Wednesday, February 26, 2025

WAJUMBE WA BODI YA KIMA CHA CHINI CHA MSHAHARA WASILISHENI MAPENDEKEZO YATAKAYOLETA TIJA KWA TAIFA-Mhe.Simbachawene

 Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 27 Februari, 2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amewataka Wajumbe wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara kuwasilisha mapendekezo ya Kima cha chini cha mshahara yanayochozingatia hali halisi ya maisha na maslahi ya wafanyakazi ili kuepuka migogoro na kushuka kwa morali ya wafanyakazi, tija na uzalishaji.

Mhe. Simbachawene amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizindua Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma.

Mhe. Simbachawene amesema Kima cha Chini cha Mshahara ni suala muhimu sana na lisiposhughulikiwa vizuri linaweza kusababisha migogoro isiyo ya lazima na hivyo kuzorotesha uchumi na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Ameongeza kuwa, Kima cha chini cha mshahara kisichozingatia hali halisi ya uchumi ni hatari katika maendeleo ya nchi hasa kutokana na ukweli kwamba kunaweza kusababisha kutokea kwa mfumuko wa bei, na kuongeza gharama za uendeshaji.

Waziri Simbachawene amesema Bodi ya Mshahara katika Sekta ya Umma ina jukumu la kufanya uchunguzi na kupendekeza kwa Waziri mwenye dhamana na masuala ya Utumishi wa Umma kuhusu Kima cha Chini cha Mshahara katika Sekta ya Umma, hivyo katika kutekeleza majukumu haya, Bodi ina wajibu wa kuzingatia maslahi ya nchi na mustakabali wa uchumi wa nchi wakati wa kutoa mapendekezo stahiki.

Kwa Upande wake, Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda amesema pamoja na uzinduzi wa bodi hiyo, Wajumbe watapatiwa mafunzo kwa ajili ya kujengewa uwezo zaidi na kupata uelewa kuhusu majukumu ya upangaji wa kima cha chini cha mshahara katika Utumishi wa Umma.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma, Bw. Mathias Kabunduguru amemuahidi Waziri Simbachawene kuwa watatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na malengo yaliyokusudiwa katika kupendekeza na kutoa ushauri kwa ustawi wa nchi.

Uteuzi wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara umefanywa kwa mujibu wa Kifungu cha 35(1) cha Sheria ya Taasisi za Kazi Na. 7 ya mwaka 2004 na kufanyiwa marekebisho kupitia kifungu cha 14(b) cha Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ajira na Kazi (The Employment and Labor Laws (Miscellaneous Amendment Act) Na. 24 ya mwaka 2015.

Kupitia Marekebisho hayo yaliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 08/07/2015, Serikali ilianzisha Bodi mbili, moja kwa ajili ya Sekta binafsi na nyingine kwa ajili ya Sekta ya Umma. Marekebisho hayo yalilenga kuboresha ufanisi na kupunguza gharama za uendeshaji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza wakati wa kikao cha uzinduzi wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma kilichofanyika jijini Dodoma.


Wajumbe wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akizindua bodi hiyo kwenye kikao kilichofanyika jijini Dodoma.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzindua Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma kwenye kikao kilichofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Wajumbe wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma wakiwa kwenye kikao cha uzinduzi wa bodi hiyo uliozinduliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene jijini Dodoma.


Mwenyekiti wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma, Bw. Mathias Kabunduguru akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene mara baada ya Waziri huyo kuzindua bodi hiyo jijini Dodoma.

Sehemu ya Wajumbe wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akizindua bodi hiyo jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akikabidhi vitendea kazi kwa Mwenyekiti wa  Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma Bw. Mathias Kabunduguru mara baada ya kuzindua bodi hiyo jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu, Bi. Mariam Mwanilwa mara baada ya Waziri huyo kuwasili kwa lengo la kuzindua Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara katika Utumishi wa Umma baada ya kuzindua bodi hiyo jijini Dodoma.



