Thursday, August 21, 2025

UTEKELEZAJI WA MRADI WA UJENZI WA MAKAZI YA WATUMISHI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MPWAPWA

 HABARI KATIKA PICHA

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akizungumza jambo na Afisa Usimamizi wa Fedha Mwandamizi kutoka Wizara ya fedha, Bw. Ezekiel Odipo (wakwanza kushoto) wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma katika Shule ya Sekondari Lumuma Green, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.


Mwonekano wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma lililopo katika Shule ya Sekondari Lumuma Green, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.


Fundi mkuu anayejenga makazi ya watumishi wa umma, katika Shule ya Msingi Chaludewa, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Bw. Fadhili Kabainda (wapili kutoka kulia) akifafanua jambo kwa Mhandisi Salum Chanzi kutoka Watumishi Housing Investments (wakwanza kulia) wakati wa ziara ya timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments iliyolenga kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma katika Halmashauri hiyo mkoani Dodoma.


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Watumishi Housing Investments ikijadili jambo wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma katika Shule ya Sekondari Lumuma Green, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.


Mwonekano wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma lililopo katika Shule ya Msingi Chaludewa, kijiji cha Mlunduzi, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wakwanza kulia) akisisitiza jambo kwa Mtakwimu Mwandamizi Bw. Ombeni Kasayo (wapili kutoka kushoto) na Mchumi Mwandamizi kutoka Watumishi Housing Investments, Bw. Damian Mnenwa (wakwanza kushoto) mara baada ya timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na WHI kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma katika Kijiji cha Ludewa, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.

 



No comments:

Post a Comment