Thursday, October 2, 2025

SAYANSI NA TEKNOLOJIA YASUKUMA MABORESHO YA KANUNI ZA KUDUMU KATIKA UTUMISHI WA UMMA

 Na. Antonia Mbwambo

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI SACP. Ibrahim Mahumi amesema Serikali imeamua kufanya mapitio na maboresho makubwa ya kanuni za kudumu katika Utumishi wa Umma kutokana na mabadiliko na ukuaji wa sanyansi na teknolojia ambayo imeathiri eneo la Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma.

SACP. Mahumi alisema hayo Oktoba 2, 2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Jijini Dodoma wakati wa kufungua kikao kazi cha Wadau cha kuhakiki rasimu ya Kanuni za Kudumu  katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la mwaka 2025. Kikao kazi hicho kilihusisha Wakurugenzi na Mameneja wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka katika taasisi mbalimbali za umma.

“Mwitiko huu ni ishara tosha kuwa maoni thabiti yatapatikana kwa kuzingatia kuwa ninyi ndio mnaopata changamoto wakati wa utekelezaji wa kanuni hizi, hivyo maoni yenu kama wadau ni muhimu katika kuboresha Kanuni hizi za kudumu katika Utumishi wa Umma” alisema SACP. Mahumi.

SACP. Mahumi alisema kuwa kwa sasa kuna sheria nyingi zinazosimamia maeneo ya Utumishi wa Umma ikiwemo Sheria ya Utumishi wa Umma, Sheria ya Mahusiano Kazini, Sheria za hifadhi ya jamii hivyo mawazo yenu yanatakiwa kuleta muunganiko mzuri  kati ya Sera, Sheria na Kanuni za kudumu katika Utumishi wa Umma.

Aidha SACP. Mahumi alisisitiza wadau hao kutoa maoni kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya 2050 ili kuwa na muunganiko wa kanuni hizo na kuleta urahisi kwa watumishi wa umma hasa pale wanapofanya  marejeo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga amehitimisha mjadala huo kwa kuwashukuru washiriki wa kikao hicho kwa mawazo waliyotoa na kuahidi kuwa yote yaliyojadiliwa yamepokelewa na yatafanyiwa kazi.




Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, na Utawala Bora SACP. Ibrahim Mahumi akitoa hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi cha Wadau cha kuhakiki Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la mwaka 2025 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jijini Dodoma .


Wakurugenzi na Mameneja kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi (hayupo pichani), iliyolenga kufungua kikao kazi cha Wadau cha kuhakiki Kanuni za Kudumu  katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la mwaka 2025 Jijini Dodoma .


Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria,Ofisi ya Rais – UTUMISHI,Bi Hilda Kabissa akiwasihi wadau wa rasimu ya kanuni za kudumu katika Utumishi wa Umma kutoa maoni yatakayosaidia kuboresha rasimu ya kanuni hizo kwa manufaa ya Taifa.




Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bi Leila Mavika (aliyesimama) akifafanua jambo kuhusu rasimu ya kanuni za kudumu katika Utumishi wa Umma katika kikao kazi cha kuhakiki rasimu ya Kanuni hizo jijini Dodoma.




Wakurugenzi na Mameneja kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi (hayupo pichani), iliyolenga kufungua kikao kazi cha Wadau cha kuhakiki Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la mwaka 2025 Jijini Dodoma 

Mkurugenzi wa Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga akitoa maneno ya shukrani kwa wadau mbalimbali wa kikao kazi cha kuhakiki rasimu ya Kanuni za Kudumu  katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la mwaka 2025 kwa ushiriki wao alipokuwa akihitimisha kikao kazi hicho ambacho kilicholenga kupata maoni ya kuboresha kanuni hizo,



Mwenyekiti wa kikao cha wadau wa kuhakiki rasimu ya kanuni za kudumu katika utumishi wa Umma ambaye ni Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi Makumbusho ya Taifa, Bw. Zakariyya Kera (aliyesimama), akitoa ufafanuzi wa jambo alipokuwa akipokea maoni ya maboresho ya kanuni hizo kutoka kwa washiriki wa kikao hicho (hawapo pichani) mnamo tarehe 2, oktoba,2025 jijini Dodoma.



Baadhi ya wakurugenzi kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za umma wakifuatilia mjadala wa kutoa maoni  kutoka kwa washiriki wengine (hawapo pichani) ya kuboresha rasimu ya Kanuni za kudumu katika Utumishi wa Umma kwenye kikao cha wadau wa kuhakiki Kanuni hizo kilichofanyika Oktoba 2, 2025 jijini Dodoma 


Meza kuu ambayo imemjumuisha Mwenyekiti wa kikao hicho, (aliyekaa katikati), mtunza muda, (wa kwanza kutoka kulia) na Mkurugenzi wa Undelezaji Sera Ofisi ya Rais – UTUMISHI, (wa kwanza kutoka kushoto) wakifuatilia maoni mbalimbali ya uboreshaji wa kanuni za kudumu katika Utumishi wa Umma yalikuwa yakitolewa na wadau waliokuwa wanafanya mapitio ya kanuni hizo jana tarehe 2 oktoba,2025, jijini Dodoma


Baadhi ya washiriki ambao ni Wakurugenzi wa Rasilimaliwatu wakiunga mkono hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na wadau wa kuhakiki rasimu ya Kanuni za Kudumu  katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la mwaka 2025 (hawapo pichani) kilichofanyika tarehe 2,oktoba,2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Jijini Dodoma .

 

Mwakilishi wa Meneja sehemu ya Utawala Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Bi Hawa Goronya akitoa maoni juu ya maboresho ya Kanuni za kudumu za Utumishi wa Umma   katika kikao kazi cha Wadau cha kuhakiki Kanuni hizoToleo la Nne la mwaka 2025 kilichofanyika oktoba 2,2025 jijini Dodoma.

Baadhi ya wajumbe kutoka Sekretarieti Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi (hayupo pichani), iliyolenga kufungua kikao kazi cha Wadau cha kuhakiki Kanuni za Kudumu  katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la mwaka 2025 Jijini Dodoma .


Mchumi Mwandamizi, Bw. Mwendesha Makelemelo kutoka Ofisi ya Rais – UTUMISHI,akitoa wasilisho la maboresho ya Kanuni za kudumu katika Utumishi wa Umma kwenye kikao kazi cha wadau (hawapo pichani) kilichofanyika oktoba 2,2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji uliopo Mtumba Dodoma.  

Mkurugenzi wa Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga kakiteta jambo na Afisa Habari Mwandamizi Bw Reiner Budodi  wa Ofisi hiyo katika kikao kazi cha Wadau cha kuhakiki Kanuni hizoToleo la Nne la mwaka 2025 kilichofanyika oktoba 2,2025 jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment