Na Veronica Mwafisi-Chato
Tarehe 17 Machi, 2026
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete amesema Serikali itaendelea kuwahudumia na kuwaenzi Viongozi
wa Kitaifa Wastaafu kwa kiwango stahiki kwa mujibu wa sheria na kwa kuzingatia
maelekezo ya mara kwa mara yatakayotolewa na Mamlaka.
Mhe.
Kikwete ametoa kauli hiyo leo tarehe 17 Machi 2026 kwenye kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita.
Amesema,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ndiyo yenye
dhamana na Matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa Mujibu wa Hati Idhini
ambayo Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aligawa majukumu kwa Mawaziri na
suala hili la kumbukizi ni mojawapo ya utekelezaji wa Sheria ya Mafao ya
Hitimisho la Kazi kwa Viongozi wa Kisiasa Sura 225 jambo ambalo hata Hayati
Dkt. John Joseph Magufuli, aliwahi kulitolea maelekezo.
“Kwa msingi
huo, tunatoa uhakika wa uendelevu wa huduma bora kwa Viongozi wa Kitaifa
Wastaafu na Wajane wa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu,” amesisitiza Mhe. Kikwete.
Aidha,
ameongeza kuwa Rais wa Awamu ya Tano alielekeza kuwa suala la kumbukizi
linatakiwa kufanyika kwa umakini na ubora wa hali ya juu ili kuwafanya viongozi
waliostaafu na wanaojiandaa kustaafu kuwa na ari ya kufanya kazi kubwa ya
kulijenga Taifa wakiwa kazini kutokana na kupata uhakika wa uendelevu wa
mustabali wa maisha yao na kuweka misingi bora ya kukabidhi kijiti cha uongozi
wa nchi yetu.
Mhe. Kikwete
amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan kwa kutoa ruhusa na maelekezo mbalimbali kuhusu kufanyika kwa kumbukizi
hiyo.
“Nikiwa ndiye
Waziri mwenye dhamana na matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu naomba nikushukuru
wewe binafsi kwa kutoa fedha za kufanikisha shughuli hii sambamba na
kutusimamia katika kufanikisha jambo hili muhimu kwa Ofisi yetu, Serikali kwa
ujumla na Familia ya Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo hapa inaongozwa Mama Janeth, Mjane wa
Hayati Dkt. John P. J. Magufuli,” ameongeza.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa kumbukizi ya
miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato
mkoani Geita ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (hayupo pichani)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa
kwanza kushoto) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka
Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani
Geita.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya
Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt.
John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Askofu wa Jimbo Katoliki Rulenge – Ngara,
Mhashamu Severine Niwemugizi akiongoza Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya
Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato,
mkoani Geita.
Sehemu ya Mawaziri na Viongozi wengine wa
Serikali wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya
Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt.
John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia)
akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha
Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe
Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu Bw. Musa Magufuli (Aliyeva suti ya blue) akifuatilia jambo
wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais
wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe
Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha
Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John
Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Sehemu ya ndugu, jamaa na marafiki wa familia ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais huyo iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.




















