Friday, October 28, 2022

MAKTABA YA UONGOZI KUCHOCHEA UWAJIBIKAJI WA VIONGOZI KATIKA KULITUMIKIA TAIFA - Mhe. Jenista

Na. James K. Mwanamyoto-Dar es Salaam

Tarehe 28 Oktoba, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amesema viongozi walio katika Taasisi za Umma na Sekta Binafsi wakijenga utamaduni wa kusoma vitabu mbalimbali watapata elimu na maarifa yatakayowawezesha kuwajibika kikamilifu katika kuwahudumia wananchi na kulitumikia taifa. 

Mhe. Jenisa amesema hayo jijini Dar es Salaam, wakati akizindua Maktaba ya Uongozi iliyoanzishwa na Taasisi ya UONGOZI kwa lengo la kuwajengea uwezo viongozi walio katika sekta ya umma na sekta binafsi nchini. 

Mhe. Jenista amesema kuwa, maktaba hiyo ya uongozi ikitumiwa vizuri itakuwa ni kituo muhimu cha kuchochea uwajibikaji wa viongozi katika taifa kwani maudhui watakayoyasoma kupitia vitabu mbalimbali yatawapatia maarifa yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kikamilifu. 

“Ninakubaliana na wale wanaoamini kwamba msomaji wa vitabu akipata fursa ya kusoma vitabu anaongeza wigo wa kujielimisha, hivyo viongozi wanapaswa kuitumia maktaba hii kuongeza maarifa,” Mhe. Jenista amesisitiza. 

Mhe. Jenista ameongeza kuwa, maktaba hiyo itakuwa ni msaada kwa viongozi katika kuwaongezea maarifa yatakayowawezesha kutekeleza jukumu la kuwaongoza wananchi kuutekeleza mpango wa taifa wa kujenga uchumi wa viwanda, ikiwa ni pamoja na kutekeleza Dira ya Taifa ya mwaka 2025. 

Mhe. Jenista amesema, Serikali inaamini kupitia machapisho na vitabu vilivyopo katika maktaba ya uongozi au maktaba nyingine zilizopo nchini, viongozi watasoma tafiti nyingi ambazo zitawajengea uwezo wa kufanya uchambuzi na upembuzi yakinifu kuhusu namna bora ya kutekeleza mipango ya maendeleo katika taifa. 

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo amesema taasisi yake iliona umuhimu wa kuanzisha Maktaba ya Uongozi yenye machapisho, vitabu na taarifa mbalimbali zinazokidhi mahitaji ya viongozi na wadau wengine kitaifa na kimataifa ambayo yamejikita kwenye maeneo ya uongozi, maendeleo endelevu, utawala bora, tawasifu za viongozi, historia, siasa na uchumi. 

Akitoa takwimu za idadi ya wanachama wa maktaba ya uongozi, Bw. Singo amesema kuwa, hadi kufikia Julai mwaka huu, maktaba hiyo ina wanachama hai zaidi ya 800 tofauti na wale wanaokuja kuitumia mara moja moja kulingana mahitaji yao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akisoma moja ya kitabu katika Maktaba ya Uongozi inayoratibiwa na Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuizindua rasmi maktaba hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Waliokaa kulia kwake ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Ikulu, Dkt. Moses Kusiluka na kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wadau wa Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuzindua rasmi maktaba ya Uongozi na toleo la Kiswahili la tawasifu ya Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa “Maisha Yangu, Kusudi Langu” katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.


Sehemu ya wadau wa Taasisi ya UONGOZI wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama alipokuwa akizungumza nao kabla ya kuzindua rasmi maktaba ya Uongozi na toleo la Kiswahili la tawasifu ya Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa “Maisha Yangu, Kusudi Langu” katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Ikulu, Dkt. Moses Kusiluka na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama wakati wa uzinduzi wa maktaba ya Uongozi na toleo la Kiswahili la tawasifu ya Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa “Maisha Yangu, Kusudi Langu” katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizindua maktaba ya Uongozi inayoratibiwa na Taasisi ya UONGOZI katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiangalia moja ya kitabu katika Maktaba ya Uongozi inayoratibiwa na Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuzindua rasmi maktaba hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akifurahia maudhui yaliyomo katika moja ya kitabu kwenye Maktaba ya Uongozi inayoratibiwa na Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuzindua rasmi maktaba hiyo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.  Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizindua toleo la Kiswahili la tawasifu ya Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa “Maisha Yangu, Kusudi Langu” katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Anayeshiriki nae ni Mke wa Hayati Benjamin William Mkapa, Mama Anna. Wanaoshuhudia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu, Dkt. Moses Kusiluka (kulia) na Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Ombeni Sefue (kushoto) ambaye ameshiriki kutafsiri kitabu hicho.


 

No comments:

Post a Comment