Na. Mwandishi Wetu- Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
George Simbachawene amemuelekeza Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi kuhakikisha barua za walioshinda usaili na kupangiwa
vituo vya kazi zinatolewa kwenye mikoa husika walikofanyia usaili
badala ya kuwalazimu kusafiri hadi jijini Dodoma
Sekretarieti ya Ajira kufuata barua hizo.
Amesema kitendo cha watumishi
hao wapya kupatiwa barua katika mikoa husika kitasaidia kupunguza
gharama, usumbufu pamoja na muda wanaoutumia kufika hadi Dodoma.
Mhe. Simbachawene
ametoa maelekezo hayo leo jijini Dodoma wakati akizinda Baraza la Wafanyakazi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Mhe. Simbachawene amefafanua kuwa unaweza ukakuta mwananchi amefaulu usaili Mkoa wa Kigoma anaifuata barua jijini Dodoma halafu pengine kapangiwa tena Mkoa
huo huo wa Kigoma au Lindi.
Mhe. Simbachawene
amesema hayo ni matumizi mabaya ya rasilimali za nchi, ikiwemo mwananchi mwenyewe pamoja
na fedha anazotumia.
“Hii si sawa kwani tunawasumbua wanachoka hata kabla
ya kuanza kazi, tuwahurumie, barua hizo wachukulie kwenye mikoa walikofanyia
usaili, tuwaamini Makatibu Tawala wetu, tunaamini wapo wataalam wenye maadili
wa kufanya kazi hiyo, hivyo tuwape
dhamana waifanye, Mhe. Simbachawene amesisitiza.
Amesema anatamani
kuona kwa mfano mwananchi aliyefanyia usaili katika Mkoa wa Rukwa anaifuata
barua yake katika Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa kisha anakwenda
pengine Kigoma alikopangiwa kazi na sio kwenda Dodoma kwanza.
Katika hatua nyingine, Mhe.
Simbachawene amemuelekeza Katibu Mkuu, UTUMISHI, kuandaa kituo cha pamoja (One Stop Centre) katika ofisi hiyo kwa lengo la kusikiliza
changamoto zinazowakabili Watumishi
wa Umma, ikiwa ni ubunifu wa kuzitafutia ufumbuzi changamoto
hizo papo kwa hapo kwa
Watumishi wenye changamoto za kiutumishi
wanaofika Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora zilizopo Mtumba jijini Dodoma.
Amesema Kituo hicho kinatakiwa
kiwe na Maafisa Waandamizi wa kila kada ikiwemo
wanasaikolojia nguli watakaohakikisha
mtumishi yeyote mwenye changamoto za kitumishi anayefika katika Kituo hicho
anapata ufumbuzi wa changamoto yake inayomkabili papo kwa hapo.
Amefafanua kuwa,
kituo hicho kitakuwa na mawasiliano ya
waajiriwa wote nchini hivyo mtumishi hatalazimika kurudi
tena mkoani kwake kurekebisha taarifa zake badala yake suluhu zote za changamoto alizo nazo zitapatikana hapo.
Amesema hali hiyo itapunguza msururu wa Watumishi
wanaotoka maeneo mbalimbali nchini ambapo kila mmoja akifika Ofisini hapo
anataka kumuona na Waziri au Katibu Mkuu.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bw.
Juma Mkomi ametumia fursa hiyo kumshukuru Waziri Simbachawene kwa
maelekezo aliyoyatoa na kwa ubunifu huo huku akimuahidi kuyatekeleza
kikamilifu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora,
Bw. Mhe. George Simbachawene
akizungumza wakati wa Mkutano Maalum wa
Baraza la Wafanyakazi la
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliofanyika
katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina
jijini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George
Simbachawene
(hayupo pichani) alipokuwa akizungumza katika Mkutano Maalum
wa Baraza hilo uliofanyika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza
la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora akiongoza Mkutano Maalum wa Baraza la Wafanyakazi la ofisi hiyo kabla ya Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George Simbachawene kuzindua
Baraza hilo.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala
Bora wakimsikiliza Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George Simbachawene
(hayupo pichani)
alipokuwa akizungumza katika
Mkutano Maalum wa Baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina jijini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora wakifuatilia hotuba ya
Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George Simbachawene
(hayupo pichani) alipokuwa akizungumza katika
Mkutano Maalum wa Baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina jijini
Dodoma.
Katibu Mstaafu wa Baraza la Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Rocky Setembo akitoa neno la shukrani baada ya
kumaliza muda wake katika kulitumikia Baraza hilo kwenye Mkutano Maalum wa Baraza la Wafanyakazi la
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliofanyika
katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina
jijini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora wakifuatilia hotuba ya
Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George Simbachawene
(hayupo pichani) alipokuwa akizungumza
Mkutano Maalum wa Baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina
jijini Dodoma.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza katika Mkutano Maalum wa Baraza hilo uliofanyika
katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina
jijini Dodoma.
Sehemu ya Wajumbe
wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora,
Bw. Mhe. George Simbachawene
(hayupo pichani) alipokuwa akizungumza katika Mkutano Maalum wa Baraza hilo uliofanyika
katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina
jijini Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa TUGHE Mkoa, Bw. Nsubisi Mwasandende.
Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George Simbachawene (katikati) akiwa katika picha
ya pamoja na sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora mara baada ya kuzindua Mkutano
Maalum wa Baraza hilo uliofanyika
katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina
jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mhe. George Simbachawene (katikati) akiwa katika picha
ya pamoja na sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora mara baada ya kuzindua Mkutano
Maalum wa Baraza hilo uliofanyika
katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina
jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora,
Bw. Mhe. George Simbachawene (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya
pamoja Viongozi wapya akiwemo Katibu wa Baraza la Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Mwendesha Mkandya
na Katibu Msaidizi, Bi. Catherine Massawe (kulia waliosimama) mara baada ya
kuzindua Mkutano Maalum
wa Baraza hilo uliofanyika
katika ukumbi wa Kambarage uliopo Hazina jijini Dodoma.
No comments:
Post a Comment