Friday, May 19, 2023

MHE. SIMBACHAWENE NA MHE. RIDHIWANI WAHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na Menejimenti hiyo kilicholenga kuhimiza uwajibikaji.


Sehemu ya Watendaji wa Tume ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (meza kuu katikati) alipokuwa akizungumza nao wakati wa kikao kazi cha Waziri huyo na watendaji hao kilicholenga kuhimiza uwajibikaji.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo kwa Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene na Menejimenti ya Tume hiyo kilicholenga kuhimiza uwajibikaji.


Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Mathew Kirama akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (katikati) wakati wa kikao kazi cha Waziri huyo na Menejimenti ya Tume hiyo kilichofanyika jijini Dodoma. Wa kwanza kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete.


Mtumishi wa Tume ya Utumishi wa Umma ambaye ni Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Confort Kimaro akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati wa kikao kazi cha Waziri huyo na Menejimenti ya Tume hiyo kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (katikati) na Naibu Waziri wake Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) wakisikiliza hoja zilizokuwa zikiwasilishwa na watumishi wa Tume ya Utumishi wa Umma wakati wa kikao kazi cha Waziri huyo na Menejimenti ya Tume hiyo kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji. Wa kwanza kushoto ni Katibu wa Tume wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Mathew Kirama.


Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Charles Mulamula (aliyevaa miwani) akieleza majukumu ya kitengo chake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi cha Waziri huyo na Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Umma kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kuhimmiza uwajibikaji.


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Richard Cheyo akieleza majukumu ya kitengo chake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachaene (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi cha Waziri huyo na Menejimenti ya Utumishi wa Umma kilicholenga kuhimiza uwajibikaji.


Naibu Katibu, Idara ya Ukaguzi na Uzingatiaji wa Masuala ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma wa Tume ya Utumishi wa Umma Bi. Celina Maongezi (aliyesimama) akitoa neno la shukrani mara baada ya   Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuhitimisha kikao kazi chake na Menejimenti ya Tume hiyo kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Tume ya Utumishi wa Umma mara baada ya kuhitimisha kikao kazi chake na Menejimenti ya Tume hiyo kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji. Kushoto kwake ni Naibu Waziri wake, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kulia kwake ni Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Mathew Kirama.





No comments:

Post a Comment