Tuesday, October 15, 2019

SWEDEN YAIPONGEZA SERIKALI YA TANZANIA KWA KUFANYA VIZURI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA




Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akimkaribisha Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg alipotembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Kampasi ya Dar es Salaam jana kwa lengo la kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma kwa nchi za Sweden na Tanzania.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg wakishuhudia jinsi mashine ya kupiga chapa inavyofanya kazi mara baada ya Balozi kutembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC)  jana kwa lengo la kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma kwa nchi za Sweden na Tanzania. Wa kwanza kulia ni Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg wakionyesha zawadi ya ramani ya Afrika yenye nembo ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania baada ya Balozi huyo kukabidhiwa zawadi hiyo na Naibu Waziri kuonyesha ushirikiano mwema baina ya Tanzania na Sweden katika masuala ya utumishi wa umma wakati Balozi aliotembelea chuoni hapo jana kwa lengo la kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma kwa nchi za Sweden na Tanzania.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mhe. Anders Sjoberg wakicheza wimbo unaosifu utendaji kazi wa Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Awamu ya Kwanza mpaka sasa wa kwaya ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania  wakati Balozi aliotembelea chuoni hapo jana kwa lengo la kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma kwa nchi za Sweden na Tanzania. Kushoto kwa Balozi ni Kaimu Katibu Mkuu Utumishi, Bw. Mick Kiliba.

No comments:

Post a Comment