Saturday, March 16, 2019

WAKURUGENZI WATENDAJI WA HALMASHAURI NCHINI WATAKIWA KUHAKIKISHA FEDHA ZA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI ZINAWAFIKIA WALENGWA



Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Jason Rweikiza (Mb) akizungumza na wananchi na wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wa kijiji cha Namela Manispaa ya Mtwara wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Mtwara.

Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wa kijiji cha Namela Manispaa ya Mtwara wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Jason Rweikiza (Mb) alipokuwa akizungumza nao kuhusu umuhimu wa TASAF wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Mtwara.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiwahimiza wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kuzitumia vizuri ruzuku wanayoipata.


No comments:

Post a Comment