Tuesday, February 4, 2025

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAZINOA TAASISI ZA MALIASILI NA UTALII KUHUSU KUANDAA DAFTARI LA HUDUMA ZA SERIKALI


Na.Lusungu Helela- Dodoma

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeanza kuwanoa Watumishi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuhusu kuandaa Daftari la kielektroniki la Huduma za Serikali kwa Taasisi zote za Serikali kwa lengo  la kuwawezesha wananchi na wadau mbalimbali  kupata  taarifa za huduma zote zinazotolewa  na Taasisi za Serikali kwenye chanzo kimoja.

 

Hayo yamesemwa jijini Dodoma na Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi wakati akifungua kikao kazi kuhusu Daftari la Huduma za Serikali kilichowakutanisha baadhi ya Watumishi kutoka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii,

 

SACP Mahumi amesema Daftari hilo ni muendelezo wa utengenezaji wa mifumo ya kuiwezesha serikali kutoa huduma bora kwa wananchi.

 

Kufuatia hatua hiyo SACP. Mahumi amewataka Watumishi hao kuzingatia mafunzo ya uandaaji wa daftari hilo kwani litakuwa chachu ya kuboresha utoaji wa huduma katika Taasisi za Wizara hiyo.

 

Amewasihi Watumishi hao kutambua kuwa Mteja ndiyo mlengwa mkuu wa daftari hilo hivyo wahakikishe huduma zote zinazotolewa  na Taasisi zao  zinaainishwa na kuingizwa  kwenye daftari hilo kwa usahihi wa hali ya juu.

 

Akitolea mfano wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) SACP. Mahumi amesema ili Mwananchi aweze kupata huduma katika taasisi hiyo ni lazima awe na taarifa za kutosha  kwa kuzingatia huduma zinazotolewa,  gharama na muda utakaotumika kupata huduma hizo.

 

Katika hatua nyingine, SACP. Mahumi amewataka washiriki wa mafunzo hayo wakawe mabalozi na wakatumie muda kuwafundisha watumishi wengine ili waweze kujua umuhimu wa  daftari hilo.

 

Awali, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Patrick Marcelline, ameushukuru uongozi wa Ofisi Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa mafunzo hayo muhimu, na kuahidi kuwa Wizara itayatumia Mafunzo hayo kama nyenzo muhimu ya kuboresha huduma zake kwa maslahi mapana ya Uhifadhi na Utalii na Taifa kwa ujumla

 

Kikao kazi hicho cha siku tatu cha uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali kinawezeshwa na timu ya wataalam wabobezi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

 

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP.Ibrahim Mahumi akizungumza wakati akifungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali kilichowakutanisha baadhi ya Watumishi kutoka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii

 


Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP.Ibrahim Mahumi  akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Patrick Marcelline   mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kufungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali kilichowakutanisha baadhi ya Watumishi kutoka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii

 

Baadhi ya Watumishi kutoka Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi akizungumza wakati akifungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari la Huduma za Serikali

 



Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Patrick Marcelline akizungumza kabla ya kumkaribisha Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi kuzungumza na Watumishi wakati akifungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari  la Huduma za Serikali

 

 




Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI, SACP.Ibrahim Mahumi akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii mara baada  kufungua kikao kazi kuhusu uandaaji wa Daftari  la Huduma za Serikali

No comments:

Post a Comment