 

Tuesday, February 25, 2025

Monday, February 24, 2025

WATUMISHI OFISI YA RAIS-UTUMISHI WAASWA KUBADILI MFUMO WA MAISHA ILI KUJIEPUSHA NA MARADHI YASIYOAMBUKIZA

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 24 Februari, 2025

Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wametakiwa kuzingatia na kubadili mfumo wa maisha ili kujiepusha na maradhi yasiyoambukiza kwa lengo la kuwahudumia wananchi pasipokuwa na changamoto zozote za kiafya.

Wito huo umetolewa leo February 24, 2025 na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge wakati akiwasilisha mada kuhusu afya kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Dkt. Kisenge amesema Magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la damu yanatokana na namna watu wanavyoendesha maisha yao hivyo, ni vema kupunguza matumizi makubwa ya sukari na matumizi ya ulaji wa chumvi nyingi inayosababisha shinikizo la juu la damu ambalo moja ya madhara yake ni kutanuka kwa moyo ambao matibabu yake ni gharama kubwa.

Aidha, Dkt. Kisenge amewataka watumishi wa ofisi hiyo kujitahidi kutumia mtindo bora wa maisha ikiwa ni pamoja na kufanya mazoezi na kuzingatia lishe bora ili kukabiliana na magonjwa ya moyo.

Dkt. Kisenge ametoa wito kwa watumishi hao kupima afya zao mara kwa mara ili kujua tatizo mapema pamoja na kupunguza gharama za matibabu kwani ugonjwa ukishakuwa mkubwa gharama huongezeka zaidi.

Akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi hao, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amemshukuru Dkt. Kisenge pamoja na wataalamu alioambatana nao kwa kutoa elimu hiyo kwa watumishi wa ofisi yake na kuahidi kuzingatia suala la afya ili kutoa huduma bora kwa wananchi kwa ustawi wa Taifa la Tanzania.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa utaratibu uliowekwa na Ofisi ya Rais –UTUMISHI wa kutoa uelewa kuhusu masuala mbalimbali katika Utumishi wa Umma ili kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akisisitiza jambo wakati wa mafunzo kuhusu utunzaji wa afya bora yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi kwa watumishi wa ofisi yake.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo kuhusu utunzaji wa afya yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akizungumza na watumishi wa ofisi yake wakati wa mafunzo kuhusu utunzaji wa afya bora yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge akifanya wasilisho kuhusu Magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la damu wakati wa mafunzo yaliyotolewa kwa watumishi wa ofisi hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (katikati) akifuatilia wasilisho kuhusu Magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la damu wakati wa mafunzo yaliyotolewa kwa watumishi wa ofisi hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mafunzo kuhusu utunzaji wa afya bora yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mafunzo kuhusu utunzaji wa afya bora yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mtumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Stephano Mgala (aliyenyanyua mkono) akiuliza swali kuhusu afya mara baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge (hayupo pichani) kuwasilishwa mada kuhusu Magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la damu wakati wa mafunzo yanayotolewa kwa watumishi wa ofisi hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi.



Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kushoto) akifuatilia wasilisho kuhusu Magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la damu wakati wa mafunzo yanayotolewa kwa watumishi wa ofisi hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi. Wa tatu kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge (hayupo pichani) wakati akifanya wasilisho kuhusu Magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la damu kwenye mafunzo yaliyofanyika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge (hayupo pichani) wakati akifanya wasilisho kuhusu Magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la damu kwenye mafunzo yaliyofanyika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi.



Friday, February 21, 2025

NAIBU WAZIRI SANGU ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KUPITIA TASAF






 

NAIBU WAZIRI SANGU ARIDHISHWA NA UTEKELZAJI WA MIRADI YA TASAF MKOANI IRINGA

Na Lusungu Helela- IRINGA

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) mkoani Iringa huku akiitaka Mikoa mingine kuiga mfano wa Iringa kwenye matumizi bora ya  fedha za Mfuko huo.

