Monday, October 13, 2025

WITO WATOLEWA KWA WATUMISHI WA UMMA KUBADILIKA KIMTAZAMO KATIKA UTENDAJI ILI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

 Na Antonia Mbwambo- Dodoma.

Tarehe 13/10/2025

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi ametoa wito kwa Watumishi wa Umma nchini kubadilika kimtazamo katika utendaji ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ikiwemo matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

 Bw. Daudi ametoa wito huo leo tarehe 13/10/2025 alipokuwa akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo eneo maalum linalotumika kutoa mafunzo katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma, yanayofanyika kila siku ya Jumatatu kwa lengo la kuwajengea uwezo watumishi hao ili kuboresha Utendaji kazi.

 

Kaimu Katibu Mkuu Bw. Daudi amesema, Watumishi wa Umma kubadilika kimtazamo katika utendaji ni jambo muhimu kwani kunakuwa na ufanisi wa wa kazi unaowezesha kuwa na Taifa jumuishi lenye ustawi, haki na linalojitegemea.

 

“Ninatoa wito kwenu, msitekeleze majukumu yenu kwa mazoea, kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, mbadilike kiutendaji ili kuendana na mabadiliko yakiwemo ya kidijiti kwa kuleta ubunifu na mawazo chanya yatakayoiwezesha serikali kufikia malengo yake ya kutoa huduma bora kwa wananchi kupitia matumizi sahihi ya mifumo ya TEHAMA,” Bw. Daudi alisema. 

 

Kwa upande wake Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo wakati akiwasilisha mada kwa watumishi hao kuhusu Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, amesema mabadiliko makubwa ya Sayansi na Teknolojia ni kichocheo kikubwa cha maendeleo katika Taifa letu ambapo Dira hii imelenga kuwa kufikia mwaka 2050, asilimia 70 ya Watanzania watakuwa wanatumia mifumo ya TEHAMA na asilimia 80 ya  huduma mbalimbali za kiserikali zitakuwa zikitolewa kidiji ili kuleta Ufanisi katika Utendaji.


Wakurugenzi wa Idara na vitengo mbalimbali kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na mwezeshaji ambaye ni Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (hayupo pichani) leo tarehe13/10/2025 katika mafunzo ambayo hutolewa kila siku ya jumatatu kwenye Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (aliyesimama mbele) akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo baada ya wasilisho la mada ya Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 lililotolewa leo tarehe13/10/2025 na Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo katika mafunzo ya kuwajengea watumishi wa Ofisi hiyo uwezo wa kiutendaji, ambayo hutolewa kila siku ya jumatatu kwenye Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.

Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (aliyesimama mbele) akiwasilisha mada ya Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI,yaliyofanyika leo tarehe 13/10/2025 katika Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (wa kwanza kushoto aliyevaa miwani) akifurahia jambo alipokuwa akifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo ambayo hufanyika kila siku ya jumatatu katika Ofisi hiyo Mtumba Dodoma.


Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na mwezeshaji ambaye ni Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (hayupo pichani) kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo ambayo hufanyika kila siku ya jumatatu katika Ofisi hiyo Mtumba Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akiteta jambo na Mkurugenzi wa Mipango wa Ofisi hiyo Bw. Cosmas Ngangaji wakati wa mafunzo ya kuwajengea watumishi wa Ofisi hiyo uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara na vitengo pamoja na watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na mwezeshaji ambaye ni Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (hayupo pichani) leo tarehe13/10/2025 katika mafunzo ambayo hutolewa kila siku ya jumatatu kwenye Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.

Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (aliyesimama mbele, mwenye miwani) akitoa ufafanuzi na majibu ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na watumishi baada ya kuhitimisha wasilisho la mada ya Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 lililotolewa katika eneo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI leo tarehe 13/10/2025 jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment