Friday, April 29, 2022

BW. HASSAN SHAIBU MFANYAKAZI HODARI WA OFISI YA RAIS - UTUMISHI KWA MWAKA 2021/2022

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwasalimia watumishi wa Ofisi yake jijini Dodoma kabla ya kuanza kwa kikao cha kumchagua mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022.  

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na watumishi wa ofisi yake kwenye kikao cha kumchagua mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022. 

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora, Bw. Mussa Magufuli akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu, ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma, Dkt. Laurean Ndumbaro kuzungumza na watumishi wa ofisi hiyo wakati wa kikao cha kumchagua mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022. 


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo wa Ofisi ya Rais Memeijimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) kwenye kikao cha kumchagua mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais Memeijimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akimtangaza mfanyakazi hodari wa Ofisi yake kwa mwaka 2021/2022.

 

Mfanyakazi hodari wa Ofisi ya Rais Memeijimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Hassan Shaibu akiwa amesimama mbele ya Watumishi wenzake kuwashukuru mara baada ya kuchaguliwa kuwa mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022.  

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt.Laurean Ndumbaro (wapili kutoka kushoto) akiwaongoza wasimamizi waliokuwa wakizihesabu kura baada ya kumchagua mfanyakazi hodari wa ofisi yake.  Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utawala Rasilimaliwatu Bw. Mussa Magufuli na kushoto kwake ni Mwakilishi wa TUGHE Tawi la Utumishi Bi. Mwadawa Nchemwa.

Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais - Memeijimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimpongeza mtumishi mwenzao Bw. Hassan Shaibu (watatu kutoka kushoto) baada ya kutangazwa kuwa mfanyakazi hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022. 


Mwakilishi wa TUGHE Tawi la Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bi. Mwadawa Nchemwa akiwafahamisha watumishi wa Ofisi hiyo vigezo vya kumpata mfanyakazi hodari wakati wa kikao cha kuchagua mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022.  Wakwanza kulia kwake ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt.Laurean Ndumbaro na wapili kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Bw. Mussa Magufuli.

Mmoja kati wa wasimamizi wa uchaguzi wa kumpata mfanyakazi hodari wa   Ofisi ya Rais Memeijimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Elibariki Kahungya akigawa karatasi za kupigia kura kwa ajili ya kumpata mtumishi mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo kwa mwaka 2021/2022.

 


 

 



 












No comments:

Post a Comment