Saturday, January 24, 2026

SERIKALI KUIMARISHA UFANISI WA UTENDAJI KAZI KUPITIA UJENZI WA OFISI ZA TAKUKURU

 Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Chalinze

Tarehe 24 Januari, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema uzinduzi wa jengo la TAKUKURU katika Halmashauri ya Chalinze ni hatua muhimu inayothibitisha dhamira ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuimarisha mazingira ya utendaji kazi, kuongeza ufanisi pamoja na kutoa huduma bora kwa wananchi ili kuleta Maendeleo ya Watanzania.

Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo Mkoani Pwani katika Halmashauri ya Chalinze wakati akizindua jengo la Ofisi ya TAKUKURU ambalo litaboresha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi wa TAKUKURU ikiwemo utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Mhe Kikwete amesema kuwa, Serikali imewawezesha TAKUKURU kwa kiwango kikubwa sana hivyo amewaasa kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa bidii na weledi zaidi ili dhamira ya Serikali ya kuitokomeza rushwa nchini pamoja na maono ya TAKUKURU ya kuwa na Tanzania isiyo na rushwa yaweze kufikiwa.

Vilevile, Mhe. Kikwete ametoa wito kwa Watumishi wa TAKUKURU Chalinze pamoja na Mikoa na Wilaya ambazo kuna majengo mapya kutunza na kuthamini majengo hayo pamoja na vitendea kazi vyote vilivyomo ili viweze kutumika hata na vizazi vijavyo.

Aidha, ametoa wito kwa taasisi ya TAKUKURU, Sekta za Umma na  Watanzania wote kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha fedha za Serikali zinazotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri zinatumika kulingana na malengo yaliyowekwa.

Amesema, utaratibu huo ni muhimu katika kuongeza uwazi na uwajibikaji na hivyo kuziba mianya ya rushwa na kuongeza ushiriki wa Wananchi katika kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa ipasavyo.

Akihitimisha hotuba yake, Waziri Kikwete amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila pamoja na watendaji wa taasisi hiyo kwa uadilifu na weledi unaoonekana katika usimamizi wa ujenzi wa jengo hilo.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila amesema Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye ujenzi wa majengo katika wilaya na mikoa mbalimbali nchini na hii ni kuonesha utashi wa Mhe. Rais katika mapambano dhidi ya rushwa nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Watumishi na Wananchi wakati akizindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali na Watumishi alipowasili kwa ajili ya kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani

Baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Watumishi na Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza nao kabla ya kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispian Chalamila (kushoto) kabla ya Waziri huyo kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge kabla ya Waziri huyo kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani


Mkurugenzi Mtendaji wa TAKUKURU, Bw. Crispian Chalamila akitoa neno la utangulizi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuzungumza na kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi na Watumishi  wa TAKUKURU mara baada ya kuzindua jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.

Muonekano wa nje wa jengo la Ofisi za TAKUKURU lililopo Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani ambalo uzinduzi wake umefanywa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete leo tarehe 24 January, 2026.

Kaimu Mkurugenzi wa Milki, Bw. Frank Mkiranya akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuhusu utelezaji wa Ujenzi wa Mradi wa Jengo la Ofisi ya TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.

Baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Watumishi na Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza nao kabla ya kuzindua Jengo la TAKUKURU ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akikata utepe alipokuwa akizindua Jengo la TAKUKURU Mkoa wa Pwani ambalo ni Kituo maalumu kilichopo katika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Friday, January 23, 2026

WATUMISHI WA UMMA WAANDALIWE KUWA VIONGOZI-MHE. KIKWETE

 Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dar es salaam

Tarehe 23 Januari, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema ni muhimu kwa Taasisi ya UONGOZI kuendelea kuwaandalia program za Uongozi Watumishi wa Umma wenye mwelekeo wa Uongozi “leadership potential” ili kuwa na Viongozi watakaokuwa na uzalendo na weledi katika taifa.

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dar es salaam alipotembelea taasisi hiyo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Mhe. Kikwete amesema, uamuzi wa kushirikisha wafanyakazi wa Taasisi za Umma, binafsi na za kiraia  katika program hizo unatoa fursa kwa washiriki hao kubadilishana uzoefu na kuboresha utendaji.

Amesema ni wakati sahihi wa kuweka mikakati ya ujenzi wa Kituo cha Uongozi (Leadership Center) ambacho  zaidi kitawajengaViongozi katika Utumishi wa Umma.

Akihitimisha hotuba yake Mhe. Kikwete ameipongeza Menejimenti na Watumishi wote wa Taasisi ya Uongozi kwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua katika nafasi ya Naibu Waziri wa Ofisi hiyo ambapo ameomba ushirikiano Ili kwa pamoja waweze kumsaidia Rais katika kutekeleza majukumu ya Utumishi na Utawala Bora.

