Tuesday, February 4, 2025

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAPATIWA ELIMU YA KINGA NA TAHADHARI DHIDI YA MAJANGA YA MOTO

 Na. Mwandishi Wetu

Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wameaswa kuchukua tahadhari dhidi ya majanga ya moto pamoja na matumizi sahihi ya namba ya dharula 114 ili kutunza jengo la ofisi hiyo na kuendelea kutoa huduma kwa wateja wanaofika ofisini hapo bila kuwa na shaka yoyote.

Wito huo umetolewa na Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Bw. Iddi Chanyika wakati wa mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yanayotolewa kila Jumatatu ya wiki kwa lengo la kujenga uelewa wa masuala ya kiutumishi ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.

Bw. Chanyika ameeleza kuwa, Ofisi ya Rais-UTUMISHI inapokea wateja wengi kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali za kiutumishi hivyo, ili kulinda usalama wa wateja wanaoingia na kutoka kwa ajili ya kupata huduma hizo ni muhimu kuchukua tahadhari hasa katika kuangalia usalama wa jengo la ofisi hiyo.

Aidha Bw. Chanyika ameipongeza Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa kuwa na vifaa mbalimbali vya tahadhari kwa ajili ya kujikinga na madhara ya moto yanayoweza kutokea. 

“Niipongeze ofisi hii kwa kuzingatia usalama wa jengo kwani nimeona mna vifaa kwa ajili ya tahadhari dhidi ya moto vikiwemo ving’amua moto,’’ amesema Bw. Chanyika

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cosmas Ngangaji ametoa shukrani kwa niaba ya Watumishi wa ofisi hiyo kwa mafunzo mazuri ambayo yatasaidia kuongeza umakini katika utunzaji wa majengo ya ofisi hiyo na kuahidi kuchukua tahadhari zote zinazohusu kinga dhidi ya majanga ya moto.

Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Bw. Iddi Chanyika (kushoto) wakati akielezea namna ya kuchukua tahadhari dhidi ya majanga ya moto kwenye mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao yaliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo kuhusu namna ya kuchukua tahadhari dhidi ya majanga ya moto yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Bw. Iddi Chanyika (aliyesimama) akielezea matumizi ya kizima moto cha aina ya unga mkavu wakati wa mafunzo ya kuwajengea uelewa kuhusu tahadhari dhidi ya majanga ya moto kwa watumishi hao yaliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Afisa Tawala Mwandamizi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. George Ndatta akifanya zoezi kwa vitendo la kuzima moto kwa kutumia gesi ya ukaa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uelewa kuhusu tahadhari dhidi ya majanga ya moto kwa watumishi hao yaliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo kuhusu namna ya kuchukua tahadhari dhidi ya majanga ya moto yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Bw. Iddi Chanyika (kulia) wakati akifafanua jambo kwenye mafunzo ya uelewa kuhusu kuchukua tahadhari dhidi ya majanga ya moto yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cosmas Ngangaji akitoa shukrani kwa Maafisa kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mara baada ya kumaliza kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa ofisi hiyo kuhusu kuchukua tahadhari dhidi ya majanga ya moto yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Bajeti, Bi. Julieth Magambo (aliyeinama) akifanya zoezi kwa vitendo la kufungua kizima moto cha aina ya unga mkavu wakati wa mafunzo ya kuwajengea uelewa kuhusu tahadhari dhidi ya majanga ya moto kwa watumishi hao yaliyofanyika Mtumba jijini Dodoma. Anayemwelekeza ni Mkaguzi kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Bw. Steven Katte.








No comments:

Post a Comment