Monday, July 3, 2023

WAZIRI MKUU, MHE. KASSIM MAJALIWA ARIDHISHWA NA OFISI YA RAIS-UTUMISHI KWA KUFIKISHA ASILIMIA 88 YA UJENZI WA JENGO LA OFISI, MTUMBA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ameridhishwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kufikisha asilimia 88 ya ujenzi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma. 

Akitoa pongezi hizo leo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi za Serikali zinazoendelea kujengwa katika Mji huo wa Serikali, Waziri Mkuu Majaliwa amesema  ujenzi wa jengo hilo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI, umefikia hatua nzuri huku akisisitiza kuwa ifikapo mwezi wa 10, 2023  jengo hilo liwe limekamilika ikiwemo  mindombinu ya maji na umeme.                    

"Nataka ifikapo mwezi Novemba na Disemba mwaka huu, muwe mmekamilisha hatua ya kununua vifaa vya ofisi, wakati mnaendelea kukamilisha ujenzi, anzeni kutangaza zabuni kwa ajili ya kupata vifaa hivyo ili ifikapo Januari 1, 2024 Watumishi wote wawe kwenye jengo moja" amesisitiza Majaliwa. 

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa amewasisitiza Viongozi na Watendaji wa Ofisi hiyo kuhakikisha wanatembelea katika jengo hilo mara kwa mara kwa ajili ya  kukagua  ili kujua kila hatua inayoendelea kwa lengo la kukamilisha kwa wakati ujenzi. 

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuiwezesha Ofisi hiyo kwa hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa jengo hilo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza mara baada ya kuwasili katika jengo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambalo limefikia asilimia 88 ya ujenzi wake katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akisalimiana na baadhi ya viongozi mara baada ya kuwasili katika jengo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambalo limefikia asilimia 88 ya ujenzi wake katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akimuelezea hatua ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ilipofikia.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwan Kikwete akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Daudi Kondoro wakati wakimsubiri Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa kukagua jengo hilo katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wake Bw. Xavier Daudi wakati wakimsubiri Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa kukagua jengo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa ameongoza na Naibu Waziri wake Mhe.Ridhiwan Kikwete wakati wakikagua hatua ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambalo limefikia asilimia 88 ya ujenzi wake katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma.


Muonekano wa jengo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambalo limefikia asilimia 88 ya ujenzi wake katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma






   

No comments:

Post a Comment