Friday, February 7, 2025

WAZIRI WA UTUMISHI ZANZIBAR MHE. HAROUN ASISITIZA MASHIRIKIANO BAINA YA SJMT NA SMZ KATIKA MASUALA YA UTUMISHI

 Na. Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman amewataka Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (SJMT) na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kuendeleza mashirikiano katika masuala ya utumishi kwa ustawi wa maendeleo ya taifa.

Mhe. Suleiman amesema hayo leo wakati akihitimisha kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi baina ya ofisi hizo mbili kilichofanyika kwa siku tatu jijini Dodoma.

Mhe. Suleiman amesema kikao hicho kiongeze tija katika utendaji kazi ikiwemo kubadilishana uzoefu kuhusu masuala mbalimbali ya kiutumishi pamoja na kujadili changamoto mbalimbali zitakazosaidia kuimarisha utumishi  kwa ufanisi mkubwa kwa maendeleo ya taifa.

Aidha, Waziri Suleiman amewataka washiriki wa kikao hicho kuwa wazalendo, waaminifu na waadilifu, kusimamia walio chini yao na kutii maagizo ya viongozi walio juu yao.

Kwa Upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu akimwakilisha Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. George Simbachawene amesema kikao hicho  kitawajengea uwezo mkubwa katika kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kuzingatia miongozo na kanuni za Utumishi wa Umma. 

Awali, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amesema kikao hicho kitasaidia kuimarisha mashirikiano mazuri baina ya ofisi hizo mbili na kuahidi kuendelea kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa majukumu kwa masilahi mapana ya nchi.

Katika Kikao hicho cha siku tatu moja ya maazimio yaliyopitishwa ni kutoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kusimamia vema masuala ya Utumishi na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (kushoto) akizungumza wakati wa kikao baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (aliyesimama) akizungumza wakati wa kikao baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (aliyevaa tai nyeusi) akiwasili katika eneo la kikao kilichofanyika baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi.


Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakiwa kwenye kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akitoa maelezo ya awali kabla ya kuanza rasmi kwa kikao baina ya ofisi yake na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia kikao  kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi baina ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (kulia) akizungumza jambo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (katikati) kabla ya Mhe. Suleiman kufunga kikao baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI (SJMT) na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.  Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi.

Viongozi na Watendaji wa Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakifuatilia kikao cha ofisi hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (SJMT) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (SJMT) na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) baada ya kufunga kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi.


 

No comments:

Post a Comment