Mhe.Sangu ametoa  pongezi hizo leo baada ya kutembelea na kukagua ujenzi  wa Kituo cha Afya cha Isele kilichopo Kata ya Mlenge, Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa kinachoendelea kujengwa na TASAF.
Kituo hicho  cha Afya hadi kukamilika kwake  kitakuwa na uwezo wa kuwahudumia zaidi ya wananchi 12,000 na  kimelenga kupunguza vifo vya akina mama wajawazito pindi wanapojifungua pamoja na wagonjwa wengine.

Mhe. Sangu amesema Kituo hicho ni  moja ya vituo 15 vya Afya vya kimkakati  vinavyojengwa nchi nzima kupitia mradi wa  TASAF kwa mwaka wa fedha 2025/2026 

Amesema ujenzi wa vituo hivyo ni  kielelezo cha umakini wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM)  katika kutekeleza Ilani yake ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma  za afya  kwa wananchi wote pasipo kujali mazingira wanayoishi lengo likiwa ni kupunguza vifo hususan vya akina mama wanapojifungua.

Ninawapongeza wananchi wa Isele licha ya kuletewa fedha za ujenzi wa kituo hiki na TASAF  lakini nanyi mmejitolea kiasi cha Sh. milioni 19 na mmeshiriki kwenye kazi za kuchimba msingi pamoja na kusogeza mchanga, hii ni ishara ya uhitaji na utayari wa kukitumia Kituo hiki, amesisitiza Mhe.Sangu 

 Nimejionea majengo ikiwemo wodi la akina mama wajawazito pamoja na wodi ya wagonjwa wa kawaida  yana ubora na thamani ya fedha inaonekana, hongereni sana kwa usimamizi makini " 

Katika hatua nyingine, Mhe.Sangu ameridhishwa na ujenzi wa vivuko vya watembea kwa miguu vilivyojengwa katika maeneo korofi katika mitaa ya Ndwika na Kitwilu katika Manispaa ya Iringa  ambavyo vimekuwa msaada mkubwa kwa wanafunzi kwani walikuwa hawawezi kwenda shule pindi mvua ikinyesha.

"Watoto wetu walikuwa hawawezi kuvuka mvua ikinyesha, shughuli za kiuchumi pia zilikuwa zinasimama kwani wa upande wa pili  walikuwa hawawezi kuja kwetu na sisi tulikuwa hatuwezi kwenda upande wa pili" amesema Juma Mwakarobo mmoja wa wakazi wa eneo Kitwilu.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata hiyo, Mhe. Msafiri Nzalamoto  ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa fedha za ujenzi wa Kituo hicho katika eneo analoliongoza huku akibainisha kuwa Kituo hicho kitakuwa mkombozi kwa wananchi wake hususan akina mama wajawazito ambao wengi wao walikuwa wakipoteza maisha kutokana na kukosekana kwa huduma hiyo.

Ujenzi wa Kituo hiki umekuja wakati muafaka tunaahidi kukitunza ili kuhakikisha maono ya Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kupunguza vifo vya akina mama wajawazito yanatimia kwa wananchi wa Isele" amesema Mhe. Nzalamoto.

Awali Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ambaye pia ni Mhandisi wa Miradi ya TASAF  Mhandisi Emmanuel Chuwa  alisema utekelezaji wa miradi unalengo la kuboresha huduma za kijamii katika maeneo ya wananchi Mkoani Iringa

 



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akizungumza leo na wananchi wa mtaa wa Kitwilu katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mara baada ya kukagua na kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akizungumza leo na wananchi wa kijiji cha Isele katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mara baada ya kukagua na kutembelea Kituo cha Afya ikiwa ni moja ya  mradi ya maendeleo unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).



Sehemu ya wananchi wa Mtaa wa Ndyuka na Kitwilu katika  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu mara baada kutembelea na kukagua kivuko cha watembea kwa miguu 


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akiwa ameongozana na wananchi wa Kijiji cha Isele mara baada ya kutembelea na kukagua Kituo cha Afya cha Isele kinachoendelea kujengwa katika eneo hilo. 
Baadhi ya majengo ya Kituo cha Afya cha Isele yanayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa. 



 Baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Ndyuka na Kitwilu katika  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wakimshangilia Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu mara baada kutembelea na kukagua kivuko cha watembea kwa miguu 

 Baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Ndyuka na Kitwilu katika  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wakimshangilia huku wakiagana naye  Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu mara baada kutembelea na kukagua kivuko cha watembea kwa miguu 

Tuesday, February 18, 2025

KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA TASAF ZANZIBAR

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika kisiwa cha Unguja Zanzibar.

Kamati hiyo, imetoa pongezi hizo baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Ukumbi wa Mitihani na  Dahalia ya wanafunzi wa kike katika skuli ya Sekondari Kizimkazi Dimbani iliyopo mkoa wa Kusini Unguja  iliyojengwa na TASAF.

Dahalia hiyo ya kisasa yenye uwezo wa kubeba wanafunzi 248, imelenga kuongeza kiwango cha ufaulu kwa kwa wanafunzi wa skuli ya Kizimkazi Dimbani.

 Akizungumza leo kwa niaba ya Kamati hiyo   mara  baada ya kutembelea mradi huo, Mwenyekiti wa Kamati  Mhe. Florent Kyombo amesema, ujenzi wa dahalia hiyo ni kielelezo na   unasaidia kuboresha upatikanaji wa huduma  za kijamii pamoja kwa wanachi wa shehia ya Kizimkazi Dimbani .

“Tunaipongeza TASAF kwa kazi nzuri iliyofanyika hapa, tumejionea mradi huu ulivyotekelezwa kwa viwango na ubora wa hali ya juu,  miradi ya aina hii ni muhimu sana kwani inachochea ari  ya kusoma kwa wanafunzi wetu,” asisitiza

 “Tumeona ni miradi inayoleta tija na imetekelezwa kwa ubora na thamani ya fedha imeonekana, hii ni kazi nzuri ambayo Rais Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ameweza kuifanya kupitia TASAF lakini pia usimamizi mzuri ulipofanywa na Rais Mhe Dkt Hussein Mwinyi kupitia  ofisi zinazosimamia TASAF visiwani Zanzibar" 

 Kwa upande wake, Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu, amesema utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Miundombinu ya utoaji huduma za kijamii unaofanywa na TASAF unalenga kusogeza huduma za kijamii karibu na wanachi  pamoja na kuboresha huduma hizo.

 “TASAF imeweza kujenga shule, madarasa, vituo vya afya, zahanati, madaraja, barabara pamoja na miundombinu ya maji na umwagiliaji, hii yote ni kutaka  kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii" amesema Mhe.Sangu 

Amesema ujenzi huo wa dahalia kwa ajili ya watoto wa kike wapatao 248  uliogharimu kiasi cha Shilingi  Milioni 336 utakuwa mkombozi kwa watoto hao kwa kuwa karibu na shule hali itakayosababisha mahudhurio na ufaulu kuwa mzuri tofauti na ilivyokuwa mwanzo. 

 Mbali na hilo, Mhe.Sangu amesema Kamati imejionea na imeridhika na  thamani halisi ya fedha ya ujenzi wa bwalo kwa ajili ya chakula kwa ajili ya watoto hao kike katika shule na hivyo kuwafanya watoto hao kusoma shule katika mazingira mazuri na rafiki kwa ajili ya mustakabali ya maisha yao ya badae.

 Awali Mwakilishi wa  Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa TASAF,  Bw. Godwin Mkisi alisema utekelezaji wa miradi  unalengo la kuboresha huduma za kijamii na katika  maeneo yote ya visiwa vya Unguja na Pemba.

