Friday, October 25, 2019

MKURABITA YATAKIWA KUHAKIKISHA HATIMILIKI ZA KIMILA ZINATUMIKA KUWAPATIA MIKOPO WANUFAIKA WA MPANGO HUO ILI WAJIENDELEZE KIUCHUMI




Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Brigedia Jenerali Nicodemus Mwangela akimkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) katika mkoa wake jana kabla ya Naibu Waziri huyo kuanza ziara ya kikazi mkoani humo ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA).

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na baadhi ya Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Momba na Tunduma mkoani Songwe jana wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani humo ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) na kuzungumza na watumishi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akimsikiliza Mkuu wa Idara ya Ardhi, Bw. Kelvin Joseph alipokuwa akitoa maelezo ya utekelezaji wa Mradi wa urasimishaji mashamba ya wakulima katika Kijiji cha Naming’ongo wilayani Momba Mkoa wa Songwe wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani humo jana ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA). Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Momba, Mhe. Juma Irando.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akitoa maelekezo ya namna ya kuwaunganisha wanufaika wa MKURABITA na taasisi za fedha ili waweze kupata mikopo na kujiinua kiuchumi wakati Naibu Waziri huyo aliposimama kukagua utekelezaji wa Mradi wa urasimishaji mashamba ya wakulima katika Kijiji cha Naming’ongo wilayani Momba Mkoa wa Songwe katika ziara yake ya kikazi mkoani humo jana ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA). 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na wanufaika wa  Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) wa Kijiji cha Naming’ongo wilayani Momba Mkoa wa Songwe wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani humo jana ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Mpango huo.



No comments:

Post a Comment