Monday, October 27, 2025

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAWAPONGEZA WASTAAFU WA OFISI HIYO KWA KULITUMIKIA TAIFA KIKAMILIFU

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 28 Oktoba, 2025

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imewapongeza Watumishi wa Ofisi hiyo waliofikia ukomo katika Utumishi wa Umma kutokana na utumishi uliotukuka kwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ambao umechangia kutolewa kwa huduma bora katika Idara walizokuwa wakifanyia kazi.

Akitoa pongezi hizo kwa niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, leo tarehe 27 Oktoba, 2025, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi amesema kufikisha umri wa miaka 60 sio mchezo, ni jambo la kumshukuru Mungu.

 “Hongereni sana, mmeondoka katika Utumishi wa Umma mkiwa na sifa nzuri katika kulitumikia taifa na mkiwa na afya njema ni mfano mzuri wa kuigwa na tunaoendelea kufanya kazi,” amesema SACP. Mahumi.

SACP. Mahumi amemshukuru Katibu Mkuu-UTUMISHI kupitia Idara ya Utawala kwa kuanzisha utamaduni wa kukutana kila Jumatatu na kuwa na ubunifu mbalimbali wa kuwaweka watumishi pamoja kwa lengo la kuboresha utendaji.

“Tangu jambo hili la kukutana pamoja kila siku ya Jumatatu kupata elimu ya kuboresha utendaji kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kiutendaji, nawasihi tuendelee kuyatumia mafunzo haya kuboresha utendaji zaidi.” Amesisitiza.

Akitoa neno la shukrani, Mtumishi Mstaafu wa Ofisi hiyo, Bw. Jerome Nchimbi amesema, ndani ya miaka 8 aliyofanya kazi katika ofisi hiyo amejfunza masuala mengi ya Kiutumishi pamoja na kufundishwa upendo, ushirikiano na kuwajali watu.

Kwa upande wake, Mstaafu mwingine, Bi. Godliver Byemerwa ametoa wito kwa Watumishi wa ofisi hiyo kuendelea kuwahudumia Wananchi kwa moyo wa upendo na ufanisi mkubwa kwa kuwa ofisi hiyo ni kioo cha jamii.

Aidha, Ofisi hiyo imewapongeza Watumishi waliozaliwa mwezi Oktoba na kuwatakia heri katika maisha yao ya Utumishi wa Umma ili kuwatumikia wananchi pamoja na kuongeza tija katika utendajikazi.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (wakwanza kulia) akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa Watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. 


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakiwasikiliza Watumishi wastaafu Bw. Jerome Nchimbi na Bi. Godliver Byemerwa (hawapo pichani) wa ofisi hiyo walipokuwa wakitoa shukrani kwa Viongozi na Watumishi mara baada ya kufikia ukomo katika Utumishi wa Umma. 


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa Watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. 

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa Watumishi hao katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. 

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, wa ofisi hiyo, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mtumishi Mstaafu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Jerome Nchimbi akitoa neno la shukrani kwa Wakurugenzi na Watumishi wa ofisi hiyo baada ya kuhitimisha Utumishi wake wa Umma.

Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. 

Mtumishi Mstaafu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Godliver Byemerwa akitoa neno la shukrani kwa Wakurugenzi na Watumishi wa ofisi hiyo baada ya kuhitimisha Utumishi wake wa Umma.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. 


No comments:

Post a Comment