Monday, April 6, 2026
Saturday, April 4, 2026
Thursday, April 2, 2026
Tuesday, March 31, 2026
MAAFISA RASILIMALIWATU WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWENYE SUALA LA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA
Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe 01 Aprili, 2026.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi ametoa
wito kwa Maafisa Rasilimaliwatu kufanya tathmini kwenye suala la uhamisho kwa watumishi
wa umma ili kuondoa vikwazo na kuongeza tija ya utendajikazi katika Utumishi wa
Umma.
Bw.
Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa
e-Watumishi kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma yaliyokuwa yakifanyika kwa siku tisa kuanzia tarehe 23 Machi
hadi 01 Aprili, 2026 jijini Dodoma.
Bw.
Mkomi amesema, uhamisho ni haki ya mtumishi na mwajiri kutaka kumtumia mtumishi
fulani katika eneo fulani au ni haki ya mwajiri kuendelea kumtumia mtumishi
husika sehemu anayotumikia vizuri.
Hivyo,
Bw. Mkomi amewataka Maafisa Rasilimaliwatu hao kufanya tathmini katika maeneo
yao ya kazi hasa katika Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika
Utumishi wa Umma (e-Msawazo)
“Nitoe
msisitizo kuhusu tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu, naamini ninyi ndio
wasimamizi wakubwa katika maeneo mengi na ndio mnaoleta taarifa ya masuala husika
ya kiutumishi, utaratibu wa uhamisho una vigezo na vinajulikana hivyo ni vema kupata
usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi hao pasipo kuwa na
vikwazo au mifarakano isiyokuwa na tija kwa sababu ya uhamisho,” amesisitiza
Bw. Mkomi.
Aidha,
Bw. Mkomi ameongeza kuwa, Maafisa Rasilimaliwatu wana jukumu la kumshauri
vizuri mwajiri linapotokea suala la uhamisho kwa mtumishi ni vema kutoa vigezo
sahihi baada ya kufanya tathmini ya kutosha.
“Tunatamani
umwambie mwajiri uhamishio wa mtumishi huyu tusiutekeleze kwa sababu tathmini tuliyoifanya
ya rasilimaliwatu katika eneo letu tuna upungufu wa afisa husika au uhamisho
huu tuutekeleze kwa sababu tuna maafisa wa kutosha kadhaa kwenye eneo letu,”
amesema Bw, Mkomi
Vilevile,
Bw. Mkomi amesema eneo la uhamisho limeonekana kuwa na changamoto kutokana na
watumishi wanaoomba uhamisho kuzuiliwa bila kuwa na sababu za kutosha.
Bw.
Mkomi amewataka Maafisa hao kufanyia kazi mafunzo yote waliyoyapata
watakaporudi kwenye maeneo yao ya kazi ili yakaongeze tija katika Utumishi wa Umma
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu
Serikalini, Bw. Hamis Mkunga amesema jumla ya washiriki 275 wamepatiwa mafunzo
hayo hivyo amewataka washiriki hao kwenda kufanyia kazi ili kuleta matokeo chanya
katika maeneo yao ya kazi kwa maendeleo ya ofisi au taasisi husika na taifa kwa
ujumla.
Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti
wa Mafunzo hayo, Bi. Isabela Chilumba amemuahidi Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi kuwa kwa niaba ya washiriki wote watazingatia
maelekezo ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa
Taifa.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya
Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kushoto)
kabla ya kufunga Mafunzo ya Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma kuhusu Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia
tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu
na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga
mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu
na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga
mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.
Mkurugenzi wa Idara ya
Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Bw. Hamis Mkunga (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya
Usimamizi na Payrol Jeanfrida
Mushumbusi (kulia) wakifuatilia
hotuba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili,
2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mkufunzi wa
Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara
ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kulia), kabla ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kufunga
mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa
e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe
1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiteta jambo na Afisa Rasilimaliwatu kutoka
Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Bi. Zuhura Kizuguto baada ya Katibu huyo
kufunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyotolewa Jijini Dodoma kuanzia
tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala
kutoka Taasisi mbalimbali za Umma .
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa
e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe
1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.
Monday, March 30, 2026
WATUMISHI WA UMMA WAHIMIZWA KUONGEZA UWAJIBIKAJI KATIKA KUTOA HUDUMA BORA
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 30 Machi, 2026.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewahimiza Watumishi wa Umma kuongeza uwajibikaji
katika kuwahudumia wananchi.
Bw. Daudi ametoa wito huo leo alipokuwa akiwapongeza Watumishi wa Ofisi
hiyo waliozaliwa mwezi Machi, 2026 mara baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila siku ya Jumatatu Mtumba Jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha
utendaji kazi watumishi wa ofisi hiyo.
Bw. Daudi amesema, mtumishi wa umma anapoongeza umri imsaidie kuongeza chachu ya utendajikazi ili kutimiza malengo ya Serikali ya kutoa huduma bora kwa wananchi.
