Na. Antonia Mbwambo-Morogoro
Tarehe: 9 Februari, 2026
“Ninatoa
rai kwa kwa Waajiri wote,
Mamlaka za ajira
na Mamlaka za nidhamu
kuwasilisha vielelezo vya rufaa na malalamiko Tume ya Utumishi wa Umma kwa
wakati kama Sheria inavyoelekeza
vingenevyo Serikali haitasita kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yao”.
Rai hiyo imetolelewa leo tarehe 9 Februari, 2026 na Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.
Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha Tume ya Utumishi
wa Umma na Mamlaka za Maji nchini kuhusu utekelezaji wa sheria ya utumishi wa
umma Sura 298 na matumizi ya mfumo
wa kielektroni wa kushughulikia rufaa na malalamiko na uwasilishaji wa taarifa
za kiutumishi Tume.
Mhe. Kikwete alisema kuwa Waajiri, Mamlaka za Ajira na Mamlaka za Nidhamu katika Utumishi wa Umma zinaweza kuwasilisha vielelezo vya rufaa na malalamiko ya watumishi wao Tume kupitia Mfumo wa Kielektroni wa Kushughulikia Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma na Uwasilishaji wa Taarifa za Kiutumishi (PSCMIS).
“Ninafahamu
kuwa wapo Waajiri, Mamlaka za Ajira na Mamlaka za Nidhamu ambazo hazitekelezi wajibu wao ipasavyo hasa Tume inapowaelekeza kuwasilisha vielelezo vya
rufaa na malalamiko, jambo hili limekuwa
likisababisha watumishi wa Umma
kukaa muda mrefu bila kupata haki zao na
Serikali Kupata hasara” alisema Mhe. Kikwete.
Aliongeza kuwa, muda wa kuwasilisha
vielelezo hivyo unapopita, Tume hulazimika kuamua rufaa hizo kwa kutumia
vielelezo vya upande mmoja kwa kuzingatia
sheria, jambo hili siyo sawa
kwa kuwa Mamlaka haziwatendei haki Warufani na Walalamikaji
pamoja na Serikali iliyowaamini na kuwapa dhamana ya kusimamia Utumishi wa
Umma.
Kwa
kuzingatia utawala bora unaoshamilishwa na uwepo wa mifumo ya TEHAMA, Warufani wataweza kufuatilia, kufahamu hali ya rufaa na malalamiko yao
yamefikia hatua gani kwa urahisi.
Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala tumepewa dhamana ya kuhakikisha dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kujenga Utumishi wa Umma
wenye uadilifu na unaowajibika kwa wananchi kwa kutoa huduma bora inatimia kupitia Tume ya Utumishi wa Umma" Mhe.
Kikwete alisisitiza.
Vile
vile, aliwashukuru Wanahabari kwa kuhabarisha umma kuhusu jitihada zinazofanywa
na Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuijenga Tanzania hasa katika kuboresha haki za Watumishi
wa Umma na kuimarisha Utawala Bora.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete,
akizungumza na Maafisa Utawala na Maafisa Sheria (hawapo pichani) wakati
akifungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za
Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo
wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala
ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa NSSF Mkoani Morogoro leo tarehe 9
February, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini
kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi za NSSF Mkoani Morogoro katika
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Mhe. Ridhiwani Kikwete WTM5
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete
(kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe. Hamisa
Kalombola, wakati wa kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji
wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa
kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo
tarehe 9 Februari, 2026
Viongozi wa Tume ya Utumishi wa Umma wakimsubiri Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete kuwasili katika katika kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari, 2026
Washiriki wa kikao kazi cha mafunzo
ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa
Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa
kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi
wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo
alipokuwa akizungumza nao leo Mkoani Morogoro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete
(aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Tume ya
Utumishi wa Umma baada ya Waziri huyo kufungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume
ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya
Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa
na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari,
2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete
(aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya Tume ya
Utumishi wa Umma baada ya Waziri huyo kufungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume
ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya
Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa
na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari,
2026

No comments:
Post a Comment