Monday, October 14, 2019

KKKT YAIPONGEZA SERIKALI KWA KULETA MAENDELEO NA KUTOA USHIRIKIANO KATIKA HUDUMA ZA KIJAMII NCHINI




Askofu wa Dayosisi ya Kusini, Awamu ya Sita Dkt. George Mark Fihavango akiipongeza Serikali kwa kuleta maendeleo nchini mara baada ya kusimikwa kuwa askofu wa Dayosisi hiyo katika Ibada takatifu iliyofanyika Mjini Njombe na kuongozwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Dkt. Frederick Shoo (hayupo pichani).


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika ibada ya kumsimika Askofu wa Dayosisi ya Kusini, Awamu ya Sita Dkt. George Mark Fihavango iliyofanyika Mjini Njombe na kuongozwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Dkt. Frederick Shoo (hayupo pichani). 

Baadhi ya waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na madhehebu mengine wakishiriki ibada ya kumsimika Askofu wa Dayosisi ya Kusini, Awamu ya Sita Dkt. George Mark Fihavango iliyofanyika Mjini Njombe na kuongozwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Dkt. Frederick Shoo (hayupo pichani). 


Mkuu wa KKKT, Askofu Dkt. Frederick Shoo akimpongeza Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake kwa kuwaletea watanzania maendeleo, pongezi hizo amezitoa mbele ya waumini wa KKKT na madhehebu mengine wakati wa ibada ya kumsimika Askofu wa Dayosisi ya Kusini, Awamu ya Sita Dkt. George Mark Fihavango iliyofanyika mjini Njombe.

No comments:

Post a Comment