Tuesday, March 17, 2026

WAZIRI KIKWETE ASEMA SERIKALI ITAENDELEA KUWAHUDUMIA NA KUWAENZI VIONGOZI WA KITAIFA WASTAAFU KWA MCHANGO WAO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA TAIFA

 Na Veronica Mwafisi-Chato

Tarehe 17 Machi, 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Serikali itaendelea kuwahudumia na kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa kiwango stahiki kwa mujibu wa sheria na kwa kuzingatia maelekezo ya mara kwa mara yatakayotolewa na Mamlaka.

Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo tarehe 17 Machi 2026 kwenye kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita.

Amesema, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ndiyo yenye dhamana na Matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa Mujibu wa Hati Idhini ambayo Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aligawa majukumu kwa Mawaziri na suala hili la kumbukizi ni mojawapo ya utekelezaji wa Sheria ya Mafao ya Hitimisho la Kazi kwa Viongozi wa Kisiasa Sura 225 jambo ambalo hata Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, aliwahi kulitolea maelekezo.

“Kwa msingi huo, tunatoa uhakika wa uendelevu wa huduma bora kwa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu na Wajane wa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu,” amesisitiza Mhe. Kikwete.

Aidha, ameongeza kuwa Rais wa Awamu ya Tano alielekeza kuwa suala la kumbukizi linatakiwa kufanyika kwa umakini na ubora wa hali ya juu ili kuwafanya viongozi waliostaafu na wanaojiandaa kustaafu kuwa na ari ya kufanya kazi kubwa ya kulijenga Taifa wakiwa kazini kutokana na kupata uhakika wa uendelevu wa mustabali wa maisha yao na kuweka misingi bora ya kukabidhi kijiti cha uongozi wa nchi yetu.

Mhe. Kikwete amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ruhusa na maelekezo mbalimbali kuhusu kufanyika kwa kumbukizi hiyo.

“Nikiwa ndiye Waziri mwenye dhamana na matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu naomba nikushukuru wewe binafsi kwa kutoa fedha za kufanikisha shughuli hii sambamba na kutusimamia katika kufanikisha jambo hili muhimu kwa Ofisi yetu, Serikali kwa ujumla na Familia ya Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo hapa inaongozwa Mama Janeth, Mjane wa Hayati Dkt. John P. J. Magufuli,” ameongeza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (hayupo pichani)


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kushoto) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Wananchi mbalimbali wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Askofu wa Jimbo Katoliki Rulenge – Ngara, Mhashamu Severine Niwemugizi akiongoza Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Mawaziri na Viongozi wengine wa Serikali wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita. 


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Bw. Musa Magufuli (Aliyeva suti ya blue) akifuatilia jambo wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya ndugu, jamaa na marafiki wa familia ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais huyo iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.






Monday, March 16, 2026

SERIKALI KUPITIA TASAF YAIKOSHA KAMATI YA BUNGE KWA KUTEKELEZA MRADI WA ZAHANATI KATIKA ENEO LENYE CHANGAMOTO YA MIUNDOMBINU

Na Veronica Mwafisi-Mwanza

Tarehe 16 Machi, 2026

Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kutekeleza Mradi wa Zahanati katika eneo lenye changamoto ya miundombinu na kuokoa maisha ya wakazi wa eneo hilo.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 16 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt.  Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 

Akizungumza kwa niaba ya kamati yake, Mhe. Dkt.  Ndumbaro amesema ujenzi wa zahanati hiyo ni msaada mkubwa kwa wakazi wa Mihama na Kata ya Kitangiri ambao ilikuwa ni changamoto kutoka katika eneo hilo kutafuta huduma sehemu nyingine.

 “Kwa changamoto ya kufika huku, niwapongeze TASAF kwa kutekeleza mradi huu katika eneo hili kwani itaokoa maisha ya wananchi wa eneo hili na gharama walizokuwa wakitumia kufuata huduma za matibabu katika eneo lingine.” Ameongeza.

