Na.Lusungu Helela- Dodoma
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeanza kuwanoa Watumishi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuhusu kuandaa Daftari la kielektroniki la Huduma za Serikali kwa Taasisi zote za Serikali kwa lengo la kuwawezesha wananchi na wadau mbalimbali kupata taarifa za huduma zote zinazotolewa na Taasisi za Serikali kwenye chanzo kimoja.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP.Ibrahim Mahumi akizungumza wakati akifungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali kilichowakutanisha baadhi ya Watumishi kutoka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP.Ibrahim Mahumi akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Patrick Marcelline mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kufungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali kilichowakutanisha baadhi ya Watumishi kutoka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii
Baadhi ya Watumishi kutoka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi akizungumza wakati akifungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa kutoka
Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Patrick Marcelline akizungumza kabla ya
kumkaribisha Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP. Ibrahim
Mahumi kuzungumza na Watumishi wakati akifungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP.Ibrahim Mahumi
akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara
ya Maliasili na Utalii mara baada
kufungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali
No comments:
Post a Comment