Alisema, Katika kipindi cha Pili cha Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini, jumla ya miradi 14 ya miundombinu ya elimu na afya yenye thamani ya shilingi bilioni 2.3 imetekelezwa hadi kufikia mwezi Januari 2025. Kati ya miradi yote hiyo miradi 11 imekamilika na kukabidhiwa sekta husika na miradi mitatu bado inaendelea na utekelezaji

 

 


Moja ya dahalia  ya kisasa yenye uwezo wa kubeba wanafunzi 248 ambayo  imelenga kuongeza kiwango cha ufaulu kwa kwa wanafunzi wa skuli ya Kizimkazi Dimbani iliyojengwa kupitia  Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika kisiwa cha Unguja Zanzibar. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,   Mhe. Florent Kyombo akizungumza na Wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika kisiwa cha Unguja Zanzibar. 
Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu akiwa ameongoza na baadhi ya Wajumbe wa ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiangalia mabomba ya maji katika dahalia
Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu akiwa ameongoza na baadhi ya Wajumbe wa ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakikagua baadhi ya vitanda vya watoto wa kike katika moja ya chumba katika  dahalia iliyojengwa kwa ufadhili wa Mradi wa TASAF 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe, Hamza Hassan Juma akiwa kwenye picha ya pamoja na   Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu mara baada ya kufanya mazungumzo wakati Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kuanza  kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kupitia TASAF, Wengine ni viongozi wa TASAF Zanzibar 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe, Hamza Hassan Juma akizungumza na    Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu mara kabla ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kupitia TASAF
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,   Mhe. Florent Kyombo akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria  mara baada ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo ya  kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika kisiwa cha Unguja Zanzibar
  Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu  wakati akizungumza na wanufaika  wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)  mara baaada ya kutembelea na kukagua baadhi ya miradi iliyotekelezwa na  TASAF
Baadhi ya wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsikiliza   Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu  wakati akizungumza nao mara baaada ya kutembelea na kukagua baadhi ya miradi iliyotekelezwa na  TASAF

Friday, February 14, 2025

RIPOTI: ZAIDI YA ASILIMIA 40 YA WATUMISHI WA UMMA NCHINI WANAPOKEA MSHAHARA HAWAFANYI KAZI

Na Lusungu Helela-ARUSHA 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. George Simbachawene amesema zaidi ya asilimia 40 ya Watumishi wa Umma hawafanyi kazi licha ya kulipwa mshahara kila mwezi.

Amesema hiyo ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni na Tume ya Utumishi wa Umma nchini

Mhe. Simbachawene amesema hayo  leo  jijini Arusha wakati  akifunga Kikao kazi cha tano cha Serikali Mtandao ambapo amesema Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma wanawajibu wa kuhakikisha  kila mtumishi anatekeleza majukumu yake ipasavyo.

‘’Watumishi ni lazima wafanye kazi kwani wasipofanya kazi wanakuangusha wewe Mkuu wa Taasisi, lazima tuwe na jamii inayoandaliwa kufanya kazi’’ amesisitiza Mhe. Simbachawene

Amefafanua kuwa kwa mujibu wa tafiti hiyo, wavivu, wazembe, wagonjwa pamoja na waliosusiwa kutokana na vipaji na uwezo wao ni  asilimia 40 ya Watumishi wanaolipwa pasipo kufanya kazi

Amewataka Wakuu hao kuwatumia Watumishi wa Umma wenye vipaji na uwezo badala ya kuwafanyia fitina na hujuma hali inayopelekea kurudisha nyuma maendeleo ya nchi

Amesema hali hiyo imesababisha kutokuwepo kwa urithishanaji wa madaraka jambo ambalo limechangia kudhoofika kwa Taasisi pale kiongozi wa Taasisi anapostaafu au kuhama

Aidha, Mhe. Simbachawene amesema kumeibuka tabia ya baadhi ya  Watendaji wakuu hao pindi Mtumishi  mwenye sifa za ziada anapohamia kwenye Taasisi anayoiongoza hupata hofu na kutompangia najukumu kwa hisia kuwa ametumwa kumchunguza a au kuchukua nafasi yake

Ameeleza kuwa tabia hiyo kwenye utumishi wa umma haikubaliki na wale wenye tabia hiyo wajirekebishe haraka kwani Taasisi hizo wanazoziongoza ni za umma na  sio mali yao binafsi

