Tuesday, August 2, 2016

KIKAO KAZI KUHUSU UTOAJI HUDUMA NA MATUMIZI YA TEHAMA SERIKALINI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (kulia) akimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro (aliyeinua mkono) alipokuwa akifafanua jambo wakati wa kikao kazi na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais- Utumishi kuhusu utoaji huduma na matumizi ya TEHAMA katika Utumishi wa Umma  kilichofanyika katika ukumbi wa utumishi leo, wa tatu kulia (mstari wa mbele) ni Naibu Katibu Mkuu Utumishi na Utawala Bora, Bi. Susan Mlawi.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akielekeza jambo kwa baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais Utumishi wakati wa kikao kazi kuhusu utoaji huduma na matumizi ya TEHAMA kilichofanyika katika ukumbi wa utumishi leo. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) na baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi wakijadili kuhusu matumizi ya TEHAMA katika utoaji huduma Serikalini wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa utumishi leo. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akimsikiliza Mkurugenzi wa TEHAMA katika Utumishi wa Umma, Bw. Priscus Kiwango wakati wa kikao kazi kuhusu utoaji huduma na matumizi ya TEHAMA katika Utumishi wa Umma kilichofanyika katika ukumbi wa utumishi leo. 

No comments:

Post a Comment