Na. Mwandishi Wetu-Dodoma
Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Uendelezaji Sera, Sehemu
ya Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo ametoa wito kwa Waelimisha
Rika wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kutoa elimu kwa watumishi walio kwenye Idara na
Vitengo vya Ofisi hiyo namna ya kutunza na kuimarisha afya ili waweze kutekeleza
majukumu yao kwa ufanisi kwa masilahi mapana ya taifa.
Bi. Mtoo ametoa wito huo jijini Dodoma wakati
akifungua mafunzo yaliyotolewa kwa Waelimisha Rika hao yaliyolenga kuwajengea
uwezo katika kutekeleza majukumu yao.
Amesema kuwa Waelimisha Rika katika ofisi ni watu
muhimu hivyo mafunzo hayo yatawasaidia kufahamu mbinu mbalimbali za kutumia
katika utoaji wa elimu na namna ya kuimarisha afya za watumishi wenzao ili ziwasaidie
katika kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kuzingatia utunzaji ya afya bora.
“Ninyi ni watu muhimu sana katika ofisi zetu, naamini
mafunzo haya yatawajengea uwezo mkubwa wa kutoa elimu na kuwaelekeza watumishi
wenzenu namna ya kutunza na kuimarisha afya iliyo bora, na hapa niwakumbushe kuzingatia
lishe iliyo bora ili muweze kutekeleza majukumu ya taifa,” Bi. Mtoo amesema.
Akiwasilisha mada kuhusu lishe bora, Afisa Lishe
kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Nusrat Rubambura amesisitiza
masuala ya kuzingatia katika kuimarisha afya ikiwemo kufanya mazoezi, kunywa
maji ya kutosha pamoja na kula vyakula mchanganyiko kutoka katika makundi sita
ikiwemo nafaka, mizizi na ndizi za kupika, asili ya wanyama, jamii ya kunde,
mbogamboga, matunda na Mafuta salama.
Akizungumza
kwa niaba ya Waelimisha Rika hao, Mwenyekiti
wa Waelimisha Rika Bw. Kokolo Lusanda ameahidi watashirikiana katika kutoa
elimu kwa watumishi wenzao ili kuzingatia utunzaji wa afya zao na kuwawezesha kutekeleza
majukumu yao kwa ufanisi.
Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Uendelezaji Sera, Sehemu
ya Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akisisitiza
jambo wakati akifungua mafunzo yaliyolenga kuwajengea uwezo Waelimisha Rika wa Idara na Vitengo vya
ofisi hiyo ili
kupambana na Afua za VVU, UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi.
Sehemu ya Waelimisha Rika, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo yaliyolenga kuwajengea uwezo Waelimisha Rika wa Idara na Vitengo vya
ofisi hiyo ili
kupambana na Afua za VVU, UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi yaliyofanyika
katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba.
Afisa Lishe kutoka Hospitali
ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Nusrat Rubambura (aliyesimama) akiwasilisha
mada kuhusu lishe bora wakati wa mafunzo kwa Waelimisha Rika wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
yaliyolenga kuwajengea uwezo Waelimisha Rika
wa Idara
na Vitengo vya ofisi hiyo ili
kupambana na Afua za VVU, UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi.
Sehemu ya Waelimisha Rika, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza
Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Uendelezaji Sera, Sehemu
ya Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo (hayupo
pichani) wakati akifungua mafunzo yaliyolenga kuwajengea
uwezo Waelimisha Rika
wa Idara
na Vitengo vya ofisi hiyo ili
kupambana na Afua za VVU, UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi.
Sehemu ya Waelimisha Rika, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo yaliyolenga kuwajengea
uwezo Waelimisha Rika
wa Idara
na Vitengo vya ofisi hiyo ili
kupambana na Afua za VVU, UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi yaliyofanyika
katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba.
No comments:
Post a Comment