Katika hatua nyingine, Kutokana na ongezeko la matumizi ya simu kwa wananchi, Mhe. Simbachawene amezitaka Taasisi za Umma kutoa huduma za kidijitali kutokana na fursa hiyo

Vilevile, Mhe. Simbachawene  amezitaka Taasisi za Umma ambazo hazijaanza kutumia mfumo wa kidijitari wa e-Mrejesho ziingie mara moja la sivyo zitachukuliwa hatua kali na Ofisi anayoiongoza.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka  ya Serikali Mtandao, ( e-GA)  Mhandisi Benedict Ndomba aliwashukuru washiriki wa kikao hicho cha jumla   1526  ya ushiriki wao ambapo jumla ya mada 18  ziliwasilishwa ikiwa ni pamoja na kujiwekea mikakati ya kukabiliana na changamoto za usalama wa mtandao Serikalini.

Amesema kikao hicho kimejadili changamoto mbalimbali zinazoikabili Serikali Mtandao pamoja na kuweka mikakati madhubuti ya kuchangamkia fursa ya kujifunza teknolojia mpya zinazoibukia ili kuendana na mabadiliko yanayotokea duniani kote.

Kwa upande wake,  Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia  ni Mkuu wa Wilaya ya Monduli,  Mhe.Festo Kiswaga ameishukuru e-GA kwa kuendelea kuuamini Mkoa wa Arusha ikiwa ni mara ya tano sasa vikao hivyo vimekuwa vikifanyika Mkoani humo hali iliyopelekea Mkoa huo kuwa wanufaika wakubwa wa kiuchumi pamoja na kuwa wadau namba moja  wa matumizi ya Serikali Mtandao.

Naye Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka amesema Ofisi yake itasimamia na   kufanyia kazi maazimio  yote yaliyowasilishwa leo na kuhakikisha  utekelezaji wake unawasilishwa katika kikao kijacho

Pia,  Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya e-GA, Dkt. Jasmine Bunga amesema kikao kazi hicho kimekuwa muhimu kwa washiriki ambapo mbali  ya kujadili changamoto mbalimbali  zinazowakabili  pia wamejiwekea mikakati ya kuendelea  kujenga Serikali ya kidigitali 

Amesema lengo ya kujiwekea mikakati hiyo ni kuhakikisha Serikali inapiga hatua kubwa kwenye matumizi ya mifumo ya TEHAMA itakayoleta tija na ufanisi wa hali ya juu katika utoaji wa huduma bora za haraka na za uhakika kwa wananchi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa  na Katibu Mkuu - IKULU,  Bw.Mululi Mahendeka na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora, Bw.Xavier Daudi wakiwa pamoja na viongozi wengine  wa e-GA kwenye kikao kazi cha tano  Serikali Mtandao kilichofanyika kwa muda wa siku tatu jijini Arusha wakisikiliza maazimio ya kikao hicho wakati yakiwasilishwa

Sehemu ya Washiriki wa kikao kazi cha tano cha Serikali Mtandao kilichofanyika kwa muda wa siku tatu jijini Arusha ambacho kimefungwa   leo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza wakati  akifunga  Kikao kazi cha tano  cha Serikali Mtandao kinachofanyika kwa muda wa siku tatu jijini Arusha

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwakabidhi tuzo Afisa TEHAMA wa TTCL Bi.Daris Lema ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa shirika hilo katika kutambua mchango wake katika kuiwezesha Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kufikia malengo yake kufanya kikao kazi cha tano cha Serikali Mtandao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa ameongozana na Katibu Mkuu - IKULU,  Bw.Mululi Mahendeka na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora, Bw.Xavier Daudi wakiwa pamoja na viongozi wengine  wa e-GA  mara baada ya kuwasili kwa ajili ya  kufunga  Kikao kazi cha tano  cha Serikali Mtandao kilichofanyika kwa muda wa siku tatu jijini Arusha