Thursday, August 4, 2016

UTUMISHI YATOA MAFUNZO YA KANZI DATA YA FOMU ZA SERIKALI


Serikali kupitia Ofisi ya Rais ,Menejimenti ya Utumishi wa Umma, imeendesha mafunzo ya Kanzidata ya Fomu za Serikali  yanayolenga kukabilina na changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika usimamizi wa fomu hizo.

Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw.Mick Kiliba akifungua mafunzo hayo katika Ukumbi wa Utumishi alisema kuwa mafunzo hayo  ni muhimu sana katika usimamizi wa Fomu za Serikali  na utoaji huduma  kwa ujumla .

 “Imebainika kuwa  zoezi zima la usimamizi wa Fomu za Serikali   lina  upungufu mkubwa katika usimamizi  ikiwa ni pamoja  taasisi kuibua fomu  mpya , kuhuisha  na kuanza kutumia bila ya ridhaa ya Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi Umma” Bw. Kiliba alisema.

Aliongeza “ Jukumu la usimamizi wa utendaji wa serikali liko chini ya  Ofisi ya Rais –Utumishi, Fomu za Serikali ni njia mojawapo ya kutekeleza jukumu hili  na hivyo uthibiti  wa fomu za serikali ni jambo muhimu kuzingatiwa .” Mkurugenzi Kiliba alisisitiza  na kusema kuwa katika uthibiti huo   General Orders ( G.O.C 48) imeelekeza kuwa mapendekezo  ya kuibua Fomu mpya   na kuhuisha  fomu zilizopo yapate  ushauri  na kibali  kutoka  Utumishi.

 Mkurugenzi  Kiliba aliendelea kufafanua kuwa  kuna taasisi za serikali zinaenda kinyume na taratibu kwa  kuibua na kutumia fomu tofauti  na zile zinazokubalika katika kutoka huduma  husika, kutumia fomu zilizopitwa na wakati  na kutotambua  idadi ya fomu zinazotumika katika taasisi husika  na kutosimamia ipasavyo.

 “ Katika ufuatiliaji  wa utekelezaji wa mifumo ya viwango vya utendaji  uliofanyika  Mei  mwaka 2015 na Mei 2016  katika Idara zinazojitegemea  na Wakala za Serikali  kiwango cha usimamizi  wa fomu za serikali  ni wastani wa asilimia 27 na 53 “ Mkurugenzi Kiliba aliainisha.

 Alisema kutokana na hali hiyo, Serikali imeona ipo haja  ya kuwa na Kanzidata ya Fomu za Serikali (Government Forms Database) itakayosaidia kuweka kumbukumbu muhimu  na kuratibu  usimamizi  wa Fomu ili kufikia azma ya kuleta ufanisi katika utendaji serikalini.
Akitoa mafunzo hayo kwa washiriki kutoka katika taasisi mbalimbali za Serikali Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi,  Sehemu ya Mifumo  na Viwango  vya Utendaji Kazi – Utumishi Bi.Veila Shoo alisema kuwa Fomu hizo za serikali ni zile ambazo hutumika  kukamilisha taratibu mbalimbali  za kiutumishi na usimamizi wa fedha katika Utumishi wa Umma .


 Mafunzo hayo  ya siku moja yamehudhuriwa na  wawakilishi wa wizara  zote Serikali 

No comments:

Post a Comment