Mhe. Ndumbaro ameongeza kuwa maendeleo haya ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambacho kimekusudia kuwajali wananchi wake kwa kuwapa huduma mbalimbali ikiwemo za kijamii.

Aidha, ametoa wito kwa uongozi wa Halmashauri hiyo ya Ilemela kuhakikisha zahanati hiyo inawekwa chini ya Halmashauri hiyo. “TASAF imetekeleza, zahanati hii ni ya kwenu sasa, mfanye utaratibu iwe chini ya Halmashauri,” amesisitiza Mhe. Dkt. Ndumbaro.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema zahanati ya Mihama ni sehemu ya vielelezo vya miradi inayotekelezwa na TASAF kwa lengo la kuwahudumia wananchi.

Mhe. Kikwete amewataka wananchi wa Mihama na Kitangiri kuitunza zahanati hiyo ili iweze kuwahudumia kama ilivyokusudiwa.

Ameongeza kuwa, katika kuhakikisha wananchi wanahudumiwa kikamilifu, katika ajira 12,000 zilizotolewa na Serikali ndani ya siku 100, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemelea imepewa watumishi wa afya 37 na elimu 40.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray ameishukuru Kamati kwa kuitembelea zahanati hiyo na kushuhudia maendeleo yaliyofanywa na Serikali katika eneo hilo.

Akitoa neno la shukurani kwa niaba ya wananchi wa eneo la Mihama, Bi. Mary Nyanda ameishukuru Serikali kwa kujenga zahanati katika eneo hilo kwani walikuwa na uhitaji mkubwa wa zahanati.

“Zahanati hii ni mkombozi kwetu watu wa Mihama, kwa miaka 25 tumekuwa tukihangaika kufuata huduma sehemu nyingine, tunaishukuru sana Serikali kwa kutekeleza hili,” ameongeza Bi. Nyanda.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, imehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Geita na jijini Mwanza.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa Zahanati ya Mihama na Wananchi wa Mihama wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt, Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.



Sehemu ya Wauguzi na Maafisa Tabibu wa Zahanati ya Mihama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakikagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wengine ni Viongozi wa Mkoa wa Mwanza, Watendaji wa TASAF na Mganga Mfawidhi wa Zahanati hiyo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (kushoto) wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Sehemu ya Wananchi wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Zahanati ya Mihama wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Edwin Swalle


Mwonekano wa jengo la Zahanati ya Mihami lililojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) lililopo katika Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza ambapo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ilitembelea kukagua mradi wa utekelezaji wa Zahanati hiyo.


Mkurugenzi wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kufanya ziara ya kikazi kutembelea mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Mihama kwa lengo la kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akijadili jambo na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro


Bi. Mary Nyanda akitoa shukrani kwa niaba ya Wananchi kwa Serikali kupitia TASAF kwa kujenga zahanati ya Mihama iliyopo katika Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Wanakikundi cha Wasikivu-TASAF wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Mwonekano wa vifaa vya Zahanati ya Mihama iliyopo katika Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Sehemu ya Watendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) pamoja na Maafisa wa Ulinzi na Usalama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.






WITO WATOLEWA WATUMISHI WA UMMA KUENDELEA KUJENGEWA UWEZO KIUTENDAJI ILI KUTOA HUDUMA BORA KWA UMMA

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 16 Machi, 2026

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi ameielekeza Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu ya Ofisi hiyo kuendeleza programu ya mafunzo kwa Watumishi wa Umma kila Jumatatu ya wiki kupitia wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Ofisi hiyo ili kuwajengea uwezo watumishi katika utekelezaji wa majukumu yao utakaosababisha Ufanisi katika utoaji wa huduma na kuleta tija kwa jamii.

Bw. Daudi ameyasema hayo Machi 16, 2026 wakati akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora alipokuwa akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao jijini Dodoma.

“Nipende kuwapongeza watumishi wenzetu walioendesha mada mbalimbali katika programu hii ya mafunzo kwa weledi, ujasiri, na umahiri mkubwa ili kuhakikisha uelewa unajengeka kwa watumishi wa umma na kuimarisha utendaji kazi kwa maslahi ya Taifa”. Bw. Daudi alisema

Aidha, amewasisitiza watumishi wa Ofisi yake kuutumia utaalamu walionao na uwezo wanaojengewa mara kwa mara kutekeleza majukumu yao kwa juhudi na ufanisi ili kutoa huduma bora na kwa wakati kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahimu Mahumi amesema Ofisi ya Rais-UTUMISHI imeanzisha utaratibu wa kushirikishana uzoefu wa kitaalamu kwa watumishi wengine kwa kila Idara kupitia programu ya mafunzo ya kila wiki ili kujenga uelewa mpana utakaosababisha umahiri katika utendaji kazi.

Akiwasilisha mada inayohusiana na masuala ya Uhamisho katika Utumishi wa Umma, Afisa Utumishi Mwandamizi, kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Said Ally amesema lengo la kushirikishana uzoefu kwa wataalamu wa ndani ni kuhakikisha kila mtumishi ndani ya Ofisi hiyo anakuwa na uelewa utakaomuwezesha kuyajua majukumu ya kila Idara ili kutoa huduma kwa wananchi kwa uharaka na ubora zaidi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Sera za TEHAMA na Viwango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Ibrahim Toure, akiwasilisha mada ya Usalama Mtandaoni, amesema lengo la mada hiyo ni kukumbushana juu ya matumizi sahihi ya mifumo ili kuwa na mtazamo na utamaduni wa usalama mtandaoni wanapokuwa katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku na hata wawapo nje ya Ofisi.

Vilevile Afisa TEHAMA Mkuu, Idara ya TEHAMA Serikalini, Bi. Zalika Hussein amesema elimu ya usalama mtandaoni itawawezesha watumishi kuhakikisha mifumo na miundombinu ya TEHAMA na taarifa zinazohifadhiwa kwenye mifumo hiyo zinakuwa salama bila kufikiwa na watu wasiohusika kwa kuhakikisha wanatumia nywila zao wenyewe bila kumshirikisha mtu mwingine yeyote kwa lengo la kulinda taarifa za serikali ikiwa ni utaratibu wa kuhakikisha usalama, usiri, na uadilifu wa data za umma dhidi ya ufikiaji usioidhinishwa.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo wakati akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao leo tarehe 16 Machi, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, SACP. Ibrahimu Mahumi akiwaelimisha watumishi wa Ofisi hiyo kuhusu umuhimu wa kushirikishana uzoefu wa kitaaluma katika kuleta ufanisi wa kazi wakati wa mafunzo ya kuwajengea watumishi hao uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma 

Sehemu ya Watumishi wa umma kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Sera za Tehama na Viwango, Ofisi ya Rais- ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Itawala Bora, Bw. Ibrahim Toure, akiwasilisha mada ya Usalama Mtandaoni wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo machi 16, 2026 jijini Dodoma.

Bi. Zalika Hussein  Afisa Tehama Mkuu wa Idara ya Tehama Serikalini akiwasilisha mada ya Usalama Mtandaoni wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo machi 16, 2026 jijini Dodoma. 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto) pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa Ofisi hiyo wakifuatilia mafunzo maalumu ambayo hufanyika kila wiki kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma

Sehemu ya Watumishi wa umma kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa umma kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa umma kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa umma kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao jijini Dodoma.
Afisa Utumishi Mwandamizi, kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Said Ally akiwasilisha mada inayohusiana na masuala ya Uhamisho katika Utumishi wa Umma,wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo machi 16, 2026 jijini Dodoma. 

Sehemu ya Watumishi wa umma kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati akihitimisha programu ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao jijini Dodoma.

