Monday, February 23, 2026

NAIBU KATIBU MKUU - UTUMISHI BW. XAVIER DAUDI AWAASA WATUMISHI WA UMMA KUWA KARIBU NA FAMILIA ZAO KUEPUSHA MSONGO WA MAWAZO NA ATHARI KATIKA UTENDAJI KAZI.

Na Eric Amani Dodoma, Tanzania

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi, amewahimiza Watumishi wa Umma nchini kutumia muda wao ipasavyo wakiwa pamoja na familia zao ili kuepuka msongo wa mawazo unaoweza kuathiri utendaji kazi wao.

Bw. Daudi ametoa wito huo wakati akizungumza na watumishi wa umma katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo leo Februari 23, 2026 jijini Dodoma ili kuimarisha ustawi wa watumishi mahali pa kazi, ambapo alisisitiza kuwa afya ya akili ni nyenzo muhimu katika kuongeza ufanisi na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema kuwa watumishi wengi hawatengi muda wa kutosha wa kupumzika au kuwa karibu na familia zao hali inayoweza kusababisha uchovu wa akili na hatimaye kupunguza ufanisi kazini.

''Ni muhimu kwa watumishi wa umma kuhakikisha wanapata muda wa kuwa na familia zao, kushiriki shughuli za kijamii na kupumzika ili kujenga afya njema ya akili ambayo itawawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi,'' amesema Bw. Daudi.

Kwa upande wake, alieleza kuwa Ofisi ya Rais - UTUMISHI itaendelea kuweka mazingira rafiki ya kazi kwa watumishi ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi huku wakizingatia ustawi wao binafsi.

Aidha, Mwezeshaji ambaye ni Mwanasaikolojia, Mshauri Nasaha, Mtaalamu wa Mahusiano na Mwandishi Dkt. Chris Mauki wakati akitoa mafunzo hayo amesisitiza kuwa uwiano mzuri kati ya maisha ya kazi na familia husaidia kuongeza morali kazini, kupunguza msongo wa mawazo pamoja na kuboresha mahusiano kazini na nyumbani.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti Ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi akizungumza na watumishi wa ofisi hiyo baada ya kukamilika kwa mafunzo ya kuwajengea uwezo ambayo hufanyika kila jumatatu kwenye ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma leo Februari 23, 2026.  


Sehemu ya Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na mwezeshaji Dkt. Chris Mauki (Hayupo kwenye Picha) wakati akitoa mafunzo kuhusu watumishi wa Umma kutumia muda vizuri na familia zao ili kuepusha msongo wa mawazo unaoathari utendaji wa kazi Leo Februari 23, 2026 Dodoma, Tanzania.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Umma SACP Ibrahim Mahumi akitoa neno la Shukrani kwa Menejimenti na Uongozi wa Ofisi hiyo kwa niaba ya watumishi wote wenye kumbukizi ya Siku ya kuzaliwa mwezi Februari Mtumba Jijini Dodoma.


Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakisherekea kumbukizi ya tarehe yao ya kuzaliwa leo Februari 23, 2026 katika Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu Bi Leila Mavika akifuatilia kwa kina mada iliyokuwa ikitolea na Mwezeshaji Dkt. Chris Mauki (Hayupo kwenye Picha) februari 23, 2026 katika Mji wa Serikali Mtumba Dodoma.


Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakimsikiliza mwezeshaji Dkt. Chris Mauki (hayupo Pichani) wakati akitoa mafunzo kuhusu watumishi wa Umma kutumia muda vizuri na familia zao ili Kuepusha msongo wa mawazo unaoathari utendaji wa kazi Februari 23, 2026 Mtumba Jijini Dodoma.



Friday, February 20, 2026

“SERIKALI YADHAMIRIA KUINUA ELIMU NA KUKUZA UCHUMI WA WANATANGA KUPITIA UJENZI WA CHUO CHA UTUMISHI”-Mhe.Kikwete

Na Veronica Mwafisi-Tanga

Tarehe 20.02.2026

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuinua elimu na kukuza uchumi wa wananchi katika Mkoa wa Tanga kupitia mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Kampasi ya Tanga ambao umeanza kutekelezwa katika Kata ya Maweni, Kange tarehe 8 Februari, 2025.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 20 Februari, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma na wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kabla ya kuweka jiwe la msingi.

