Na.Lusungu Helela-
Dar es Salaam
Mkurugenzi wa
Usimamizi wa Maadili, Ofisi Rais, UTUMISHI, Bi.Felister Shuli amewaasa
Watumishi wa Umma nchini kuacha tabia ya kukopa kupita kiasi huku akisisitiza
kuwa kitendo hicho ni kinyume na maadili katika Utumishi wa Umma nchini.
Mkurugenzi Shuli
ametoa kauli hiyo leo Jumanne Agosti 26, 2025 jijini Dar es Salaam wakati
akiwasilisha mada ya Maadili katika Utumishi wa Umma katika Mkutano wa 13 wa
Chama Cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka ( TRAMPA) unaotarajiwa
kufunguliwa rasmi kesho na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mhe.Kassim Majaliwa.
Amesema kitendo
hicho cha Mtumishi kukopa kupita kiasi humpelekea kupata msongo wa mawazo
na kusababisha kuwahudumia wateja kwa ukali au kwa kukosa staha kutokana
msongo wa mawazo alionao unaosababishwa na madeni
Ameongeza kuwa
baadhi ya Watumishi waliokopa kupita kiasi hujikuta ni watu wa kuhangaika
hangaika na muda mwingine huwa na mahudhurio hafifu kazini "
huwa ni watu wa kujificha na kukimbia kimbia ili wadai wake
wasiweze kuwaona kwani baadhi ya wadai wao huwafuata ofisini"
amesema
Kufuatia hatua
hiyo, Bi.Shuli amewataka Watumishi kuishi kulingana na kipato chao ili wasiweze
kujiingiza kwenye madeni yasiyolipika na hivyo kusababisha kushindwa
kutoa huduma bora kwa wananchi.
Katika hatua
nyingine, Bi.Shuli amewataka watumishi wa umma kujiepusha na michezo ya bahati nasibu na kubashiri (
betting ) kwani ni ukiukwaji wa Maadili katika Utumishi wa Umma nchini
" Jiepusheni
na "betting" kwani watumishi wanaocheza michezo hiyo hujikuta
wakitumia muda mwingi na fedha nyingi kucheza michezo hiyo na hivyo kusababisha
kukopa kupita kiasi.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi Rais,
UTUMISHI, Bi.Felister Shuli akizungumza
leo jijini Dar es Salaam wakati
akiwasilisha mada ya Maadili katika Utumishi wa Umma katika Mkutano wa 13 wa
Chama Cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka ( TRAMPA) unaotarajiwa
kufunguliwa rasmi kesho na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mhe.Kassim Majaliwa.
Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Menejimenti ya
Kumbukumbu na Nyaraka (TRAMPA)
wakimsikiliza Mkurugenzi wa Usimamizi
wa Maadili, Ofisi Rais, UTUMISHI,
Bi.Felister Shuli wakati
akiwasilisha mada ya Maadili katika Utumishi wa Umma katika Mkutano wa 13
wa TRAMPA unaotarajiwa kufunguliwa rasmi
kesho na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa.
Rais wa Chama
cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka (TRAMPA) Bi. Devotha Mrope akizungumza na Wanachama wa TRAMPA
kwenye Mkutano wa 13 wa TRAMPA ulioanza jana na unaotarajiwa kufunguliwa rasmi kesho na
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Utumishi wa
Umma kutoka Ofisi Rais, UTUMISHI, Bw. Andrew Ponda akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akiwasilisha mada
ya masuala ya Uhamisho kwa njia ya mfumo
katika Mkutano wa 13 wa Chama Cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka (
TRAMPA) unaotarajiwa kufunguliwa rasmi kesho na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa
No comments:
Post a Comment