Wednesday, October 29, 2025

WATENDAJI WAKUU OFISI YA RAIS-UTUMISHI WAPIGA KURA, KATIBU MKUU MKOMI ATOA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA NA WANANCHI KUJITOKEZA KUTIMIZA HAKI YAO YA KIKATIBA

Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi -Dodoma

Tarehe 29 Oktoba, 2025

Watendaji Wakuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora leo tarehe 29.10.2025 wameshiriki zoezi la kupiga kura katika Vituo mbalimbali na kuchagua Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani.

Akishiriki zoezi hilo katika Kituo cha Kupiga Kura cha Msangalale Mashariki, Kata ya Dodoma Makulu, jijini Dodoma, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa Watumishi wa Umma na Wananchi kujitokeza kuchagua viongozi wanaowahitaji kwa maendeleo ya Taifa.

“Namshukuru Mungu nimeshikiri salama zoezi hili muhimu la Kikatiba, nipende kutoa wito kwa Watumishi wa Umma na Wananchi kwa ujumla kushikiriki pia kwani ni haki yao ya msingi.” Bw. Mkomi amesisitiza.

Amesema hali katika Kituo hicho ni ya utulivu na wananchi wamekua wakimiminika kwenda kupiga kura hivyo amewasisitiza kila mwenye haki ya kushiriki zoezi hilo afanye hivyo.

Aidha, Bw. Mkomi amewapongeza Waratibu wa zoezi hilo katika Kituo hicho kwa kuonyesha ushirikiano kwa wananchi wanaoenda kushiriki katika zoezi hilo na kuhakikisha kila mwenye sifa anashiriki kikamilifu.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi ameshiriki zoezi hili muhimu katika Kituo cha Mwatano, Kata ya Miyuji, Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiweka fomu ya kupiga Kura katika sanduku la Kura mara baada ya kushiriki zoezi hilo la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akiweka fomu ya kupiga Kura katika sanduku la Kura mara baada ya kushiriki zoezi hilo la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akipokea fomu ya kushiriki kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (aliyesimama) akisubiri kupatiwa fomu ya kushiriki kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akionesha jina lake katika orodha ya wapiga Kura iliyobandikwa katika kituo hicho kabla ya kushiriki kupiga kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akishiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akionesha kadi yake ya kupiga Kura kabla ya kushiriki zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akihakiki jina na picha yake kwenye daftari la kudumu kabla ya kushiriki zoezi la kupiga Kura katika Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akipakwa wino mara baada ya kushiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi kwenye ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (wa kwanza kushoto) akipokea fomu ya kushiriki kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akionesha kidole kilichopakwa wino mara baada ya kushiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi kwenye ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.

 



No comments:

Post a Comment