Friday, October 18, 2019

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUENDANA NA WAKATI KIUTENDAJI



Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanri akielezea historia fupi ya Mkoa wa Tabora kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg walipomtembelea ofisini kwake jana kabla ya kutembelea Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Tabora kwa lengo la kuona maendeleo ya chuo hicho kilichojengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Sweden mwaka 1970. Kushoto kwa Naibu Waziri ni Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mjini, Mhe. Kitwala Komanya.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanri na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg kuingia Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Tabora jana kwa lengo la kuona maendeleo ya chuo hicho kilichojengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Sweden mwaka 1970. Kulia kwa Mkuu wa Mkoa ni Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb), Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanri na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg wakiungana na wanafunzi na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Tabora na wageni wengine kucheza muziki uliokuwa ukitumbuizwa na bendi ya Msange JKT wakati wageni hao walipotembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Tabora jana kwa lengo la kuona maendeleo ya chuo hicho kilichojengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Sweden mwaka 1970. Kulia kwa Mkuu wa Mkoa ni Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika.

Mkufunzi Msaidizi wa Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Tabora, Bw. Alex Massengo akiwaonyesha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb), Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanri na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg matukio mbalimbali katika picha yakiwemo yanayohusu ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Sweden katika kujenga Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Tabora wakati wageni hao walipotembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la Tabora jana kwa lengo la kuona maendeleo ya chuo hicho.

Mkuu wa Idara ya Uhazili,  Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Tabora, Bw. Given Simkwai akiwaonyesha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb), Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanri na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg umuhimu wa  matumizi ya hati  mkato wakati wageni hao walipotembelea Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Tabora jana kwa lengo la kuona maendeleo ya chuo hicho kilichojengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Sweden mwaka 1970.

Meneja wa Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Tabora, Bi. Felister Akonaay akiwaonyesha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg kibao kinachoonyesha ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Sweden katika kujenga Chuo cha Utumishi wa Umma, Tawi la Tabora wakati wageni hao walipotembelea Chuo hicho jana kwa lengo la kuona maendeleo yake.

No comments:

Post a Comment