Thursday, October 10, 2024

KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WADAU KUTOA MAONI KATIKA MFUMO WA TATHMINI YA MAHITAJI YA RASILIMALIWATU ILI KUBORESHA UTENDAJI KATIKA UTUMISHI WA UMMA

 Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 10 Oktoba, 2024

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amesema Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu utaisaidia Serikali kufanya msawazo katika Utumishi wa Umma ili kuwa na mtawanyo mzuri wa watumishi kwa lengo la kuboresha utendaji katika utumishi wa umma.

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akifungua kikao kazi cha kujadili matokeo ya tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu katika utumishi wa umma kwa Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara zote, wataalamu wanaosimamia uandaaji na ujazaji wa mahitaji ya watumishi kutoka wizara zote pamoja na Wakurugenzi na wataalamu kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

Bw. Mkomi amesema kila Mkurugenzi anafahamu umuhimu wa mahitaji ya rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma na kuwasihi wafanye tathmini ya kutosha.

“Ukisema una watumishi wachache, tutakuuliza unahitaji watumishi wangapi? kwani unatakiwa uwe umefanya tathmini ya kutosha kwasababu inawezekana kumhitaji kwako mtumishi au kutokumhitaji kunatokana na matakwa yako na si mfumo unaokufahamisha kuwa mtumishi huyu ni wa ziada.” Bw. Mkomi amesema.

Bw. Mkomi amesema msawazo katika utumishi wa umma unahitajika kufanywa katika maeneo mawili ikiwemo mjini ili kutokuwa na watumishi wa ziada ambao hawana majukumu ya kutosha katika maeneo yao ya kazi lakini pia msawazo huo utasaidia kuunganisha familia.

Bw. Mkomi ameongeza kuwa, msawazo hautaweza kufanyika bila kuwa na taarifa halisi ya mahitaji na idadi ya watumishi waliopo katika maeneo husika hivyo, ni vizuri washiriki wakaangalia namna ya kufanya kwani inatakiwa kujua watumishi wangapi wanahitajika wapi, wakafanye nini na baada ya kujua hayo itapatikana nafasi nzuri ya kuboresha. 

“Niwatake mshiriki kikamilifu kwa kuipokea taarifa hiyo, kuichambua na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha Mfumo huo utakaowezesha kuwa na mtawanyo mzuri wa watumishi katika Taasisi za Umma.” Bw. Mkomi amesisitiza.

Akitoa neno la utangulizi, Mkurugenzi wa Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda ameelezea lengo la kikao kazi hicho kuwa ni kujadili matokeo ya tathmini ya Rasilimaliwatu katika Taasisi za Umma ili kupata maoni toka kwa wadau hao na kuboresha mfumo huo katika Utumishi wa Umma kwa masilahi mapana ya taifa.  

Kikao kazi hicho kilichoanza leo kinafanyika kwa muda wa siku mbili ambapo mada mbalimbali zitawasilishwa ikiwemo Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma, matokeo ya Wizara na vigezo kwa upande wa Wizara na Makundi ya Taasisi.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo.

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kufungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (kulia) akiwa katika kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kabla ya kufungua kikao hicho kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji  Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda 

Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi wakati akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo.

Baadhi ya Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi wakati akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Felista Shuli akijibu moja ya hoja iliyowasilishwa wakati wa kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Felista Shuli akijibu moja ya hoja iliyowasilishwa wakati wa kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini mara baada ya kufungua kikao hicho kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda.

Sehemu ya washiriki wa kikao kazi cha kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dodoma leo.

Afisa Tawala Mwandamizi, Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Waziri Mkumbo akiwasilisha mada kwa Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kuhusu Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma wakati wa kikao kazi cha kujadili matokeo ya tathmini hiyo kilichofanyika jijini Dodoma leo.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Wizara ya Kilimo, Bw. Philbert Lutale akichangia mada wakati wa kikao kazi cha Wakurugenzi wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Wizara ya Fedha, ambaye ni Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Wakurugenzi wa Idara ya Rasilimaliwatu wa Wizara zote, Bw. Lusius Mwenda (kulia) akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi cha Wakurugenzi hao na Maafisa Utumishi kutoka serikalini kilicholenga kujadili Matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma leo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda.


WAZIRI SIMBACHAWENE AWASIHI WATUMISHI KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA



 

VIONGOZI WAKUU WA OFISI YA RAIS, UTUMISHI NA UTAWALA BORA WAPOKEA VIKOMBE VYA USHINDI