Monday, December 15, 2025

MKOMI ATOA WITO KWA WATUMISHI KUJICHUNGUZA KAMA WANAFAA KUWA VIONGOZI

 Na.Mwandishi Wetu

Tarehe 15 Disemba, 2025

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi amesema kuwa mtumishi wa umma anaweza kujifanyia uchunguzi (vetting) mwenyewe juu ya tabia na mwenendo katika utendaji kazi bila kusubiri taarifa ya vyombo vya usalama.

Bw. Mkomi alisema hayo Desemba 15, 2025 kwa Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa kuhitimisha mafunzo ya uelewa wa namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi yaliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

“Mtumishi anaweza kujichunguza na kuona kama anafaa kuwa kiongozi au la, kwa sababu tabia njema au mbaya anaweza kuitambua kwa ufasaha mtumishi mwenyewe” alisema Bw. Mkomi.

Bw. Mkomi aliongeza kuwa tabia na mienendo ya watumishi inatakiwa kuwa na taswira chanya kwao wenyewe na mbele ya macho ya wale wanaopokea huduma kutoka kwao.

Aidha, Bw. Mkomi alisisitiza kuwa tabia na mienendo ya watumishi wa ofisi hiyo inatakiwa kwenda sambamba na misingi mikuu ya utendaji kazi wa ofisi, pia tabia hizo zitoe mitazamo chanya juu ya utendaji kazi wao na namna anavyowahudumia watumishi wa umma na umma kwa jumla.

Awali, Mkufunzi Bw. Moses Raymond alisema kuwa Watumishi  wa Ofisi ya Rais UTUMISHI ni kioo kwa watumishi wengine wote katika utumishi wa umma na ndio wenye dhamana ya kusimamia utumishi wa umma nchini. Hivyo, hawana budi kuwaongoza watumishi wengine vyema katika ujenzi wa taswira chanya ya Serikali.

Alifafanua kuwa, mtumishi wa Ofisi ya Rais UTUMISHI akifanya vibaya katika utoaji wa huduma, wananchi wanatafsiri kuwa watumishi wote wa ofisi hiyo wana tabia hiyo.

“Binafsi natoa rai katika mafunzo haya kuhakikisha  kila mmoja anashiriki ipasavyo katika jitihada za ujenzi wa taswira nzuri ya ofisi kwa kufanya vyema hususani katika utekelezaji wa majukumu yake ili kulinda taswira chanya ya ofisi” aliongeza Bw. Raymond.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya uelewa yanayofanyika kila Jumatatu ya Wiki katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi (Kulia) na Naibu Katibu Mkuu Bw. Xavier Daudi wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi wakati wa mafunzo ya uelewa yanaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi (Katika Mbele) na Naibu Katibu Mkuu Bw. Xavier Daudi (Wa kwanza kushoto), Viongozi na Watumishi wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond (Hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.

Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi. Nyasinde Mkono  akitoa neno la shukurani baada ya mafunzo ya namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.