Monday, May 3, 2021

IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA YATAKIWA KUBORESHA MIFUMO YA KIDIGITALI KUIMARISHA USALAMA WA NYARAKA ZA TAIFA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na Watumishi wa Kituo cha Kumbukumbu Tuli Kanda ya Ziwa kilichopo Jijini Mwanza wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma mkoani humo. 


Baadhi ya Watumishi wa Kituo cha Kumbukumbu Tuli Kanda ya Ziwa kilichopo Jijini Mwanza wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma mkoani humo.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi akiwasilisha kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa taarifa ya utekelezaji wa Kituo cha Kumbukumbu Tuli Kanda ya Ziwa kilichopo Jijini Mwanza wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma mkoani humo. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiangalia moja ya nyaraka zinazotunzwa katika Kituo cha Kumbukumbu Tuli Kanda ya Ziwa kilichopo Jijini Mwanza wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma mkoani humo.


 

No comments:

Post a Comment