Amesema
ndoto ya Tanzania ijayo haiwezi kutimia bila uwepo wa chombo hicho.
Mhe.
Dkt. Mhagama ametoa kauli hiyo leo
Jumamosi Machi 15, 2025 wakati wa ziara ya Kamati
ya Kudumu ya Utawala, Katiba na Sheria ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la
TAKUKURU, Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro ambapo
amesisitiza kuwa suala la TAKUKURU kuwa na majengo yake ya kisasa ni jambo
lisiloepukika.
Amesema
Kamati hiyo iliamua kuweka kipaumbele cha kuhakikisha TAKUKURU inatekeleza
majukumu yake ipasavyo ambapo moja ya kipaumbele hicho ni TAKUKURU kuwa na majengo ya kisasa yatakayokuwa rafiki na
wezeshi katika kusimika vifaa vya kidijitali ili kurahisisha utendaji
kazi.
"Tumehakikisha
TAKUKURU inakuwa na majengo ya kisasa yenye hadhi na faragha ili
iweze kutimiza majukumu yake na sio majengo ya kupanga kama ilivyokuwa
mwanzo amesisitiza Mhe. Dkt. Mhagama.
Amesema
Kamati hiyo imeendelea kuipigania Taasisi hiyo ili iendelee
kuongezewa bajeti ya fedha kila mwaka.
Kufuatia
hatua hiyo Mhe. Dkt. Mhagama amesema
huo ni mwelekeo wa Serikali katika
kuhakikisha kuwa TAKUKURU inakuwa chombo huru,
chenye uwezo wa kutenda haki kwenye Taifa.
"Sisi
Wajumbe wa Kamati hii kwa pamoja
tunatoa pongezi zetu za dhati kwa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa
kusimama imara kwenye masuala ya rushwa katika
Uongozi wake " amesisitiza
Ameongeza
kuwa "TAKUKURU mnafanya kazi yetu ya Kamati kuwa nyepesi, sisi
Wanakamati tunajisikia fahari na heshima kwa jinsi mnavyowatendea
Watanzania, hakika tumeridhishwa sana na utendaji wenu"
Akizungumzia
kuhusu ujenzi wa jengo hilo, Mhe. Dkt.
Mhagama amesema Kamati yake imeridhishwa na ujenzi wa jengo hilo
huku akisisitiza kuwa thamani ya fedha inaonekana dhahiri kuanzia kwenye lango kuu hadi ndani ya jengo.
Kwa
upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu amesema utashi wa
kisiasa wa Rais Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan umeiwezesha TAKUKURU kupata vitendea kazi na
kutimiza majukumu yake kwenye mazingira
wezeshi.
Amesema
katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita zaidi ya Watumishi 1000
wameajiriwa na TAKUKURU, ikiwa ni jitihada za Rais Mhe.
Dkt. Samia Suluhu Hassan katika
kuiwezesha TAKUKURU.
Amesema
mbali na magari 88 TAKUKURU iliyowezeshwa,
inatarajia kwa mara nyingine tena kupokea jumla magari 100 ili
kuwawezesha maafisa hao kutekeleza majukumu yao mahali popote na saa yeyote
wanakohitajika.
Amesema
hiyo ni nia ya dhati ya Rais Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha TAKUKURU inakuwa ni chombo chenye uhalali katika jamii.
"Taasisi
yetu sio tu inaziangalia Taasisi nyingine
bali imekuwa mfano na kioo kwa Taasisi nyingine
katika kuonesha thamani halisi ya fedha iliyotumika katika ujenzi wa jengo hili
la Rombo" Mhe. Sangu amefafanua.
Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria imehitimisha ziara yake ya siku
tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mikoa ya Pwani, Tanga na
Kilimanjaro na kukagua mradi wa jengo la Ofisi ya TAKUKURU katika Halmashauri
ya Wilaya ya Rombo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro
Muonekano wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro ambapo Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria waliptembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akizungumza mara baada ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama (katikati) akiwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakipata maelezo ya miradi ya ujenzi wa majengo yanayojengwa katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini mara baada Wajumbe wa Kamati hiyo kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro
No comments:
Post a Comment