Wednesday, March 5, 2025

HABARI KATIKA PICHA: OFISI YA RAIS-UTUMISHI YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 2025

HABARI KATIKA PICHA:

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 2025 KATIKA VIWANJA VYA SHEIKH AMRI ABEID KARUME JIJINI ARUSHA KUANZIA TAREHE 01-8 MACHI, 2025

Baadhi ya wananchi waliotembelea Banda la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakitazama bango la Mwongozo wa  Mavazi kwa Utumishi wa Umma wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayofanyika katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha.


Afisa Sheria, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Richard Lugomela (wa kwanza kulia) akiwahudumia Watumishi wa Umma Wastaafu waliotembelea banda la Ofisi hiyo kwa lengo la kufuatilia taarifa zao za kustaafu wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayofanyika katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha.


Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimpatia vitabu vya Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma mwananchi aliyetembelea banda la Ofisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayofanyika katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha.


Wananchi mbalimbali wakipatiwa taarifa za Kiutumishi kutoka kwa Maafisa wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayofanyika katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment