Wednesday, December 31, 2025
Wednesday, December 24, 2025
Monday, December 15, 2025
MKOMI ATOA WITO KWA WATUMISHI KUJICHUNGUZA KAMA WANAFAA KUWA VIONGOZI
Na.Mwandishi Wetu
Tarehe 15 Disemba, 2025
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Bw. Juma Mkomi amesema kuwa mtumishi wa umma anaweza kujifanyia uchunguzi (vetting)
mwenyewe juu ya tabia na mwenendo katika utendaji kazi bila kusubiri taarifa ya
vyombo vya usalama.
Bw. Mkomi
alisema hayo Desemba 15, 2025 kwa Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa kuhitimisha
mafunzo ya uelewa wa namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi yaliyofanyika
Mtumba jijini Dodoma.
“Mtumishi anaweza kujichunguza na kuona kama anafaa kuwa kiongozi
au la, kwa sababu tabia njema au mbaya anaweza kuitambua kwa ufasaha mtumishi
mwenyewe” alisema Bw. Mkomi.
Bw. Mkomi aliongeza kuwa tabia na mienendo ya watumishi
inatakiwa kuwa na taswira chanya kwao wenyewe na mbele ya macho ya wale
wanaopokea huduma kutoka kwao.
Aidha, Bw. Mkomi alisisitiza kuwa tabia na mienendo ya
watumishi wa ofisi hiyo inatakiwa kwenda sambamba na misingi mikuu ya utendaji
kazi wa ofisi, pia tabia hizo zitoe mitazamo chanya juu ya utendaji kazi wao na
namna anavyowahudumia watumishi wa umma na umma kwa jumla.
Awali, Mkufunzi Bw. Moses Raymond alisema kuwa Watumishi wa Ofisi ya Rais UTUMISHI ni kioo kwa
watumishi wengine wote katika utumishi wa umma na ndio wenye dhamana ya kusimamia
utumishi wa umma nchini. Hivyo, hawana budi kuwaongoza watumishi wengine vyema katika
ujenzi wa taswira chanya ya Serikali.
Alifafanua kuwa, mtumishi wa Ofisi ya Rais UTUMISHI akifanya
vibaya katika utoaji wa huduma, wananchi wanatafsiri kuwa watumishi wote wa
ofisi hiyo wana tabia hiyo.
“Binafsi natoa rai katika mafunzo haya kuhakikisha kila mmoja anashiriki ipasavyo katika jitihada
za ujenzi wa taswira nzuri ya ofisi kwa kufanya vyema hususani katika
utekelezaji wa majukumu yake ili kulinda taswira chanya ya ofisi” aliongeza Bw.
Raymond.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa
mafunzo ya uelewa yanayofanyika
kila Jumatatu ya Wiki katika Ofisi hiyo Mtumba
jijini Dodoma tarehe 15 Desemba,
2025.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw.
Juma Mkomi (Kulia) na Naibu Katibu Mkuu Bw. Xavier Daudi wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda
taswira nzuri ya taasisi wakati wa mafunzo ya uelewa yanaliyofanyika katika Ofisi
hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.
Viongozi
na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka
kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba,
2025.
Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.
Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi. Nyasinde Mkono akitoa neno la shukurani baada ya mafunzo ya namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.
.png)
.png)

