Friday, February 1, 2019

SERIKALI YAELEKEZA KUSIMAMISHWA KAZI MKUU WA IDARA YA UTAWALA NA UTUMISHI WA MANISPAA YA ILALA NA KUWACHUKULIA HATUA ZA KINIDHAMU WATUMISHI WENGINE WA MANISPAA HIYO



Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ofisini kwake jijini Dodoma leo kuhusu kusimamishwa kazi kwa Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Manispaa ya Ilala Bi. Benadeta Mwaikambo na kuwachukulia hatua za kinidhamu maofisa wanaohusika na Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro (kushoto) akifafanua kuhusu kusimamishwa kazi kwa Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Manispaa ya Ilala Bi. Benadeta Mwaikambo wakati akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ofisini kwake jijini Dodoma leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, ACP Ibrahim Mahumi na Mwandishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bi. Aneth Andrew.



TAASISI ZA UMMA ZATAKIWA KUZINGATIA USALAMA WA TAARIFA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERIKALI MTANDAO

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akifungua rasmi kikao kazi cha pili cha Serikali Mtandao kilichowajumuisha Watendaji Wakuu Serikalini katika ukumbi wa Chuo cha Sayansi ya Kompyuta, Habari na Mawasiliano uliopo Chuo Kikuu Dodoma.
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba akimkaribisha mgeni rasmi kufungua kikao kazi cha pili cha Serikali Mtandao kilichowajumuisha Watendaji Wakuu Serikalini katika ukumbi wa Chuo cha Sayansi ya Kompyuta, Habari na Mawasiliano uliopo Chuo Kikuu Dodoma.
Baadhi ya Watendaji Wakuu wa Taasisi serikalini wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha pili cha Serikali Mtandao katika ukumbi wa Chuo cha Sayansi ya Kompyuta, Habari na Mawasiliano uliopo Chuo Kikuu Dodoma. 
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Bilinith Mahenge akiwakaribisha katika mkoa wake wajumbe wa kikao kazi cha pili cha  Serikali Mtandao kabla ya kuanza kwa kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa Chuo cha Sayansi ya Kompyuta, Habari na Mawasiliano uliopo Chuo Kikuu Dodoma.
Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao, Dkt. Jabiri Bakari akizungumza kabla ya ufunguzi wa kikao kazi cha pili cha Serikali Mtandao katika ukumbi wa Chuo cha Sayansi ya Kompyuta, Habari na Mawasiliano uliopo Chuo Kikuu Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Bilinith Mahenge wakati wa kikao kazi cha pili cha Serikali Mtandao katika ukumbi wa Chuo cha Sayansi ya Kompyuta, Habari na Mawasiliano uliopo Chuo Kikuu Dodoma.