI wakianda Keki Maalumu kwa ajili ya Watumishi wa Ofisi hiyo waliozaliwa mwezi Septemba.

 


Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bi. Mariana Kihaya ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bw. Rashid Shedafa ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bw. Sospeter Tundura ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bw. Ally Ngowo ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bi.Aveline Ilahuka ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akimlisha keki Bi. Zulfa Makaso ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akilishwa Keki Bi. Aveline Ilahuka kwa niaba ya watumishi wote waliozaliwa Mwezi Septemba kama ishara ya upendo.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI Bw. Syrus Kapinga akilishwa Keki Bw.Paul Mashauri kwa niaba ya Wawezeshaji ikiwa ni ishara ya upendo wa watumishi wote wa ofisi hiyo waliozaliwa Mwezi Septemba.
Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia hafla fupi ya kulishwa keki kwa watumishi wa ofisi hiyo waliozaliwa Mwezi Septemba.

Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia hafla fupi ya kulishwa keki kwa watumishi wa ofisi hiyo waliozaliwa Mwezi Septemba.

Wawezeshaji Bw. Paul Mashauri ambaye ni Mchumi na Mjasiliamali (Kulia) na Mtaalamu wa Epidemiolojia sehemu ya Magonjwa Yasiyoambukiza kutoka Wizara ya Afya Bw. Jofrey Mtewele wakifuatilia hafla fupi ya kuwapongeza watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI waliozaliwa mwezi Septemba, iliyofanyika katika Jengo la hiyo, Mtumba Dodoma, Septemba 29, 2025.

Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mwalibora Saidy (Wa Nne kutoka Kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi hiyo waliozaliwa mwezi Septemba, Septemba 29, 2025.


No comments:

Post a Comment