Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Chalinze
Tarehe 24 Januari, 2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema
uzinduzi wa jengo la TAKUKURU katika Halmashauri
ya Chalinze ni hatua muhimu inayothibitisha dhamira ya Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia
Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuimarisha
mazingira ya utendaji kazi, kuongeza ufanisi pamoja na kutoa huduma bora kwa
wananchi ili kuleta Maendeleo ya Watanzania.
Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo Mkoani Pwani katika Halmashauri ya Chalinze wakati akizindua jengo la Ofisi ya TAKUKURU ambalo litaboresha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi wa TAKUKURU ikiwemo utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Mhe Kikwete amesema kuwa, Serikali imewawezesha TAKUKURU kwa kiwango kikubwa sana hivyo amewaasa kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa bidii na weledi zaidi ili dhamira ya Serikali ya kuitokomeza rushwa nchini pamoja na maono ya TAKUKURU ya kuwa na Tanzania isiyo na rushwa yaweze kufikiwa.
Vilevile, Mhe. Kikwete ametoa wito kwa Watumishi wa TAKUKURU Chalinze pamoja na Mikoa na Wilaya ambazo kuna majengo mapya kutunza na kuthamini majengo hayo pamoja na vitendea kazi vyote vilivyomo ili viweze kutumika hata na vizazi vijavyo.
Aidha, ametoa wito kwa taasisi ya TAKUKURU, Sekta za Umma na Watanzania wote kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha fedha za Serikali zinazotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri zinatumika kulingana na malengo yaliyowekwa.
Amesema, utaratibu huo ni muhimu katika kuongeza uwazi na uwajibikaji na hivyo kuziba mianya ya rushwa na kuongeza ushiriki wa Wananchi katika kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa ipasavyo.
Akihitimisha hotuba yake, Waziri Kikwete amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila pamoja na watendaji wa taasisi hiyo kwa uadilifu na weledi unaoonekana katika usimamizi wa ujenzi wa jengo hilo.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila amesema
Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye ujenzi wa majengo katika wilaya na
mikoa mbalimbali nchini na hii ni kuonesha utashi wa Mhe. Rais katika mapambano
dhidi ya rushwa nchini.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Watumishi na Wananchi wakati
akizindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri
ya Chalinze Mkoani Pwani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali na Watumishi alipowasili kwa ajili ya kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani
Baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Watumishi
na Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza nao kabla ya kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu
kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa
TAKUKURU, Bw. Crispian Chalamila (kushoto) kabla ya Waziri huyo kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu
kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge kabla ya Waziri huyo kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani
Mkurugenzi Mtendaji wa TAKUKURU, Bw. Crispian Chalamila akitoa neno la utangulizi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuzungumza na kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi na Watumishi wa TAKUKURU mara baada ya kuzindua jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.
Muonekano wa nje wa jengo la Ofisi za TAKUKURU lililopo Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani ambalo
uzinduzi wake umefanywa na Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete leo
tarehe 24 January, 2026.
Kaimu Mkurugenzi wa Milki, Bw. Frank Mkiranya akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuhusu utelezaji wa Ujenzi wa Mradi wa
Jengo la Ofisi ya TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.
Baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Watumishi
na Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza nao kabla ya kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu
kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akikata utepe alipokuwa akizindua Jengo la TAKUKURU Mkoa wa Pwani ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze
Mkoani Pwani.











