Tuesday, May 16, 2023

MHE. SIMBACHAWENE AMFARIJI WAZIRI MKUU MSTAAFU, MHE. JOHN MALECELA KUFUATIA KIFO CHA MTOTO WAKE, BW. WILLIAM MALECELA

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene, akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Malecela, Mtaa wa Kilimani jijini Dodoma kufuatia kifo cha mtoto wa Mhe. Malecela, Bw. William Malecelea kilichotokea tarehe 14 Mei, 2013. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mwenye suti ya kijivu) akiwa kwenye msiba wa mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Malecela. Kushoto kwake ni Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai. Wengine ni viongozi wa ofisi yake pamoja na waombolezaji.  



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mwenye suti ya kijivu) akimsikiliza Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Malecela (Wa kwanza kulia) alipoenda kumfariji nyumbani kwake Kilimani jijini Dodoma kufuatia kifo cha mtoto wake, Bw. William Malecela. Katikati ni Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai. 



No comments:

Post a Comment