Monday, April 27, 2026

MAFUNZO YA USIMAMIZI WA VIHATARISHI KWA WATUMISHI WA UMMA KUONGEZA UFANISI

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 27 Aprili, 2026

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi. Leila Mavika amesema mafunzo ya usimamizi wa vihatarishi kwa watumishi wa umma ni muhimu kwa kuwa yanaongeza uelewa wa kutambua, kuchambua na kudhibiti vihatarishi vinavyoweza kuathiri utendaj kazi wa shughuli za Serikali.

Bi. Mavika ameyasema hayo Aprili 27, 2026 wakati akimwakilisha Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi katika kuhitimisha mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi wa Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.

Bi. Mavika meongeza kuwa, kutokana na uelewa ambao umepatikana wakati wa mafunzo hayo ni imani yake kuwa kila mtumishi wa ofisi hiyo atakuwa na uwezo wa kuchambua na kutambua vihatarishi vilivyopo katika eneo lake la kazi na kuvidhibiti kabla ya madhara kutokea.

Awali, Afisa Ukaguzi Mkuu kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando amesema, Serikali imeweka msisitizo kwa Wizara na Taasisi za umma kuimarisha mifumo ya udhibiti wa vihatarishi ili kuboresha uwajibikaji.

Vilevile Bi. Lugando alitoa wito kwa watumishi wa kila Idara na vitengo kuhakikishe wanatambua vihatarishi vinavyoweza kutokea katika Idara na vitengo vyao ili kuimarisha usalama.



Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi. Leila Mavika akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati mkurugenzi huyo alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao katika eneo maalumu lla Ofisi hiyo ililopo Mtumba jijini Dodoma. 



Viongozi na watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma na mwezeshaji kutoka Wizara ya fedha Bi. Adolphina Lugando (hayupo pichani) kuhusu kutambua, kuchambua na kudhibiti vihatarishi vinavyoweza kuathiri utendaj kazi kwa lengo la kuwajengea uelewa watumishi hao.



Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma

Afisa Ukaguzi Mkuu kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando akitoa mafunzo ya uelewa kuhusu usimamizi wa vihatarishi kwa watumishi wa umma wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora (hawapo pichani) yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.


Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma


Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijin i Dodoma


Baadhi ya Wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya  uelewa leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatun ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijin i Dodoma

Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma


Baadhi ya Wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya  uelewa leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatun ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijin i Dodoma


No comments:

Post a Comment