 

Sunday, March 15, 2026

KAMATI YA BUNGE YAELEKEZA NYARAKA KUTUNZWA KIDIJITI KUWEZESHA KIZAZI CHA SASA KULINDA AMANI YA NCH

 Na Veronica Mwafisi-Mwanza

Tarehe 15 Machi, 2026

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeelekeza nyaraka kuhifadhiwa katika mfumo wa kidijiti ili kuwezesha kizazi cha sasa kujua historia ya nchi na kulinda amani kwa maendeleo ya taifa.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 15 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt.  Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 

Akitoa maelekezo hayo kwa niaba ya kamati yake, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema kizazi cha sasa kutokujua historia ya nchi yao kumesababisha kutoona umuhimu wa kuitunza amani ya nchi.

“Kuna umuhimu sasa yale mambo ya kihistoria ambayo siyo nyeti tuyachambue ili yawafikie vijana, tujivunie utaifa wetu, tusisubiri watoto wetu wafunzwe na ulimwengu, tuwawekee nyaraka zitakazosaidia kujua historia ya nchi yao kwenye mfumo wa kidijiti.” Mhe. Dkt. Ndumbaro amesisitiza. 

Aidha, kamati hiyo imempongeza Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Bw. Firimin Msiangi pamoja na wasaidizi wake kwa kazi nzuri wanayoifanya ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka kwa ajili ya vizazi vijavyo.

“Kazi nzuri sana imefanyika, tumeona, changamoto ya bajeti mliyonayo tunamuelekeza Waziri ifanyiwe kazi kwa kutoa kipaumbele kwenye kuziweka nyaraka katika mfumo wa kidijiti na masilahi ya watumishi wa Idara hii nyeti,” ameongeza Mhe. Dkt. Ndumbaro.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ametoa wito kwa wajumbe wa kamati hiyo kuitumia Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kujifunza historia ya nchi na kuona nyaraka ambazo zitawasaidia katika shughuli zao hasa kwa wanaohitaji kuandika vitabu.

“Kituo hiki kina utajiri wa kumbukumbu na nyaraka, kwa wanaotaka kujifunza historia ya nchi yetu na kuandika vitabu, mtumie kituo hiki, tumeona nchi hii ilivyo na historia ndefu, mtapata taarifa nyingi.” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Vile vile Mhe. Kikwete amewasisitiza wajumbe hao wa kamati kujifunza kuweka kumbukumbu zao na kuwarithisha vizazi vijavyo. “Wenzetu huko nyuma walikuwa wanaandika na ndio maana tumeweza kuona historia nzuri ya nchi yetu, basi sasa nasi tujifunze kufanya hivyo kwa vizazi vyetu vijavyo,” Mhe. Kikwete ameongeza.

Akiwasilisha taarifa ya Mradi wa Kituo hicho, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi alisema  lengo la uanzishwaji wa kituo hicho ni kusogeza huduma ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka za taasisi za serikali kwa Kanda ya Ziwa ili kulinda urithi wa kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza mara baada ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt, Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kamati hiyo katika Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Afisa Kumbukumbu, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka, Bi. Maryam Ayoub (wa kwanza kushoto) alipokuwa akitoa maelezo kuhusu Vita vya Kagera kwa Wajumbe hao wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) kuzungumza na Watumishi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akivalishwa skafu mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka wakati wa ziara ya kikazi na Kamati yake iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa kituo hicho kilichopo Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (wa kwanza kushoto) akifuatilia jambo pamoja na Wajumbe wa Kamati yake walipokuwa wakipatiwa maelezo mbalimbali ndani ya ghala la kuhifadhia nyaraka wakati wa ziara ya kikazi katika Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa kituo hicho kilichopo Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua utekelezaji wa Mradi wa hicho kilichopo Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza


Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi (wa kwanza kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya  kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wengine ni Watendaji wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka.


Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati kamati hiyo ilipokuwa ikikagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 


 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akizungunmza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi (kulia) walipokuwa wakiisubiri Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi (kushoto) walipokuwa wakiisubiri Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.

 


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisalimiana na Watendaji wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa kituo hicho kilichopo Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.