Na. Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe
27 Aprili, 2026
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Nolasco Kipanda kwa niaba ya
Katibu Mkuu na Watumishi wote wa Ofisi hiyo amemuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa
Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa
ambaye amestaafu kwa kwa mujibu wa Sheria.
Bw. Kipanda ameyasema hayo Aprili 27, 2026 katika eneo maalum
la mafunzo lililopo katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Amesema, Ofisi ya Rais-Utumishi itamkumbuka Mkurugenzi huyo
kwa upendo wake, umahiri, ujasiri, mchango na kazi nzuri aliyoifanya ya kuleta
tija katika utumishi wa Umma.
Kwa upande wake, Bi. Mwanilwa amewaasa watumishi hao kufanya
kazi kwa umoja na kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma ili
kutoa huduma kwa haki na usawa.
Bi. Mwanilwa aliwasisitiza watumishi wa umma kufanya kazi kwa
kujituma huku wakizingatia maadili ya utendaji ili kuufikia mwisho mwema wa
utumishi wao.
Wakurugenzi
wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma wakimkabidhi kwa niaba ya Katibu Mkuu –UTUMISHI keki aliyekuwa Mkurugenzi
wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa
(wanne kutoka kulia) ambaye amestaafu, utumishi wake kwa mjibu wa sheria, kama
ishara ya kumshukuru kwa mchango wake chanya katika Ofisi hiyo na kumtakia
maisha mema anapohitimisha utumishi wake.
Maafisa wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI waliowahi kufanya kazi na Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na
Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa wakipata picha ya pamoja na
Mkurugenzi huyo mara baada ya kumuaga rasmi katika eneo la Ofisi hiyo lililopo
Mtumba jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na
Marupurupu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) akimlisha
keki Afisa wa Ofisi hiyo kama ishara ya umoja na mshikamano kati yake na
watumishi hao, mara baada ya mkurugenzi huyo kuagwa rasmi katika Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Leila Mavika (kulia) akikabidhi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi zawadi aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) mara baada ya Mkurugenzi huyo kufikia ukomo wa Utumishi wake kwa mujibu wa sheria .
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Nolasco Kipanda (kushoto) akisisitiza
jambo kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na
Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (wa pili kutoka kushoto) wakati wa
alipokuwa akiagwa rasmi katika eneo maalumu la mafunzo la Ofisi hiyo lililopo
Mtumba jijini Dodoma. Wa pili na kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Rasilimaliwatu wa Ofisi hiyo Bi. Leila Mavika na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI
na Magonjwa Yasiyoambukiza wa Ofisi hiyo Bi. Mwanaamani Mtoo
Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu Ofisi Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa akifurahia jambo wakati alipokuwa akitoa neno la kuwaaga watumishi wa Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 katika eneo maalumu la mafunzo lililopo katika Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Nolasco Kipanda (kushoto) akitoa neno la shukrani pamoja na kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (aliyesimama katikati) katika eneo maalumu la mafunzo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kwa Ofisi hiyo Bi. Leila Mavika
Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na
Marupurupu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) akimlisha
keki Afisa wa Ofisi hiyo kama ishara ya umoja na mshikamano kati yake na
watumishi hao, mara baada ya mkurugenzi huyo kuagwa rasmi katika Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) akimlisha keki Afisa wa Ofisi hiyo kama ishara ya umoja na mshikamano kati yake na watumishi wa Ofisi hiyo, mara baada ya mkurugenzi huyo kuagwa rasmi katika Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 jijini Dodoma.

No comments:
Post a Comment