Waziri Kikwete amesema Kampasi hiyo ikikamilika inategemea kuchukua jumla ya wanafunzi 2,000 lakini watakaonufaika sio wanafunzi hao pekee ambao watapata elimu, bali na wananchi ambao watafanya shughuli mbalimbali za maendeleo na kuweza kuinua kipato chao.

Amemshukuru Mhe. Rais kwa kutambua umuhimu wa elimu katika mkoa huo na kutoa maelekezo ya kujenga kampasi hiyo.

Aidha, Mhe. Kikwete amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Mkoa wa Tanga Kange kwa uzalendo wao mkubwa wa kutoa eneo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo eneo hilo linapojengwa chuo hicho ili watoto wao wapate elimu.

Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha mambo yote yenye athari chanya yanatekelezwa kwa ufanisi wa hali ya juu.

Ameupongeza uongozi na Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma kwa usimamizi mzuri wa ujenzi. Mimi sio mtaalam wa ujenzi lakini kwa macho unaona kazi iliyofanyika ni nzuri na inaridhisha, hongereni sana,” Mhe. Kikwete ameongeza.

Ametoa wito kwa watendaji wa Kampasi hiyo kuweka mazingira mazuri ya eneo hilo kwa kupanda miti ya matunda na kivuli.

Amewasistiza wananchi kushirikiana na viongozi wa Serikali katika kulinda miundombinu ya Kampasi hiyo na ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa huo. 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi amemshukuru Mhe. Kikwete kwa maelekezo yake ya kuboresha utendaji kazi ambayo amekuwa akiyatoa mara kwa mara kwa taasisi zilizo chini ya ofisi anayoisimamia.                                                                                                    

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Mhe.   Dadi Kolimba ameishukuru Serikali kwa uamuzi walioufanya wa kujenga Chuo hicho kwani wangeweza kujenga popote                                                                         

“Mhe. Waziri kazi hii nzuri inayoonekana ni maelekezo yako ambayo umekuwa ukiyatoa mara kwa mara kwa watendaji katika taasisi zilizo chini ya Ofisi yako,” ameongeza,

Mhe. Kolimba ameahidi yeye pamoja na viongozi wengine wa mkoa kusimamia kwa umakini ujenzi wa chuo hicho na kukamilika kwa wakati ili kianze kutumika kama ilivyotarajiwa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi hiyo, Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho amemshukuru Mhe. Kikwete kwa kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi na kuweka jiwe la msingi.

Dkt. Mabonesho amesema kukamilika kwa Kampasi hiyo kutasaidia kuokoa fedha nyingi za pango ambazo wamekuwa wakilipa sasa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) kuzungumza na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Tanga kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia kwake) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi katika Kampasi hiyo.


Sehemu ya Viongozi, Wataalam wa ujenzi, Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo wakati akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akijadili jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho wakati Waziri huyo akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa Ujenzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akizungumza na Wataalam wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga alipokuwa akikagua utekelezaji wa mradi huo. Wengine ni Watendaji wa TPSC


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoka kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa Ujenzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipanda mti mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wanaojenga Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.


Mwonekano wa jengo la mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.



 

 

Thursday, February 19, 2026

TAARIFA HII IPUUZWE


 

“SISI SOTE TUNAFANYA KAZI KWA NIABA YA MHE.RAIS, TUACHE TABIA YA KUHAMISHA WATUMISHI PALE TUNAPOPATA TEUZI”- Mhe. Kikwete

Na Veronica Mwafisi-Arusha

Tarehe 19.02.2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amekea tabia ya baadhi ya Waajiri kuwahamisha watumishi wanaowakuta katika Ofisi walizoteuliwa na kutaka wahamishiwe katika vituo vingine vya kazi.

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 19 Februari, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha wakati akifunga rasmi mkutano wa sita wa Serikali Mtandao ulioanza tarehe 17 Februari, 2026.

