Tuesday, April 21, 2026

WATUMISHI WA UMMA WASISITIZWA KUSHUGHULIKIA MREJESHO WA WANANCHI KWA HAKI NA KWA WAKATI

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 21 Aprili, 2026

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli amewasisitiza Watumishi wa Umma kushughulikia kwa haki na kwa wakati mrejesho unaowasilishwa na wananchi kupitia Mfumo wa (e- Mrejesho) ili kujenga imani na heshima ya Serikali kwa umma.

Bi. Shuli ameyasema hayo leo Aprili 21, 2026 wakati akimuwakilisha Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi katika ufunguzi wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini yake.

“Ili kufikia utumishi wa umma unaowajibika na uliotukuka, ni vizuri tukashughulikia mrejesho wa wananchi kwa haki na uharaka zaidi.” Bi Shuli alisema.

Amesema, Watumishi wa Umma wanapaswa kuwa na mabadiliko katika fikra, mitazamo, mifumo na tabia walizonazo ili kuwa na Utumishi wa Umma wenye matokeo chanya na thamani halisi kwa mwananchi.

Bi Shuli ameongeza kuwa uzingatiaji wa maadili katika utumishi wa umma si kuzifuata tu Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma bali ni pamoja na kuutumia ipasavyo utaalamu unaohusu ushughulikiaji wa mrejesho wa wananchi .

Amesema ni jukumu la kila mshiriki kuonesha ushirikiano na kuzingatia utu hususani wanapotoa huduma kwa wateja pamoja na kuwa waaminifu hasa katika utunzaji siri kwa kuwa kazi watakazofanya zitahitaji kuwa na matumizi sahihi ya taarifa.

Aidha, amewapongeza washiriki wote kwa kuhudhuria mafunzo hayo na kuwataka wajifunze kwa bidii ili wawe wataalamu watakaowajibika kikamilifu

Kwa upande wake mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw. Albano Lukiano   amemshukuru Bi. Shuli kwa kuwafungulia mafunzo hayo na kuahidi kuwa yale yote watakayofundishwa watayazingatia na kuyafanyia kazi ili kutoa huduma bora kwa manufaa ya umma.



Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho ambaye pia ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw. Albano Lukiano (kulia) kabla ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo jijini Dodoma.  


Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Janet Mishinga, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni Rasmi kufungua mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli (kushoto) akifurahia jambo mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili wa Ofisi hiyo Bi. Janet Mishinga


Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Afisa tawala kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Semeni Muyabhaga akiwasilisha mada ya wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Mwenyekiti wa kikao cha mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho Bw. Albano Lukiano akitoa neno la shukrani kwa Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi Kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Hassan Kilenza akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa mjadala wa hoja mbalimbali kuhusu matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Afisa Tawala kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Stella Teri akiwasilisha mada kuhusu uzingatiaji wa Kanuni za Maadili ya Utendeji kwa watumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Afisa rasilimali watu mwaandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Saada Ibrahim akiwasilisha mada ya    wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika  Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Afisa rasilimali watu mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Nasra Iduri akiwasilisha mada ya wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

 

No comments:

Post a Comment