Na. Veronica Mwafisi- Dodoma.
Tarehe 16 Februari, 2026
“Mfumo wa e-Mrejesho unalenga kuboresha huduma zinazotolewa na Serikali na ni sehemu ya utekelezaji wa dhana ya Utawala Bora ambayo inajali maslahi ya wengi, kuwa na uwazi, kupiga vita dhidi ya rushwa, kuleta haki na usawa na kuhimiza uwajibikaji”.
Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Uzingatiaji wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Janet Mishinga alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo jijini Dodoma.
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia Idara ya Usimamizi Maadili imewahimiza Watumishi wa Umma na Wananchi kutumia Mfumo wa Kielektroni wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi Serikalini (e-Mrejesho) ili kuongeza ufanisi katika kushughulikia mrejesho wa masuala mbalimbali ya kiutumishi na kuboresha huduma kwa umma.
Aidha Bi. Mishinga alifafanua
kuwa, ufuatiliaji wa utekelezaji wa mfumo wa e-Mrejesho una lengo la kubaini
mafanikio na changamoto ili kuimarisha uadilifu katika kushughulikia mrejesho
wa wananchi ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya utendaji wa taasisi katika
kuhudumia wananchi.
Pia, alibainisha kuwa utaratibu
wa kushughulikia mrejesho kuhusu mfumo huo unaongeza ushirikishwaji
kwa watumishi wa umma na wananchi.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto) akifuatilia
wasilisho la mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hutolewa kila siku ya Jumatatu kwenye ofisi
hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa
Ufuatiliaji na Uzingatiaji wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Janet
Mishinga akifafanua jambo alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji
Watumishi wa ofisi hiyo jijini Dodoma.
Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI
wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya
kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi
hiyo jijini Dodoma.
Wakurugenzi
Wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu
Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi
wa ofisi hiyo ambayo
hufanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Wengine ni Watumishi wa ofisi hiyo.
Sehemu ya Watumishi
wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu
Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi
wa ofisi hiyo ambayo
hufanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi
wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu
Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi
wa ofisi hiyo ambayo
hufanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.




No comments:
Post a Comment