Amesema kama ikitokea mtumishi ana tatizo lolote la kiutumishi linalohitaji hatua za kinidhamu, apelekwe kwenye vikao vya kinidhamu ili adhabu stahiki itolewe na sio kuwaonea watu kwasababu ya unyonge wao.

“Nataka niwakumbushe kuwa, kila mmoja aliingia kwa sifa zake, wengine wameingizwa kupitia mitihani ya ajira, wengine kwa nafasi za uteuzi, hivyo kila mmoja akitimiza wajibu wake ni wazi kuwa matokeo mazuri yataonekana.

Aidha, amepiga marufuku watumishi wa umma kutumia barua pepe binafsi kutuma taarifa za ofisi badala ya kutumia barua pepe rasmi za serikali. 

“Ni changamoto kubwa sana, bado tunao watumishi wa umma wanaotumia mitandao binafsi kutuma taarifa rasmi za serikali, tunachokifanya ni jambo la hatari sana, tutumie mifumo yetu iliyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani,” Mhe. Kikwete ameongeza.

Waziri Kikwete amewapongeza e-GA kwa kazi nzuri wanayofanya na kuwasisitiza Waajiri kutumia wataalam hao kutengeneza mifumo katika taasisi zao.

Ametoa wito kwa wataalamu wa TEHAMA kuendelea kujifunza kila wakati ili waweze kukabiliana na changamoto mbambali ikiwemo shambulio la mifumo ya TEHAMA.

Akitoa salamu kwa niaba ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro amemshukuru Waziri Kikwete kwa kuona umuhimu wa kuishirikisha kamati hiyo. “Mmetambua uwepo wa mhimili wa Bunge, mngeweza hata kufanya wenyewe bila hata ya kutushirikisha,” ameongeza Mhe. Dkt. Ndumbaro.

Amesema yeye sio mtaalam wa TEHAMA, lakini bado anatambua umuhimu wa serikali mtandao na kuongeza kuwa, kwa dunia ya leo hatuwezi kusonga mbele bila ya TEHAMA.

Amesema, Tanzania imepata mafanikio makubwa ambayo yanatokana na kazi nzuri ya Serikali kupitia Chama Cha Mapinduzi pamoja, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA).

“Sisi kama kamati na Bunge tunatambua mafanikio hayo. Mafanikio ya kupeleka huduma kwa umma, kunganisha mifumo, kutuhakikishia usalama mtandaoni ni kazi nzuri yenye mafanikio makubwa

Tuko tayari kushirikiana na Wizara kuhakikisha changamoto zinazohusu sera, sharia na bajeti zinafanyiwa kazi. Kila mawasiliano ya Bunge yanakwenda kwa mtandao.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba amemshukuru Waziri Kikwete pamoja na uongozi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa maelekezo na msisitizo kuhusu uzingatiaji wa Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao kwani vimeongeza uzito, mwelekeo na ari mpya kwa washiriki wote. “Tunathamini sana mchango wako na w viongozi wote katika kuendeleza ajenda ya mageuzi ya kidijitali Serikalini,” Mhandisi Ndomba amesisitiza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakati akifunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Sehemu ya Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakiwa kwenye mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akielekea kutembelea mabanda mbalimbali kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya AICC Arusha kwa ajili ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akisikiliza maelezo kuhusu mifumo mbalimbali wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akitembelea mabanda mbalimbali kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akitembelea mabanda mbalimbali kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba


Sehemu ya Washirkiki na Wanakamati wa mkutano wa sita wa Serikali Mtandao wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.

Sehemu ya Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakiwa kwenye mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.

Sehemu ya Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakiwa kwenye mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Wednesday, February 18, 2026

WATUMISHI 14 KUSIMAMISHWA KAZI KWA TUHUMA ZA UBADHIRIFU WA FEDHA MUHEZA, WAZIRI WA UTUMISHI NA TAMISEMI WAZUNGUMZA

Na Veronica Mwafisi-Muheza

Maelekezo yametolewa ya kusimamishwa kazi Watumishi wa umma 14 katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la utawala la halmashauri hiyo.