Awali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake, aliwashukuru Viongozi hao kwa kuwatembelea na kuhimiza uwajibikaji na kuahidi kuyafanya kazi maelekezo watakayopewa.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa Taasisi ya UONGOZI (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa katika ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo baada ya kuwasili Taasisi ya UONGOZI jijini Dar es Salaam katika ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza Uwajibikaji kwa watumishi wa Ofisi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akiteta jambo na Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka (kushoto) baada ya Waziri huyo kuzungumza na watumishi wa Taasisi ya UONGOZI wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akimuonesha kitabu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) wakati Waziri huyo alipokuwa akipitishwa kwenye baadhi ya Idara za Taasisi hiyo wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji. Kushoto ni Naibu Waziri wake Mhe, Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji. Wa pili kulia waliokaa ni Naibu Waziri wake, Mhe. Regina Qwaray na wa pili kushoto waliokaa ni Katibu Mkuu-IKULU Bw. Mululi Mahendeka.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa taasisi yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Sehemu ya Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI jijini Dar es Salaam wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mh. Regina Qwaray ili amkaribishe Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) kwa ajili ya kuzungumza na Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Sehemu ya Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI wakifuatilia wasilisho la taarifa ya utekelezaji wa taasisi hiyo iliyowasilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Bw. Kadari Singo (hayupo pichani) wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete iliyolenga kuhimiza uwajibikaji jijini Dar es Salaam.




Wednesday, January 21, 2026

WAZIRI KIKWETE AMTEMBELEA MAMA SALMA OMAR ALI JUMA NA MAMA REGINA LOWASSA

Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi-Dar es salaam

Tarehe 22 Januari, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewatembelea na kuwajulia hali Mama Salma Omar Ali Juma, Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam na Mama Regina Lowassa, Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam leo Januari 22, 2026.

Mhe. Kikwete amesema, Ofisi ya Rais-UTUMISHI inazingatia maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuthamini mchango wa Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu pamoja na wajane wa Viongozi hao Wastaafu ikiwa ni pamoja na kuwatunza kwa mujibu wa Sheria.

 “Mhe. Rais yupo pamoja nanyi na amenielekeza kufikisha salamu zake kwenu kwa kuwajulia hali, kusikiliza changamoto zilizopo na kuzitafutia ufumbuzi kwa kuwa anathamni mchango wa Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu pamoja na wenza wa Viongozi hao” amesema Mhe. Kikwete

Kwa upande wake, Mama Regina Lowassa, Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemshukuru na kumpongeza Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuijali familia ya Hayati Edward Lowassa wakati wote bila kuchoka.

 “Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa pamoja nasi wakati wote, nitoe shukrani kwa niaba ya familia kwa hekima na busara ambazo mnatumia katika kutuhudumia Wenza wa Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu,”Amesema Mama Lowassa

 Aidha, Mama Salma Omar Ali Juma, Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemshukuru Mhe. Kikwete kwa kupata nafasi ya kumtembelea na kumjulia hali na kumuomba amfikishie salamu za shukrani Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufuatilia kwa karibu masuala yanayowahusu na kuyatafutia ufumbuzi kupitia Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akizungumza jambo na Mama Salma Omar Ali Juma (kushoto), Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifurahia jambo na Mama Regina Lowassa (kulia), Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati alipomtembelea nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam kumjulia hali ikiwa ni utekelezaji wa majukumu yake leo tarehe 22 Januari, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mama Salma Omar Ali Juma (wa pili kutoka kulia), Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wengine ni Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mama Regina Lowassa, Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (kulia) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) alipomtembelea nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake

Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono (kushoto) akifurahia jambo wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipomtembelea Mama Salma Omar Ali Juma (hayupo pichani), Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mama Regina Lowassa (katikati), Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Januari, 2026. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mama Salma Omar Ali Juma (kushoto), Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Msasani Jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Januari, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na  Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipomtembelea Mama Regina Lowassa, Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam kumjulia hali ikiwa ni utekelezaji wa majukumu yake leo tarehe 22 Januari, 2026.

Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora Wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza na Mama Regina Lowassa Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Januari, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mama Salma Omar Ali Juma (wa pili kushoto), Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Msasani Jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Januari, 2026. Kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Hilda Kabissa na kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono.

  


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiagana na Mama Regina Lowassa, Mjane wa Hayati Edward Ngoyai Lowassa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati alipomtembelea nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam kumjulia hali ikiwa ni utekelezaji wa majukumu yake leo tarehe 22 Januari, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiagana na Mama Salma Omar Ali Juma, Mjane wa Hayati Dkt. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati alipomtembelea nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam kumjulia hali ikiwa ni utekelezaji wa majukumu yake leo tarehe 22 Januari, 2026