''Nitoe wito kwa Watumishi wa Umma mnapoongeza umri na kusherehekea siku yenu ya kuzaliwa, hakikisheni mnawajibika ipasavyo katika maeneo yenu ya kazi hasa mnapotoa huduma kwa Watumishi wa Umma wenzenu na Wananchi, hakikisheni kuwa mnatimiza malengo ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa kila Mtanzania.” amesema Bw. Daudi.
Awali katika mafunzo hayo, Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka katika ofisi
hiyo, Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bi. Magreth Banogile akiwasilisha
mada kuhusu Motisha katika Utumishi wa Umma alisema,
motisha ni manufaa anayoyapata mtumishi baada ya mshahara kutokana na majukumu
anayoyatekeleza hivyo ni wajibu wa kila mtumishi wa umma kutekeleza majukumu
yake kwa ufanisi ili aweze kupata stahiki ya motisha husika.
Ameongeza kuwa baadhi ya motisha
katika Utumishi wa Umma ni pamoja na mazingira bora ya kazi, vitendea kazi,
fursa za mafunzo, huduma ya usafiri wa kwenda na kurudi kutoka kazini, pamoja
na fursa ya muda wa kufanya mazoezi.
Aidha, katika mafunzo hayo
kulikuwa na mada mbalimbali zilizowasilishwa na Maafisa kutoka katika Idara hiyo ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu ambapo
Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi Bw. Baraka Kilagu aliwasilisha mada kuhusu
Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara pamoja na Afisa Rasilimaliwatu
Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi aliyewasilisha mada kuhusu Miundo ya Mishahara
katika Utumishi wa Umma.
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier
Daudi (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa ofisi
hiyo waliokuwa wakiadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi,
2026. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akifurahia jambo alipokuwa
akizungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa
mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yanayofanyika
kila Jumatatu kwenye Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI
wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya
Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya
kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi
hiyo jijini Dodoma.
Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bw. Baraka Kilagu (aliyesimama) akiwasilisha
mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya kuwajengea
uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini
Dodoma. Waliokaa wa kwanza kulia ni Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka ofisi hiyo Bi.
Magreth Banogile na katikati ni Afisa
Rasilimaliwatu Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho
la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa
kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo
hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho
la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa
kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo
hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI
wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa mafunzo ya
kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi
hiyo jijini Dodoma.
Mkurugenzi
wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw.
Musa Magufuli (aliyesimama) akizungumza jambo kabla ya
kumkaribisha Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Bw. Xavier Daudi kuzungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya
kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho
la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa
kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo
hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mhasibu
Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo akikata keki kwa niaba ya
Watumishi wa ofisi hiyo wanaoadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi, 2026.
Mhasibu
Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo (kulia) akimlisha keki Mkurugenzi
wa Idara ya Usimamizi wa Maadili, Bi. Felister Shuli (kushoto) kwa niaba ya
Watumishi wote waliozaliwa Mwezi Machi, 2026.
Friday, March 27, 2026
KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WADAU WA RASILIMALIWATU KATIKA SEKTA YA UMMA KUPENDEKEZA MKAKATI MADHUBUTI WA SULUHISHO LA UPUNGUFU WA WATUMISHI
Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 27 Machi, 2026.
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi amewataka wadau wa Rasilimaliwatu Serikalini kupendekeza mkakati
madhubuti utakaosaidia kuepukana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika
taasisi za umma.
Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa
akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi za Kimkakati
kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu.
Amesema Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
ilifanya zoezi la Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika taasisi za umma
na kubaini kuwepo kwa upungufu wa watumishi kwenye baadhi ya taasisi na taasisi
nyingine kuwepo kwa ziada ya watumishi.
Amesema kufuatia tathmni hiyo, Ofisi iliona ni vema ikaandaa kikao cha
wadau hao ili kujadiliana kwa pamoja namna itakavyofaa kutafuta ufumbuzi wa changamoto
hiyo ya muda mrefu.
Amesema kila mwaka wakati wa bajeti taasisi za umma zimekuwa na
utaratibu wa kuomba watumishi, hivyo mkakati madhubuti uwekwe ili kupata
suluhisho la changamoto hiyo ya upungufu wa watumishi.
“Lengo
kubwa la kikao kazi hiki ni kupata
usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi katika taasisi za umma, kuna maeneo yanahitaji watumishi kimkakati
hivyo ni muhimu kuona namna ya kukubaliana katika kuwapata watumishi hao na
kujadiliana kwa kina ili kupata mapendekezo yatakayosaidia kuwagawa Watumishi
wa ajira mpya na watakaokuwa wakihamia katika vituo vingine vya kazi,” amesisitiza.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara
ya Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda amesema kupitia kikao kazi hicho
Serikali itapata taarifa zilizo sahihi za mahitaji ya Watumishi wa Umma kwa miaka mitano ijayo.
Akitoa
neno la shukrani Mwenyekiti wa Kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala
na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Afya, Bw. Issa Ng’imba alimuahidi Katibu
Mkuu Mkomi kuwa watazingatia maelekezo yote ambayo ameyatoa ili waweze
kuboresha utendaji kazi kwa maendeleo ya Taifa
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kabla ya Katibu huyo kufungua kikao hicho kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma
Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka
Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo mara baada ya Katibu huyo kufungua kikao
kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Sekretarieti kutoka
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi
cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga
kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na
Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika
ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Afisa kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Waziri Mkumbo akiwasilisha mada ya Mfumo wa e-Msawazo na
matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za
Kimkakati wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya
Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati
kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT
Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara na
Taasisi za kimkakati baada ya Katibu huyo kufungua kikao kazi cha kujadili
matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi hizo
kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 kilichofanyika
kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Washiriki wa kikao kazi cha
Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada
mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi
wa NAOT Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya
Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati
kilichofanyika katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Washiriki wa kikao kazi cha
Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada
mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi
wa NAOT Jijini Dodoma.
Washiriki wa kikao kazi cha
Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada
mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi
wa NAOT Jijini Dodoma.
Wednesday, March 25, 2026
Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe 26 Machi, 2026.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amezielekeza Taasisi za Serikali kuanzisha Msimbo Mraba (QR CODE) utakaowezesha kutoa mrejesho wa huduma zinazotolewa na Taasisi hizo kwa wananchi.
Bw.
Mkomi ametoa maelekezo hayo leo alipokuwa akifungua kikao kazi cha wakuu wa
Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa
Mfumo wa Kielekroni (e-Mrejesho) Toleo la Pili kilichofanyika katika Ukumbi wa
Mikutano wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.
Bw.
Mkomi amesema ushughulikiaji wa huduma za mrejesho zinazotolewa na Serikali ni
utaratibu uliowekwa mahususi kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji na usikivu
ndani ya Taasisi za Umma pamoja na kukuza misingi ya Utawala Bora.
Katibu
Mkuu Mkomi amewataka wasimamizi wa Rasilimaliwatu katika Taasisi hizo kuwa na
uelewa wa pamoja katika kutoa huduma na kuona namna ya kupata mrejesho kwa
jinsi inavyowaridhisha wahusika katika Utumishi wa Umma.
Vilevile,
Bw. Mkomi amewataka washiriki wa kikao kazi hicho kufuatilia kwa karibu
utekelezaji wa Mfumo wa e-Mrejesho katika taasisi zao ili waweze kutoa elimu
hiyo kwa watumishi wengine waliopo katika taasisi zao kwa lengo la kuimarisha
utendaji kazi.
Kadhalika,
Bw. Mkomi ameongeza kuwa ili kuboresha utekelezaji huo wa Mfumo wa e-Mrejesho
amewataka Maafisa Tehama kutengeneza QR CODE kwenye taasisi zote ili
kuwezesha wananchi kuutumia na kupeleka
malalamiko yao au mrejesho
kwenye taasisi husika
“Katika
wananchi 100 hautakosa wananchi 60 wenye simu za kupangusa hivyo, huduma hiyo ya
QR CODE kwa asilimia 60
itaenda mbali zaidi kwa muda mfupi,’’ amesema Bw. Mkomi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili,
Bi. Felista Shuli amesema lengo la kikao kazi hicho ni washiriki kuwezeshwa,
kupitishwa na kujadili kwa pamoja kuhusu usimamizi na utekelezaji
wa mfumo wa mrejesho ambao ni mojawapo ya mifumo iliyowekwa na Serikali kwa
lengo la kusimamia uwajibikaji katika Utumishi wa Umma.
Akitoa neno la shukrani
kwa mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mwenyekiti wa
Kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Michael John
amemuahidi Katibu Mkuu Mkomi kuwa watazingatia maelekezo yote ambayo ameyatoa
ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa Taifa.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kabla ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma
Mkurugenzi
wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Bi. Felista Shuli (kushoto) akifuatilia majadiliano ya Mada
mbalimbali za kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni
(e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu
na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa kikao hicho, Bw. Michael John.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili wa Ofisi hiyo Bi. Felister
Shuli (kulia) baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni
(e-Mrejesho) kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu
na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Bi. Janeth Mishinga akiwasilisha mada kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni
(e-Mrejesho) toleo la pili katika kikao cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa
Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiwa
katika picha ya pamoja na Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala
na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu kujadili matumizi
na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) kilichofanyika katika
Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi
kutoka Ofisi hiyo baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika machi 26, 2026 katika Ukumbi wa
Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili wa
ofisi hiyo Bi.Felista Shuli (kushoto). Kulia ni Mkurugenzi wa
Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki Bw. Michael John ambaye ni Mwenyekiti wa kikao kazi cha Wakuu
wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 26,
2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Sekretarieti
ya Ofisi hiyo baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika machi 26, 2026 katika Ukumbi wa
Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma


