Kusimamishwa kazi kwa watumishi hao, kunatokana na utekelezaji wa maelekezo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba aliyoyatoa wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya hivi karibuni katika Mkoa wa Tanga ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza leo tarehe 19.02.2026 Wilayani Muheza, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe wamesema Katika ziara aliyoifanya Waziri Mkuu mkoani Tanga, pamoja na shughuli nyingine, alitembelea na kukagua jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Muheza na kubaini uwepo wa changamoto katika utekelezaji wa mradi huo ambapo aliwaelekeza kuchukua hatua za haraka ili kubaini wahusika na kuchukua hatua stahiki.

Katika kutekeleza maelekezo ya Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, majukumu ya ofisi yake pamoja na ya Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI ni kuratibu masuala ya utumishi wa umma nchini, kwani Ofisi ya Rais UTUMISHI ndio mwajiri mkuu anayewapangia watumishi vituo vya kazi na vituo hivyo vinasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, linapotokea jambo linalohusu masuala ya kiutumishi, yeye Waziri wa UTUMISHI na Waziri wa TAMISEMI wanahusika kusimamia na kuratibu utekelezaji wa majukumu ya watumishi wa umma na ndio maana Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Nchemba amewaelekeza kushughulikia changamoto hiyo ya utekelezaji wa mradi wa jengo hilo.

Maelekezo aliyoyatoa Waziri Mkuu kwa mawaziri hao, yalitokana na kubaini uwepo wa changamoto ya upotevu wa nondo 700 zenye thamani ya Shilingi 9,200,000.00 zilizonunuliwa kutoka Saifi Store, upotevu wa marine board 192 zenye thamani ya Shilingi 7,800,000.00, upotevu wa mifuko ya saruji 300 yenye thamani ya shilingi 4,400,000.00, kufanyika malipo ya kiasi cha Shilingi 110,600,000.00 kwa mhandisi mshauri Edge Engineering and Consulting Limited bila uwepo wa Mkataba na Shilingi 343,900,000.00 kutumika nje ya mradi kwa kulipana posho.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amefafanua kuwa, kufuatia malekezo ya Waziri Mkuu, yeye pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete walipeleka wataalam kutoka pande zote mbili ili kushughulikia suala hili katika hatua za awali.

Mhe. Prof. Shemdoe amesema kwa mujibu wa Kanuni ya 37(1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2022, amemuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza akisimamiwa na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga kuwapumzisha kutekeleza majukumu yao watumishi hao 14 ili kupisha uchunguzi.

Mhe. Prof. Shemdoe, ameongeza kuwa, kwa mujibu Kanuni ya 36 ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2022 amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, kuunda Kamati ya Uchunguzi wa Awali ili kuwachunguza watumishi hao 14 wanaotumiwa kukwamisha utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la utawala.

Aidha, amemuelekeza Katibu Tawala wa Mkoa kufuatilia na kumsimamia Mkurugenzi wa Halmashauri kupata timu ya watu waadilifu watakaokuwa kwenye kamati hiyo ili kufanya uchunguzi wa suala hilo.

Pia, amemtaka Mkurugenzi huyo, kuchukua hatua za kinidhamu kwa watumishi waliotajwa na ambao hawakutajwa endapo watabainika kuhusika katika kusababisha changamoto katika utekelezaji wa mradi huo baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.

Aidha, kwa wahusika waliotajwa katika taarifa za awali wasio watumishi Umma, Prof. Shemdoe amevielekeza vyombo vinavyohusika na uchunguzi ikiwemo Jeshi la Polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuchukua hatua stahiki dhidi yao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza wakati wa kikao kilichofanyika mkoani Tanga kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la utawala la halmashauri hiyo.


Sehemu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza nao wakati wa kikao kilichofanyika mkoani Tanga kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la utawala la halmashauri hiyo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza wakati wa kikao kilichofanyika mkoani Tanga kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la utawala la halmashauri hiyo.


Sehemu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza nao wakati wa kikao kilichofanyika mkoani Tanga kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la utawala la halmashauri hiyo.




