Monday, February 3, 2025

WAZIRI SIMBACHAWENE AIPONGEZA MENEJIMENTI YA OFISI YAKE KUBUNI SIKU MAALUM “UTUMISHI DAY GALA” ASISITIZA ITUMIKE KUWAKUMBUSHA WATUMISHI KUTIMIZA WAJIBU

Na Mwandishi Wetu - Dodoma 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameipongeza menejimenti ya Ofisi yake kwa kuwa wabunifu katika masuala mbalimbali ya kiutumishi ikiwemo kubuni tukio la "Utumishi Day Gala”.

Mhe. Simbachawene ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki hii jijini Dodoma katika Siku maalum ya "Utumishi Day Gala 2025” iliyoandaliwa na menejimenti ya Ofisi yake kwa lengo la kubadilishana uzoefu ili kuboresha utendaji kazi hasa katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesema Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora itabaki kuwa Ofisi Kiongozi kutokana na bunifu mbalimbali ambazo imekuwa ikifanya kwa lengo la kuhakikisha Watumishi wake wanakuwa vinara wa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Ameongeza kuwa Ofisi hiyo imekuwa ikijipambanua katika masuala mbalimbali ambayo huwezi kukutana nayo katika Wizara yeyote isipokuwa Utumishi lengo likiwa ni kuhakikisha Watumishi wanajengewa mazingira bora na wezeshi katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesema utamaduni huo wa kukutana mara moja kwa kila mwaka unatoa motisha kwa watumishi na kuongeza ufanisi na uwabikaji katika kutekeleza majukumu yao 

Mhe. Simbachawene amesisitiza kuwa ni vema siku hiyo maalum ikatumika kuhamasisha na kuwakumbusha watumishi wa Ofisi hiyo kutimiza wajibu wao kwa kutoa huduma bora kwa wananchi kwani wananchi wakihudumiwa kwa furaha, amani na utumilivu vinatawala nchini.

"Nimebahatika kuwa Waziri katika Wizara tisa lakini huu utamaduni wa kukutana kwa pamoja kama leo hii tulivyokutana hapa tunafurahi kwa pamoja haikuwahi kutokea, hakika hili jambo linapaswa kuigwa na Wizara zingine" alisisitiza Mhe. Simbachawene 

Ameongeza kuwa "Unaweza kudhani umeshaona mambo yote kumbe hapana hili la "Utumishi Day Gala" kwangu mimi ni jipya hakika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora ni Ofisi Kiongozi katika nyanja zote na ndivyo inavyotakiwa, hongereni sana Menejimenti kwa ubunifu huu" 

Naye Naibu Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Deus Sangu ametumia fursa hiyo kuipongeza timu ya Menejimenti kwa wazo hilo la "Utumishi Day Gala" huku akiwataka Watumishi kufurahia huku wakibadilisha mbinu za kuhakikisha kila mmoja anakuwa kinara wa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Awali Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amesema tukio hilo hufanyika mara moja kila mwaka ambapo Watumishi hukutana kwa pamoja ikiwa ni fursa adhimu  kwao kutokana majukumu mengi wanayoyatekeleza kuwapelekea kutokuonana kwa pamoja kama ilivyo kwa ''Utumishi Day Gala”

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na watumishi wa ofisi yake kwenye Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma katika siku maalum (UTUMISHI DAY GALA 2025) iliyoandaliwa na Menejimenti ya ofisi yake kwa lengo la kujenga umoja na kuongeza chachu ya utendaji kazi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu akizungumza na watumishi wa ofisi yake jijini Dodoma katika siku maalum (UTUMISHI DAY GALA 2025) iliyoandaliwa na Menejimenti ya ofisi hiyo kwa lengo la kujenga umoja na kuongeza chachu ya utendaji kazi kwa watumishi wa ofisi yake.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) kuzungumza na watumishi wa ofisi hiyo katika siku maalum (UTUMISHI DAY GALA 2025) iliyoandaliwa kwa lengo la kujenga umoja na kuongeza chachu ya utendaji kazi kwa watumishi wa ofisi yake.

Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI waliohudhuria katika siku maalum (UTUMISHI DAY GALA 2025) iliyoandaliwa na menejimenti ya ofisi hiyo kwa lengo la kujenga umoja na kuongeza chachu ya utendaji kazi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (kulia) akifurahia jambo na  Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) katika siku maalum (UTUMISHI DAY GALA 2025) iliyoandaliwa na menejimenti ya ofisi hiyo jijini Dodoma kwa lengo la kujenga umoja na kuongeza chachu ya utendaji kazi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (wa pili kutoka kushoto) akiwasili katika eneo lililoandaliwa kwa ajili ya siku maalum (UTUMISHI DAY GALA 2025) kwa lengo la kujenga umoja na kuongeza chachu ya utendaji kazi.








No comments:

Post a Comment