Monday, August 29, 2016

MHE. KAIRUKI AWATA WATUMISHI WA UMMA NCHINI KUJIJENGEA UWEZO KATIKA MAENEO YATAKAYO HARAKISHA MAENDELEO‏

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akitoa ufafanuzi wakati wa kipindi cha TUNATEKELEZA kilichorushwa na Runinga ya Taifa (TBC-1). Kushoto ni muongozaji kipindi hicho Bi. Eshe Muhidin.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akisisitiza jambo katika  kipindi cha TUNATEKELEZA kilichorushwa na Runinga ya Taifa (TBC-1). Mhe. Kairuki aliainisha kuwa wale wanaotarajia kuomba ajira Serikalini wawe na subira wakati zoezi la uhakiki wa taarifa za kiutumishi likikamilishwa. Kushoto ni muongozaji wa kipindi hicho  Bi. Eshe Muhidin waTBC. 

Muongozaji wa kipindi cha TUNATEKELEZA Bi. Eshe Muhidin (kushoto) akiuliza swali kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) wakati wa kipindi cha TUNATEKELEZA kilichorushwa na Runinga ya Taifa (TBC-1). Miongoni mwa aliyosema Mhe. Kairuki ni wito kwa Watumishi wa Umma kujiendeleza katika maeneo yenye tija kwa Taifa ili kufikia malengo ya nchi.

TUMEKAMILISHA: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Muongozaji wa kipindi cha TUNATEKELEZA Bi. Eshe Muhidin (kushoto) baada ya kukamilisha kurusha kipindi mmbashara (live) katika studio za Runinga ya Taifa TBC-1.

No comments:

Post a Comment