TUNAWATAKIA WAISLAMU WOTE MFUNGO MWEMA WA RAMADHANI




 

TUNAWATAKIA WAKRISTO WOTE KWARESMA NJEMA


 

Tuesday, February 17, 2026

MSIHAMISHE WATUMISHI KWA KIGEZO CHA KUTOFAA KIUTENDAJI MUWAJENGEE UWEZO “Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Kusiluka”

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka amewataka waajiri katika taasisi za umma kuacha tabia ya kuomba kuhamisha watumishi kutoka katika vituo vyao vya kazi na kuwapeleka kwingine kwa kisingizio cha kutokuwa na uwezo kiutendaji.

Balozi Dkt. Kusiluka amepiga marufuku hiyo leo tarehe 17 Februari, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha wakati akifungua rasmi mkutano wa sita wa Serikali Mtandao.

Amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya waajiri kupenda kuwahamisha watumishi na kutaka kupewa mbadala ambapo amemuelekeza Katibu Mkuu-UTUMISHI kutofanya hivyo.  “Utumishi msifanye mambo hayo ya kuhamisha hamisha watumishi kwa kigezo cha kutofaa kiutendaji badala yake wapewe mafunzo ili waendane na utendaji kazi wa taaluma husika,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa, mtumishi ambaye hayuko vizuri kiutendaji ukimuhamishia kituo kingine hawezi kubadilika kwani kinachotakiwa hapo ni kujengewa uwezo na jukumu hilo ni la mwajiri wa taasisi husika.

Amesema kila mtumishi anatakiwa kupata mafunzo ya mara kwa mara lakini ni muhimu zaidi kwa wataalamu wa TEHAMA kwani teknolojia imekuwa ikibadilika, hivyo mtaalam wa TEHAMA asipopata mafunzo ya mara kwa mara ataachwa nyuma.

Ameongeza kuwa kujengewa uwezo wa kitaaluma unaweza kutekelezwa kwa namna mbalimbali ikiwemo kufanya vikao vya ndani na kuwasikiliza au kuwapeleka katika taasisi nyingine za sekta binafsi kwa mkataba.

Aidha, amewaelekeza waajiri kuweka vizuri utaratibu wa majukumu yao ili kuwarahisishia wataalamu wa TEHAMA pindi wanapotaka kubuni na kusanifu mifumo ya TEHAMA.

Amesema TEHAMA ni kipaumbele cha Serikali na hata Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Viongozi wengine wamekuwa wakitumia TEHAMA kwa kiwango kikubwa katika utekelezaji wa majukumu ya serikali.

Ameipongeza e-GA kwa kubuni na kusanifu mifumo mbalimbali ya TEHAMA ambayo imekuwa ikirahisisha utendaji kazi wa kila siku serikalini. “Tuliokuwa katika Utumishi wa Umma tangu zamani tunaona, kulikuwa na vikwazo vingi wakati tunataka kuanza kusanifu mifumo yetu, kuna watu wakasema hatutaweza, lakini sasa tumeweza, niwapongeze sana e-GA, niwasisitize kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolijia ili tusiachwe nyuma,” Katibu Mkuu Kiongozi amesisitiza.

Amesema, Serikali inathamini sana mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya TEHAMA na ndio maana imekuwa ikishirikiana nao. “tuendelee kufanya kazi pamoja kwani tunajenga nchi moja, sote tunawahudumia wananchi, tuendeleze ushirikiano ili tuwahudumie wananchi kikamilifu,” amesisitiza na kutoa angalizo la kusanifu mifumo yenye kuleta tija kwa taifa badala ya kusanifu mifumo itakayosababisha uvunjifu wa Amani. “Ninyi ndio mnaobuni na kusanifu mifumo, hivyo mbuni vitu ambavyo havileti shida kwa jamii na kuwaongoza vijana wetu kutumia mifumo hiyo kwa usahihi.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Ikulu, kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi kuzungumza na washiriki wa mkutano huo, Bw. Xavier Daudi ambaye ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora amesema katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kasi ya teknolojia, Serikali Mtandao imeendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha utawala bora na ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema Serikali itaendelea kuimarisha Mamlaka ya Serikali Mtandao, kwa kuitengea rasilimali na kuimarisha miundombinu ya TEHAMA kulingana na mahitaji na mabadiliko ya teknolojia.

