Monday, May 9, 2022

TANZANIA NCHI YA KWANZA BARANI AFRIKA KUFANYIWA MAJARIBIO YA MATUMIZI YA NYENZO YA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA AFRIKA WA MAADILI NA MISINGI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA

Na. James K. Mwanamyoto-Dar es Salaam

Tarehe 10 Mei, 2022

Tanzania imependekezwa na Sekretarieti ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika kufanyiwa majaribio ya matumizi ya Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala ambayo itakuwa ikitumika kuzitathmini nchi wanachama za Umoja wa Afrika.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ya namna bora ya kutumia Nyenzo hiyo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala.

Mhe. Jenista amesema Umoja wa Afrika (AU) umeliheshimisha taifa letu kwa kutoa fursa ya kuwa nchi ya kwanza Barani Afrika kufanyiwa majaribio ya kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala, ambao utaziwezesha Nchi Wanachama kuandaa taarifa itakayokuwa ikizingatia misingi iliyoainishwa kwenye Mkataba huo.

Waziri Jenista amesema, Nchi Wanachama za Umoja wa Afrika zilikubaliana kutengeneza Nyenzo ambayo itatumika kusaidia kupima utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala katika nchi zote wanachama.

Mhe. Jenista ameongeza kuwa, Mkataba huo unahimiza uzingatiaji wa maadili katika Utumishi wa Umma katika maeneo mbalimbali likwemo eneo la mapambano dhidi ya rushwa, uzingatiaji wa sheria na utawala bora kwa ujumla.

Waziri Jenista amesema, semina hiyo ni fursa ya kipekee kwa Watendaji wa pande zote mbili za Muungano kwenye Ofisi zinazoshughulikia masuala ya Utumishi wa Umma kuangalia ni kwa namna gani wataweza kuitumia Nyenzo hiyo vizuri katika kuandaa ripoti ambayo itawasilishwa Umoja wa Afrika.

“Jambo kubwa hapa, ni nchi yetu kuwa ya kwanza kuitumia Nyenzo hiyo, kupata mafunzo ya kuitumia pamoja na kuwa wa kwanza kutathminiwa  kwa namna gani tumeitumia Nyenzo hiyo kuandaa taarifa itakayowasilishwa Umoja wa Afrika.” Mhe. Jenista ameongeza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye Idara yake ina jukumu la kusimamia utekelezaji wa Mkataba huo, Bi. Agnes Meena amesema baada ya kukamilika kwa semina hiyo, wanatarajia kuandaa taarifa nzuri ya nchi itakayokuwa ya kwanza Afrika kwa kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala.

Naye Mshiriki wa semina hiyo kutoka Tanzania Bara, Bw. Romwald Rwamarumba amesema Tanzania imekuwa ni nchi ya kwanza Barani Afrika kufanyiwa majaribio ya kutumia Nyenzo hiyo, hivyo taarifa itakayoandaliwa na nchi itakuwa ya kwanza Barani Afrika ilizozingatia misingi iliyowekwa kwa mujibu wa Mkataba.

Ameongeza kuwa, taarifa hiyo itatumiwa pia na nchi wanachama Barani Afrika kama rejea ya uandaaji wa taarifa za utekelezaji wa mkataba huo kwenye nchi zao.

Kwa upande wake mshiriki kutoka Zanzibar, Bi. Fatma Saadalla amesema, semina hiyo itasaidia kuwajengea uelewa wa Mkataba huo na namna ya kutumia Nyenzo iliyopendekezwa kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala.

Semina hiyo ya siku nne imeandaliwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kushirikiana na Kamisheni ya Umoja wa Afrika na imewashirikisha wajumbe kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akifungua semina ya kuwajengea uwezo wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wa namna bora ya kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala iliyoanza leo jijini Dar es Salaam. 


Wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wataalam hao juu ya namna bora ya kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala iliyoanza leo jijini Dar es Salaam. 


Mwakilishi wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Bw. Issaka Garba Abdou akielezea sababu ya Tanzania kupendekezwa na Sekretarieti ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika kufanyiwa majaribio ya matumizi ya Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar iliyoanza leo jijini Dar es Salaam. 


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, Bi. Agnes Meena akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama kufungua semina ya kuwajengea uwezo wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar juu ya namna bora ya kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala iliyoanza leo jijini Dar es Salaam. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wanaoshiriki semina ya kujengewa uwezo wa kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala iliyoanza leo jijini Dar es Salaam. 


Afisa Mipango Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais-Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Fatma Mzee Saadalla akielezea umuhimu wa semina ya kuwajengea uwezo wa kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala iliyoanza leo jijini Dar es Salaam. 


Afisa Utumishi kutoka Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Tanzania Bara, Bw. Romwald Rwamarumba, Tanzania Bara, Bw. Romwald Mwamarumba akielezea umuhimu wa semina ya kuwajengea uwezo wa kutumia Nyenzo ya Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala iliyoanza leo jijini Dar es Salaam. 


 

No comments:

Post a Comment