Awali akitoa neno la utangulizi , Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba amesema e-GA imeendelea kutekeleza jukumu lake la msingi la kuratibu, kusimamia na kukuza jitihada za Serikali Mtandao, kwa kuhakikisha matumizi ya TEHAMA Serikalini yanakuwa shirikishi, salama, yanazingatia Sheria, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, ili kuleta tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi kama ilivyoelekezwa katika Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya Mwaka 2019.

Mhandisi Ndomba alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuwekeza katika sekta ya TEHAMA na kuiwezesha Mamlaka kutekeleza majukumu yake ikiwemo,  ujenzi wa Mfumo unaowezesha Mifumo ya Serikali Kuwasiliana na Kubadilishana taarifa, ujulikanao kama Government Enterprises Service Bus (GovESB). Ubadilishanaji wa taarifa kupitia mfumo huu, umechochea kuongezeka kwa ufanisi wa utendaji kazi katika taasisi za umma na utoaji wa huduma kwa wananchi.


Kikao kazi hicho cha siku tatu kinachoongozwa na Kaulimbiu isemayo Kuboresha Utendaji wa Serikali kwa Kuimarisha Utoaji wa Huduma za Umma Kupitia Mifumo Salama na Jumuishi ya Serikali Mtandao” kimewashirikisha zaidi ya wadau1400 na mada 14 kuhusu serikali mtandao zitawasilishwa kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa masuala ya TEHAMA nchini.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akizungumza na Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakati akifungua mkutano wa sita wa Serikali Mtandao katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Sehemu ya Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakiwa kwenye mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka (hayupo pichani) kufungua mkutano wa sita wa Serikali Mtandao ulioshirikisha Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini uliofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka (katikati mstari wa mbele) akifuatilia jambo wakati wa mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka (katikati) akisikiliza maelezo kuhusu mifumo mbalimbali kutoka kwa Maafisa wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kabla ya kufungua mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akimsikiliza Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka (hayupo pichani) wakati akifungua mkutano wa sita wa Serikali Mtandao katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.



Monday, February 16, 2026

WATUMISHI WA UMMA, WANANCHI WAPEWA NYENZO YA KUWASILIANA NA SERIKALI

Na. Veronica Mwafisi- Dodoma.

Tarehe 16 Februari, 2026 

“Mfumo wa e-Mrejesho unalenga kuboresha huduma zinazotolewa na Serikali na ni sehemu ya utekelezaji wa dhana ya Utawala Bora ambayo inajali maslahi ya wengi, kuwa na uwazi, kupiga vita dhidi ya rushwa, kuleta haki na usawa na kuhimiza uwajibikaji”.


Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Uzingatiaji wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Janet Mishinga alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo jijini Dodoma.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia Idara ya Usimamizi Maadili imewahimiza Watumishi wa Umma na Wananchi kutumia Mfumo wa Kielektroni wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi Serikalini (e-Mrejesho) ili kuongeza ufanisi katika kushughulikia mrejesho wa masuala mbalimbali ya kiutumishi na kuboresha huduma kwa umma.


Aidha Bi. Mishinga alifafanua kuwa, ufuatiliaji wa utekelezaji wa mfumo wa e-Mrejesho una lengo la kubaini mafanikio na changamoto ili kuimarisha uadilifu katika kushughulikia mrejesho wa wananchi ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya utendaji wa taasisi katika kuhudumia wananchi.

Pia, alibainisha kuwa utaratibu wa kushughulikia mrejesho kuhusu mfumo huo unaongeza ushirikishwaji kwa watumishi wa umma na wananchi.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto) akifuatilia wasilisho la mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hutolewa kila siku ya Jumatatu kwenye ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Uzingatiaji wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Janet Mishinga akifafanua jambo alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo jijini Dodoma.


Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Wakurugenzi Wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. Wengine ni Watumishi wa ofisi hiyo.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.